< 1 Chroniques 4 >

1 Fils de Juda: Pharets, Hetsron, Carmi, Hur et Shobal.
Uzao wa Yuda ulikuwa Peresi, Hesroni, Karmi, Huri, na Shobali.
2 Réaja, fils de Shobal, engendra Jachath; Jachath engendra Achumaï et Lahad. Ce sont les familles des Tsoreathiens.
Shobali alikuwa baba wa Reaya. Reaya alikuwa baba wa Yahathi. Yahathi alikuwa baba wa Ahumai na Lahadi. Hawa walikuwa mababu wa koo za Wasorathi.
3 Ceux-ci sont issus du père d'Étham: Jizréel, Jishma et Jidbash; le nom de leur sœur était Hatsélelponi;
Hawa walikuwa mababu wa ukoo katika mji wa Etamu: Yezreeli, Ishma, na Idbashi. Babu yao alikuwa Haselelponi.
4 Pénuel était père de Guédor, et Ézer, père de Husha. Ce sont là les fils de Hur, premier-né d'Éphrata, père de Bethléhem.
Penueli alikuwa babu wa koo katika mji wa Gedori. Ezeri alikuwa muanzilishi wa koo katika Husha. Hawa walikuwa uzao wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi na muanzilishi wa Bethelehemu.
5 Ashur, père de Thékoa, eut deux femmes: Héléa et Naara.
Ashuri baba wa Tekoa alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.
6 Naara lui enfanta Achuzam, Hépher, Théméni et Achashthari. Ce sont là les fils de Naara.
Naara alimzalia Ahuzamu, Heferi, Temeni na Ahashtari. Hawa walikua wana wa Naara.
7 Fils de Héléa: Tséreth, Tsochar et Etnan.
Wana wa Hela walikua Serethi, Ishari, Ethnani,
8 Kots engendra Anub et Hatsobéba et les familles d'Acharchel, fils d'Harum.
na Kozi, alikua baba wa Anubu na Sobeba, na koo zilizotoka kwa Aharheli mwana wa Harumu.
9 Jaebets était plus honoré que ses frères; sa mère l'avait nommé Jaebets (douleur), en disant: C'est avec douleur que je l'ai enfanté.
Yabesi aliheshimika zaidi ya kaka zake. Mama yake alimuita Yabesi. Alisema, “Kwasababu nimemzaa katika huzuni.”
10 Jaebets invoqua le Dieu d'Israël, en disant: Si tu me bénis et que tu étendes mes limites; si ta main est avec moi, et si tu me préserves du malheur, en sorte que je ne sois pas dans la souffrance! Et Dieu accorda ce qu'il avait demandé.
Yabesi akamuita Mungu wa Israeli na kusema, “Kama tu utanibariki mimi, ongeza mipaka yangu, na mkono wako ukuwa juu yangu. Ukifanya hivi utaninusuru na mabaya, ili kwamba niwe huru na huzuni!” Kwa hivyo Mungu akamjalia maombi yake.
11 Kélub, frère de Shucha, engendra Méchir, qui fut père d'Eshthon.
Kelubu kaka wa Shuha akawa baba wa Mehiri, aliyekuwa baba wa Eshtoni.
12 Eshthon engendra la maison de Rapha, Paséach et Théchinna, père de la ville de Nachash. Ce sont là les gens de Réca.
Eshtoni akawa baba wa Beth-Rafa, Pasea, na Tehina, ambaye alianzisha mji wa Nahashi. Hawa ni wanaume walioishi Reka.
13 Fils de Kénaz: Othniel et Séraja. Fils d'Othniel: Hathath.
Wana wa Kenazi walikua Othinieli na Seraia. Wana wa Othinieli walikuwa Hathathi na Meonothai.
14 Méonothaï engendra Ophra. Séraja engendra Joab, père de la vallée des ouvriers; car ils étaient ouvriers.
Meonothai akawa baba wa Ofara, na Seraia akawa baba wa Yohabu, mwanzilishi wa Ge Harashimu, ambao watu wake walikua wahunzi.
