< 1 Rois 12 >

1 Or Roboam se rendit à Sichem; car tout Israël était venu à Sichem pour l'établir roi.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Israeli yote walikuwa wameenda Shekemu kumfanya awe mfalme.
2 Et quand Jéroboam, fils de Nébat, l'apprit, il était encore en Égypte où il s'était enfui de devant le roi Salomon, et il demeurait en Égypte.
Ikatokea kuwa Yeroboamu mwana wa Nebati akayasikia haya (Kwa kuwa alikuwa bado yuko Misri, ambako alikuwa amekimbilia kumkwepa mfalme Sulemani), Kwani Yeroboamu alikuwa anaishi Misri.
3 Mais on l'envoya appeler. Ainsi Jéroboam et toute l'assemblée d'Israël vinrent et parlèrent à Roboam, en disant:
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita, na Yeroboamu pamoja na mkutano wote wa Israeli wakaja wakamwambia Rehoboamu,
4 Ton père a mis sur nous un joug pesant; mais toi, allège maintenant cette rude servitude de ton père et ce joug pesant qu'il nous a imposé, et nous te servirons.
Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito. Sasa ifanye kazi ngumu ya baba yako kuwa nyepesi kuliko nira ngumu ambayo baba yako alituwekea, nasi tutakutumikia.”
5 Et il leur répondit: Allez, et, dans trois jours, revenez vers moi. Ainsi le peuple s'en alla.
Naye Rehobiamu akawaambia, “Ondokeni kwa siku tatu, kisha nirudieni.” Kwa hiyo watu wakaondoka.
6 Et le roi Roboam consulta les vieillards qui avaient été auprès de Salomon, son père, pendant sa vie, et il leur dit: Quelle réponse me conseillez-vous de faire à ce peuple?
Mfalme Rehoboamu akatafuta ushauri kwa wazee waliokuwa wamesimama mbele ya Sulemani baba yake wakati wa uhai wake, naye akasema, “mnanishauri niwajibuje hawa watu?”
7 Et ils lui parlèrent en ces termes: Si aujourd'hui tu rends ce service à ce peuple, si tu leur cèdes, et leur réponds par de bonnes paroles, ils seront tes serviteurs à toujours.
Nao wakamwambia, “Kama wewe utakuwa mtumishi wa hawa watu na akawatumikia, na akawapa majibu ya maneno mema, ndipo watakapokuwa watumishi wako daima.”
8 Mais il ne suivit pas le conseil que les vieillards lui avaient donné; et il consulta les jeunes gens qui avaient grandi avec lui et qui se tenaient devant lui;
Lakini Rehoboamu akapuuzia ushauri aliopewa na wazee na akaenda kuomba ushauri kwa vijana ambao alikua pamoja nao wakasimama mbele yake.
9 Et il leur dit: Que me conseillez-vous de répondre à ce peuple qui m'a parlé et m'a dit: Allège le joug que ton père a mis sur nous?
Akawaambia, “Mnanipa ushauri gani ili niweze kuwajibu hawa watu waliosema nami kwamba, 'ifanye nyepesi nira ambayo baba yako alituwekea'”
10 Alors les jeunes gens qui avaient grandi avec lui, lui parlèrent et lui dirent: Tu parleras ainsi à ce peuple qui t'est venu dire: Ton père a mis sur nous un joug pesant, mais toi, allège-le; tu leur parleras ainsi: Mon petit doigt est plus gros que les reins de mon père.
Wale vijana waliokua pamoja na Rehoboamu wakamjibu, wakisema, “Waambie hawa watu kuwa baba yako Sulemani aliifanya nira yenu kuwa nzito lakini ninyi wenyewe mnaweza kuifanya rahisi. Uwaambie hivi, 'Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 Or, mon père vous a imposé un joug pesant; mais moi, je rendrai votre joug plus pesant encore. Mon père vous a châtiés avec des fouets; mais moi, je vous châtierai avec des fouets garnis de pointes.
Kwa hiyo sasa, ingawa baba yangu aliwatwika kongwa zito, Mimi nitaiongeza kongwa lenu. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeredi, Lakini mimi nitawaadhibu kwa nge.'”
12 Trois jours après, Jéroboam, avec tout le peuple, vint vers Roboam, suivant ce que le roi leur avait dit: Revenez vers moi dans trois jours.
