< 1 Samuel 3 >

1 Or, le jeune Samuel servait l'Éternel, en présence d'Héli; et la parole de l'Éternel était rare en ces jours-là, et les visions n'étaient pas communes.
Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
2 Et il arriva un jour qu'Héli était couché en son lieu. Or ses yeux commençaient à se ternir, et il ne pouvait plus voir.
Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
3 La lampe de Dieu n'était pas encore éteinte, et Samuel était couché dans le temple de l'Éternel, où était l'arche de Dieu;
Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
4 Alors l'Éternel appela Samuel, et il répondit: Me voici!
Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
5 Et il courut vers Héli, et lui dit: Me voici, car tu m'as appelé. Mais Héli dit: Je n'ai point appelé; retourne-t'en, et couche-toi. Et il s'en alla et se coucha.
Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
6 Et l'Éternel appela encore Samuel, et Samuel se leva et s'en alla vers Héli, et dit: Me voici, car tu m'as appelé. Et Héli dit: Mon fils, je n'ai point appelé; retourne-t'en et couche-toi.
Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
7 Or, Samuel ne connaissait point encore l'Éternel, et la parole de l'Éternel ne lui avait point encore été révélée.
Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 Et l'Éternel appela encore Samuel pour la troisième fois; et il se leva, et s'en alla vers Héli, et dit: Me voici, car tu m'as appelé. Et Héli comprit que l'Éternel appelait cet enfant.
Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
9 Alors Héli dit à Samuel: Va, et couche-toi; et si l'on t'appelle, tu diras: Parle, Éternel; car ton serviteur écoute. Samuel s'en alla donc, et se coucha en son lieu.
Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
10 Et l'Éternel vint, et se tint là, et appela, comme les autres fois, Samuel, Samuel! Et Samuel dit: Parle; car ton serviteur écoute.
Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
11 Alors l'Éternel dit à Samuel: Voici, je vais faire en Israël une chose que nul ne pourra entendre sans que ses deux oreilles lui tintent;
Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
12 En ce jour-là, j'exécuterai contre Héli tout ce que j'ai dit contre sa maison; je commencerai et j'achèverai.
Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
13 Car je l'ai averti que j'allais punir sa maison pour jamais, à cause de l'iniquité qu'il a connue, et par laquelle ses fils se sont rendus infâmes, sans qu'il les ait réprimés.
Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
14 C'est pourquoi, j'ai juré à la maison d'Héli que jamais l'iniquité de la maison d'Héli ne sera expiée, ni par sacrifice, ni par oblation.
Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
15 Et Samuel demeura couché jusqu'au matin, puis il ouvrit les portes de la maison de l'Éternel. Or, Samuel craignait de déclarer cette vision à Héli.
Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
16 Mais Héli appela Samuel, et dit: Samuel, mon fils;
lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
17 Et il répondit: Me voici! Et Héli dit: Quelle est la parole qu'il t'a adressée? Je te prie, ne me la cache point. Que Dieu te traite avec la dernière rigueur, si tu me caches un seul mot de tout ce qu'il t'a dit.
Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
18 Samuel lui déclara donc toutes ces paroles, et il ne lui cacha rien. Et Héli répondit: C'est l'Éternel, qu'il fasse ce qui lui semblera bon!
Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
19 Et Samuel devenait grand, et l'Éternel était avec lui, et il ne laissa tomber à terre aucune de ses paroles.
Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
20 Et tout Israël, depuis Dan jusqu'à Béer-Shéba, connut que Samuel était établi prophète de l'Éternel.
Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
21 Et l'Éternel continua d'apparaître à Silo; car l'Éternel se manifestait à Samuel, à Silo, par la parole de l'Éternel.
Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.

< 1 Samuel 3 >