< 1 Rois 11 >

1 Or, le roi Salomon aima plusieurs femmes étrangères, outre la fille de Pharaon: des Moabites, des Ammonites, des Iduméennes, des Sidoniennes et des Héthiennes,
Basi mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni: binti wa Farao na wanawake wa Wamoabu, Waamori, Waedomu, Wasidoni, na Wahiti - Haya na
2 D'entre les nations dont l'Éternel avait dit aux enfants d'Israël: Vous n'irez point chez elles, et elles ne viendront point chez vous; certaine-ment elles détourneraient votre cœur pour suivre leurs dieux. Salomon s'attacha à ces nations par l'amour.
mataifa ambayo BWANA alikuwa amewaambia Waisraeli kwamba, “Msiwaoe, wala binti zenu kuolewa nao, kwani kwa hakika wataigeuza mioyo yenu ili mfuate miungu yao.” Lakini Sulemani aliwapenda wanawake hao.
3 Il eut donc pour femmes sept cents princesses, et trois cents concubines; et ses femmes détournèrent son cœur.
Sulemani alikuwa na wanawake halali mia saba na masuria mia tatu. Wake zake waliugeuza moyo wake.
4 Et il arriva, au temps de la vieillesse de Salomon, que ses femmes détournèrent son cœur après d'autres dieux; et son cœur ne fut pas intègre avec l'Éternel son Dieu, comme le cœur de David, son père.
Kwa kuwa Sulemani alipozeeka, wake zake waliugeuza moyo wake kwa miungu mingine; hakuutoa moyo wake wote kwa BWANA, Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 Et Salomon suivit Astarté, divinité des Sidoniens, et Milcom, l'abomination des Ammonites.
Kwani Sulemani alimfuata Ashtoreth, mungu mke wa Wasidoni, na alimfuata Milkom, ambayo ni sanamu chukizo ya Waamori.
6 Ainsi Salomon fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et il ne suivit pas pleinement l'Éternel, comme David, son père.
Sulemani akafanya maovu mbele ya BWANA; hakumfuata BWANA kwa moyo wake wote, kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 Et Salomon bâtit un haut lieu à Kémos, l'idole abominable de Moab, sur la montagne qui est vis-à-vis de Jérusalem; et à Molec, l'abomination des enfants d'Ammon.
Kisha Sulemani akajenga mahali pa juu pa Kemoshi, ambayo ni sanamu chukizo ya Wamoabu, mashariki mwa Yerusalemu juu ya kilima, na vivyo hivyo na Moleki, Sanamu chukizo ya Waamoni.
8 Il en fit de même pour toutes ses femmes étrangères, qui offraient de l'encens et des sacrifices à leurs dieux.
Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa sadaka kwa miungu yao.
9 Et l'Éternel fut indigné contre Salomon, parce qu'il avait détourné son cœur de l'Éternel, le Dieu d'Israël, qui lui était apparu deux fois,
BWANA alichukizwa na Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umemwacha Mungu wa Israeli, ingawa alikuwa amejionyesha kwake mara mbili
10 Et lui avait même donné ce commandement exprès, de ne point suivre d'autres dieux; mais il n'observa point ce que l'Éternel lui avait commandé.
na kumwamuru juu ya mambo haya, kwamba asiwaendee miungu wengine. Bali Sulemani hakutii kile ambacho BWANA alikuwa amemwamuru.
11 Et l'Éternel dit à Salomon: Puisque tu as agi ainsi, et que tu n'as pas gardé mon alliance et mes ordonnances que je t'avais données, je t'arracherai certainement le royaume et je le donnerai à ton serviteur.
Kwa hiyo BWANA akamwambia Sulemani, “Kwa kuwa umeyafanya haya haukulishika agano langu na maagizo ambayo nilikuamuru, basi nitaugawa ufalme kutoka kwako na kuwapatia watumishi wako.