Kwa hiyo siku ya tatu Yeroboamu na watu wote wakaja kwa Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amewaelekeza aliposema, “mrudi kwangu siku ya tatu.”
13 Mais le roi répondit durement au peuple, délaissant le conseil que les vieillards lui avaient donné.
Naye mfalme akawaambia wale watu kwa ukali na akapuuzia ushauri wa wale wazee ule waliokuwa wamempatia.
14 Et il leur parla suivant le conseil des jeunes gens, et leur dit: Mon père a mis sur vous un joug pesant; mais moi, je rendrai votre joug plus pesant encore. Mon père vous a châtiés avec des fouets; mais moi, je vous châtierai avec des fouets garnis de pointes.
Akawaambia akifuata ushauri wa wale vijana; akasema, “Baba yangu aliwatwika kongwa zito, lakini mimi nitaongeze kongwa lenu. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeredi, mimi nitawaadhibu kwa nge.”
15 Le roi n'écouta donc point le peuple; car cela était ainsi dispensé par l'Éternel, pour ratifier la parole qu'il avait adressée par le ministère d'Achija, le Silonite, à Jéroboam fils de Nébat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza wale watu, kwa kuwa ilikuwa zamu ya tukio lililoletwa na BWANA, ili kwamba aweze kulitimiza neno lake ambalo alikuwa amelisema kupitia Ahiya.
16 Et, quand tout Israël vit que le roi ne les écoutait pas, le peuple fit cette réponse au roi: Quelle part avons-nous avec David? Nous n'avons point d'héritage avec le fils d'Isaï. A tes tentes, Israël! Maintenant, David, pourvois à ta maison! Ainsi Israël s'en alla dans ses tentes.
Israeli yote ilipoona kuwa mfalme hakuwasikiliza, watu wakamjibu wakimwambia, “Je, tuna sehemu gani kwa Daudi? Hatuna urithi kwa mwana wa Yese! Nenda kwenye hema zako, ewe Israeli. Sasa tazama kwenye nyumba yako, Daudi.” Kwa hiyo Israeli akarudi kwenye hema zake.
17 Mais quant aux enfants d'Israël qui habitaient les villes de Juda, Roboam régna sur eux.
Lakini kwa watu wa Israeli waliokuwa wakiishi kwenye miji ya Yuda, Rehoboamu akawa mfalme juu yao.
18 Cependant le roi Roboam envoya Adoram qui était préposé aux impôts; mais tout Israël le lapida, et il mourut. Et le roi Roboam se hâta de monter sur son char pour s'enfuir à Jérusalem.
Kisha mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa juu ya shokoa, lakini Waisraeli wote wakampiga kwa mawe wakamwua kwa mawe. Mflme Rehoboamu akakimbia haraka kwa gari lake kwenda Yerusalemu.
19 C'est ainsi qu'Israël s'est rebellé contre la maison de David jusqu'à ce jour.
Kwa hiyo Israeli wakawa wapinzani dhidi ya nyumba ya Daudi mpaka leo.
20 Aussitôt que tout Israël eut appris que Jéroboam était de retour, ils l'envoyèrent appeler dans l'assemblée, et ils l'établirent roi sur tout Israël. Aucune tribu ne suivit la maison de David, que la seule tribu de Juda.
Ndipo Israeli yote waliposikia kuwa Yeroboamu alikuwa amerudi, walimwita kwenye kusanyiko lao wakamweka kuwa mfalme wa Israeli. Hapakuwepo na mtu aliyeifuata familia ya Daudi, isipokuwa tu kabila la Yuda.
21 Roboam, étant arrivé à Jérusalem, assembla toute la maison de Juda et la tribu de Benjamin, cent quatre-vingt mille hommes de guerre choisis, pour combattre contre la maison d'Israël, pour ramener le royaume à Roboam, fils de Salomon.
Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akawakusanya wote wa nyumba ya Yuda na kabila la Benjamini; walichaguliwa wanaume wanajeshi 180, 000 ili wapigane na nyumba ya Israeli, kwa lengo la kurudisha ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Sulemani.
22 Mais la parole de Dieu fut adressée à Shémaeja, homme de Dieu, en ces termes:
Lakini neno la Mungu likamjia Shemaya, mtu wa Mungu; likisema,
23 Parle à Roboam, fils de Salomon, roi de Juda, et à toute la maison de Juda et de Benjamin, et au reste du peuple, et dis-leur:
“Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, na kwa nuymba yote ya Yuda na Benjamini, na kwa watu wote; uwaambie,
24 Ainsi a dit l'Éternel: Vous ne monterez point et vous ne combattrez point contre vos frères, les enfants d'Israël. Retournez-vous-en, chacun dans sa maison, car ceci vient de moi. Et ils obéirent à la parole de l'Éternel, et ils s'en retournèrent, selon la parole de l'Éternel.
“BWANA asema hivi, Usipigane wala kuwavamia ndugu zako watu wa Israeli. Kila mtu lazima arudi nyumbani kwake, kwa kuwa jambo hili nimelisababisha mimi.” Kwa hiyo wakalisikiliza neno la BWANA na wakrudi nyumbani kwa njia zao na wakalitii neno lake.
25 Or Jéroboam bâtit Sichem en la montagne d'Éphraïm et y habita; puis il sortit de là et bâtit Pénuël.
Kisha Yeroboamu akaijenga Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na akaishi huko. Akatoka huko na kuijenga Penueli.
26 Et Jéroboam dit en son cœur: Le royaume pourrait bien maintenant retourner à la maison de David.
Yeroboamu akafikiri moyoni mwake, “Sasa ufalme utarudi kwenye nyumba ya Daudi.
27 Si ce peuple monte pour faire des sacrifices dans la maison de l'Éternel à Jérusalem, le cœur de ce peuple se tournera vers son seigneur Roboam, roi de Juda; ils me tueront, et ils retourneront à Roboam, roi de Juda.
Kama hawa watu wataenda kutoa sadaka kwenye hekalu la BWANA kule Yerusalemu, basi mioyo ya hawa watu itarudi tena kwa bwana wao, kwa Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua na kurudi kwa Rehoboamu mfalme wa Yuda.”
28 Et le roi, ayant pris conseil, fit deux veaux d'or et dit au peuple: C'est trop pour vous de monter à Jérusalem. Voici tes dieux, ô Israël, qui t'ont fait monter hors du pays d'Égypte!
Kwa hiyo mfalme Yeroboamu akatafuta ushauri na akafanya ndama wawili wa dhahabu; akawaambia watu, “Ni vigumu sana kwenu kwenda Yerusalemu. Tazameni, hawa ndiyo miungu yenu, Ee Israeli, iliyowatoa toka nchi ya Misri.”
29 Et il en mit un à Béthel, et plaça l'autre à Dan.
Akamweka mmoja Betheli na mwingine Dani.
30 Et ce fut une occasion de péché; car le peuple alla même, devant l'un des veaux, jusqu'à Dan.
Kwa hiyo jambo hili likawa dhambi. Watu wakaenda kwa huyo na wengine kwa hawa, mpaka huko Dani.
31 Il fit aussi des maisons dans les hauts lieux; et il établit des sacrificateurs pris de tout le peuple et qui n'étaient pas des enfants de Lévi.
Yeroboamu akajenga nyumba mahali pa juu na kufanya makuhani kutoka kwa watu wote, ambao hawakuwa wana wa Lawi.
32 Et Jéroboam fit une fête au huitième mois, le quinzième jour du mois, comme la fête qu'on célébrait en Juda, et il offrit des sacrifices sur l'autel. Il fit ainsi à Béthel, sacrifiant aux veaux qu'il avait faits; et il établit à Béthel les sacrificateurs des hauts lieux qu'il avait faits.
Yeroboamu akafanya sikukuu katika mwezi wa nane, katika siku ya kumi na tano ya mwezi, kama sikukuu ambayo iko Yuda, na akaenda juu kwenye madhabahu. Akafanya hivyo kule Betheli, akawatolea sadaka wale ndama aliokuwa amewatengeneza, na akaweka kuhani huko Betheli mahali pa juu alipokuwa amepatengeneza.
33 Et le quinzième jour du huitième mois, du mois qu'il avait imaginé de lui-même, il offrit des sacrifices sur l'autel qu'il avait fait à Béthel, et il fit une fête pour les enfants d'Israël, et monta sur l'autel pour offrir le parfum.
Yeroboamu akapanda kwenda kwenye madhabahu ambayo aliitengeneza kule Betheli katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, ndio mwezi aliokuwa amefikiri katika akili yake; akafanya sikukuu kwa watu wa Israeli n a akaenda madhabahuni kufukiza uvumba.

< 1 Rois 12 >