12 Seulement, pour l'amour de David, ton père, je ne le ferai point pendant ta vie; c'est des mains de ton fils que je l'arracherai.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, sitalifanya hilo wakati wa uhai wako, bali nitaugawa wakati ukiwa chini ya mwanao.
13 Toutefois je n'arracherai pas tout le royaume; j'en donnerai une tribu à ton fils pour l'amour de David, mon serviteur, et pour l'amour de Jérusalem que j'ai choisie.
Bado sitaugawanya ufalme wote; Nitampa mwanao kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu, ambayo nimeichagua.”
14 L'Éternel suscita donc un ennemi à Salomon: Hadad, Iduméen, qui était de la race royale d'Édom.
Kisha BWANA akamwinulia uadui Sulemani, Hadadi Mwedomu. Alikuwa anatoka kwenye familiia ya mfalme wa Edomu.
15 Dans le temps que David était en Édom, lorsque Joab, chef de l'armée, monta pour ensevelir ceux qui avaient été tués, il tua tous les mâles d'Édom.
Daudi alipokuwa Edomu, Yoabu mkuu wa jeshi alikuwa ameenda kuzika mfu, kila mtu aliyekuwa ameuawa kule Edomu.
16 Car Joab demeura là six mois avec tout Israël, jusqu'à ce qu'il eût exterminé tous les mâles d'Édom.
Yoabu na Israeli yote walibaki huko kwa miezi sita mpaka alipokuwa amewaua wanaume wote wa Edomu.
17 Alors Hadad s'enfuit avec quelques Iduméens des serviteurs de son père, pour se retirer en Égypte. Or, Hadad était fort jeune.
Lakini Hadadi alichulukuliwa na Waedomu wengine na watumishi wa baba yake hadi Misri, kuanzia Hadadi alipokuwa mtoto mdogo.
18 Et quand ils furent partis de Madian, ils vinrent à Paran; et ils prirent avec eux des gens de Paran et se retirèrent en Égypte vers Pharaon, roi d'Égypte, qui lui donna une maison, lui assigna de quoi se nourrir, et lui donna aussi une terre.
Waliondoka Midiani wakaja Parani, ambapo walichukuliwa na wanaume mpaka Misri, kwa Farao wa Misri, ambaye alimpa nyumba na ardhi yenye chakula.
19 Et Hadad fut fort dans les bonnes grâces de Pharaon; de sorte qu'il lui fit épouser la sœur de sa femme, la sœur de la reine Thachpénès.
Hadadi alipata neema kubwa machoni pa Farao, kwa hiyoFarao akampatia mke, umbu wa mke wake mwenyewe, umbu la Tapenesi aliyekuwa Malkia.
20 Et la sœur de Thachpénès lui enfanta son fils Guénubath, que Thachpénès sevra dans la maison de Pharaon. Ainsi Guénubath était dans la maison de Pharaon, parmi les fils de Pharaon.
Naye huyo umbu la Tapenesi alimzalia Hadadi mwana. Wakamwita jina lake Genubathi. Tapenesi akamlea katika ikulu ya Farao. Kwa hiyo Genubathi alikulia kwenye ikulu ya Farao pamoja na watoto wa Farao.
21 Or, quand Hadad eut appris en Égypte que David s'était endormi avec ses pères, et que Joab, le chef de l'armée, était mort, il dit à Pharaon: Laisse-moi partir, et je m'en irai en mon pays.
Naye alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kuwa Daudi alishalala na mababu zake na kwamba Yoabu mkuu wa majeshi alishakufa, Hadadi akamwambia Farao, “Acha niondoke nirudi nchini kwangu.”
22 Et Pharaon lui dit: Que te manque-t-il donc auprès de moi, pour que tu demandes ainsi de t'en aller en ton pays? Et il lui répondit: Rien; mais laisse-moi, laisse-moi partir!
Lakini Farao alimwambia, “Umepungukiwa nini kwangu, kwamba sasa unatafuta kurudi nchini kwako?” Naye Hadadi akamjibu, “Hapana kitu lakini tafadhali niache niende.”
23 Dieu suscita encore un ennemi à Salomon: Rézon, fils d'Eljada, qui s'était enfui d'avec son seigneur Hadadézer, roi de Tsoba,
Pia Mungu akamwinulia Sulemani adui mwingine, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri mfalme wa Soba.
24 Et qui assembla des gens contre lui et était chef de bande, lorsque David tua les Syriens. Et ils s'en allèrent à Damas, y habitèrent et y régnèrent.
Rezoni alijikusanyia wanaume naye akawa mkuu wa jeshi dogo, Daudi ali owapiga wanaume wa Soba. Wale wanume Rezoni walienda Dameski kuishi huko, na Rezoni aliitawala Dameski.
25 Rézon fut donc ennemi d'Israël tout le temps de Salomon, outre le mal que fit Hadad; il eut Israël en aversion, et il régna sur la Syrie.
Yeye akawa adui wa Israeli katika siku zote za mfalme Sulemani, zaidi ya madhara ambayo Hadadi alisababisha. Rezoni akawachukia Israeli na akawa juu ya Shamu
26 Jéroboam, fils de Nébat, Éphratien de Tséréda, serviteur de Salomon, dont la mère, femme veuve, s'appelait Tséruha, se révolta aussi contre le roi.
Kisha Yeroboamu mwana wa Nebati, mwefraimu wa Sereda, akida wa Sulemani, ambaye jina la mama yake lilikuwa Serua, mjane, pia akainua mkono wake dhidi ya mfalme.
27 Et voici l'occasion pour laquelle il se révolta contre le roi: Salomon bâtissait Millo et fermait la brèche de la cité de David, son père.
Kisa cha kuinua mkono wake kinyume cha mfalme ilikuwa ni mfalme Sulemani kujenga Milo na kufunga mahali palipobomoka katika mji wa Daudi baba yake.
28 Or, Jéroboam était fort et vaillant; et Salomon, voyant ce jeune homme qui travaillait, l'établit sur toute la corvée de la maison de Joseph.
Yeroboamu alikuwa mtu hodari na shujaa. Sulemani akaona kuwa huyo kijana alikuwa na bidii, kwa hiyo akampa kuwa na mamlaka juu ya wafanyakazi katika nyumba ya Yusufu.
29 Or, il arriva dans ce temps-là que Jéroboam sortit de Jérusalem. Et le prophète Achija, le Silonite, vêtu d'un manteau neuf, le rencontra dans le chemin; et ils étaient eux deux tout seuls dans les champs.
Wakati huo, Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya Mshilo akamkuta barabarani. Sasa Ahiya alikuwa amevaa vazi jipya na kwamba hawa wawili walikuwa pekee yao kondeni.
30 Alors Achija prit le manteau neuf qu'il avait sur lui, et le déchira en douze morceaux;
Kisha Ahiya akalishika lile vazi jipya ambalo alikuwa nalo na akalichana katika vipande kumi na viwili.
31 Et il dit à Jéroboam: Prends pour toi dix morceaux; car ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Voici, je vais déchirer le royaume d'entre les mains de Salomon, et je te donnerai dix tribus;
Akamwambia Yeroboamu. “Chukua vipande kumi, kwani BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Tazama, Nitaugawa ufalme toka katika mkono wa Sulemani nami nitakupa makabila kumi.
32 Mais il aura une tribu, pour l'amour de David, mon serviteur, et de Jérusalem, la ville que j'ai choisie d'entre toutes les tribus d'Israël;
(lakini Sulemani atabaki na kabila moja, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na kwa ajili ya mji wangu Yerusalemu - mji ambao nimeuchagua toka kwenye kabila zote za Israeli),
33 Parce qu'ils m'ont abandonné et se sont prosternés devant Astarté, divinité des Sidoniens, devant Kémos, dieu de Moab, et devant Milcom, dieu des enfants d'Ammon, et n'ont point marché dans mes voies, pour faire ce qui est droit à mes yeux, pour garder mes statuts et mes ordonnances, comme l'a fait David, père de Salomon.
kwa kuwa ameniacha na kumwabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi Mungu wa Wamoabu, na Milikomu mungu wa watu wa Amoni. Wameziacha njia zangu, hawakufanya kilicho chema katika macho yangu, wala hawa kuzishika amri na maagizo yangu, kama alivyofanya Daudi baba yake.
34 Toutefois je n'ôterai rien de ce royaume d'entre ses mains; car, tout le temps qu'il vivra, je le maintiendrai prince, pour l'amour de David, mon serviteur, que j'ai choisi et qui a gardé mes commandements et mes statuts.
Hata hivyo. Stauchukua ufalme wote toka kwenye mkono wa Sulemani. Badala yake, nimemfanya kuwa mtawala katika siku zake zote za uhai wake, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu ambaye nilimchagua, mtu ambaye alizishika amri na maagizo yangu.
35 Mais j'ôterai le royaume d'entre les mains de son fils,
Bali nitauchukua ufalme ukiwa chini ya mkono wa mwanae na nitakupa wewe, makabila kumi.
36 Et je t'en donnerai dix tribus; et je donnerai une tribu à son fils, afin que David, mon serviteur, ait toujours une lampe devant moi à Jérusalem, la ville que j'ai choisie pour y mettre mon nom.
Nitampa kabila moja mwana wa Sulemani ili kwamba Daudi mtumishi wagu atabaki kuwa nuru mbele yangu huko Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua ili niweke jina langu.
37 Je te prendrai donc, tu régneras sur tout ce que souhaitera ton âme, et tu seras roi sur Israël.
Nami nitakuchukua, nawe utatawala ili kutimiza haja yako, nawe utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 Et si tu m'obéis dans tout ce que je te commanderai, si tu marches dans mes voies et que tu fasses tout ce qui est droit à mes yeux, gardant mes statuts et mes commandements, comme a fait David, mon serviteur, je serai avec toi; je te bâtirai une maison stable, comme j'en ai bâti une à David, et je te donnerai Israël.
Kama utasikiliza yote ninayokuagaza, na kama utatembea katika njia zangu na kufanya kinachopendeza mbele ya macho yangu, ukayashika maagizo na amri zangu, kama Daudi mtumishi wangu alivyofanya, ndipo nitakapokuwa na wewe na nitakujengea nyumba ya uhakika, kama niliyomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 Ainsi j'affligerai la postérité de David à cause de cela; mais non pour toujours.
Nitawaadhibu uzao wa Daudi, lakini si milele.”
40 Or Salomon chercha à faire mourir Jéroboam; mais Jéroboam se leva et s'enfuit en Égypte vers Shishak, roi d'Égypte; et il demeura en Égypte jusqu'à la mort de Salomon.
Kwa hiyo Sulemani akajaribu kumwua Yeroboamu. Lakini Yeroboamu akaamka na kukimbilia Misri, Kwa Shishaki mfalme wa Misri, naye akabaki Misri mpaka Sulemani alipokufa.
41 Quant au reste des actions de Salomon, et tout ce qu'il fit, et sa sagesse, cela n'est-il pas écrit au livre des Actes de Salomon?
Na kwa mambo mengine yanayomhusu Sulemani, Yote ambayo alifanya na hekima zake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya
42 Or, le temps que Salomon régna à Jérusalem sur tout Israël fut de quarante ans.
Sulemani? Sulemani alitawala Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka arobaini.
43 Puis Salomon s'endormit avec ses pères, et il fut enseveli dans la cité de David, son père. Et Roboam, son fils, régna à sa place.
Naye akalala na mababu zake na alizikwa katika mji wa Daudi baba yake. Rehoboamu mwanae akawa mfalme mahali pake.

< 1 Rois 11 >