15 Fils de Caleb, fils de Jéphunné: Iru, Éla et Naam, et les fils d'Éla, et Kénaz.
Wana wa Kalebu mwana wa Yefune walikua Iru, Ele na Namu. Wana wa Ela alikua Kenazi.
16 Fils de Jehalléléel: Ziph, Zipha, Thiria et Asaréel.
Wana wa Yehaleli walikua Zifi, Zifa, Tiriya, na Azareli.
17 Fils d'Esdras: Jéther, Méred, Épher et Jalon. Une femme de Méred enfanta Miriam, Shammaï, et Jishbach, père d'Eshthémoa.
Wana wa Ezra walikua Yetheri, Meredi, Eferi, na Yaloni.
18 Sa femme, la Juive, enfanta Jéred, père de Guédor, Héber, père de Soco, et Jékuthiel, père de Zanoach. Ceux-là sont les enfants de Bithia, fille de Pharaon, que Méred prit pour femme.
Mke wake Meredi wa Kimisri alimzalia Miriamu, Shamai, na Ishibahi, aliyekua baba wa Eshitemoa. Hawa walikua wana wa Bithia, binti wa Farao, ambaye Meredi alimuoa. Mke wa Kiyahudi wa Meredi alimzalia Yeredi, ambaye alikua baba wa Gedore; Heberi, aliyekua baba wa Soko; na Yekuthieli aliyekua baba wa Zanoa.
19 Fils de la femme d'Hodija, sœur de Nacham: le père de Kéhila le Garmien, et Eshthémoa le Maacathien.
Kati ya watoto wawili wa mke wa Hodia, dada wa Nahamu, mmoja wao kawa baba wa Keila Mgarimite. Mwingine alikua Eshitemoa Mmakathite.
20 Fils de Simon: Amnon, Rinna, Ben-Hanan et Thélon. Fils de Jisheï: Zocheth et Ben-Zocheth.
Wana wa Shimoni walikua Amnoni, Rina, Beni Hanani, na Tilon. Wana wa Ishi walikua Zohethi na Beni Zoheti.
21 Fils de Shéla, fils de Juda: Er, père de Léca, Laëda, père de Marésha, et les familles de la maison des ouvriers en lin fin, de la maison d'Ashbéa,
Uzao wa Shela mwana wa Yuda, Ulikua ni Eri baba wa Leka, Laada baba wa Maresha na koo za wafanyakazi wa kushona kule Beth Ashbea,
22 Et Jokim, et les gens de Cozéba, et Joas et Saraph, qui dominèrent sur Moab, et Jashubi-Léchem. Ces choses sont anciennes.
Yoakimu, Wanaume wa Kozeba, na Yoashi na Sarafi, waliokua na mali huko Moabu, lakini walirudi Bethlehemu. ( Maelezo haya yametoka kwenye nakala za zamani.)
23 C'étaient les potiers et les habitants des plantations et des parcs; ils habitaient là auprès du roi pour son ouvrage.
Baadhi ya watu hawa walikuwa ni wafinyanzi walioishi Netaimu na Gedera na wakawa wafanyakazi wa Mfalme.
24 Fils de Siméon: Némuel, Jamin, Jarib, Zérach, Saül;
Uzao wa Simeoni ulikua Jamini, Jaribu, Zera, na Shauli.
25 Shallum, son fils; Mibsam, son fils, et Mishma, son fils.
Shalumu alikua mwana wa Shauli, Mibisamu mwana wa Shalumu, na Mishima mwana wa Mibisamu.
26 Fils de Mishma: Hamuel, son fils; Zaccur, son fils; Shimeï, son fils.
Ukoo wa Mishima ulikua Hamueli mwana wake, Zakuri mjukuu wake, na Shimei kitukuu chake.
27 Shimeï eut seize fils et six filles; ses frères n'eurent pas beaucoup d'enfants, et toutes leurs familles ne se multiplièrent pas autant que les fils de Juda.
Shimei alikua na wana kumi na sita na mabinti sita. Kaka yake hakua na watoto wengi, Hivyo koo zao hazikuongezeka kwa idadi kubwa kama wato wa Yuda walivyoongezeka.
28 Ils habitèrent à Béer-Shéba, à Molada, à Hatsar-Shual,
Waliishi Beasheba, Molada, na Hazari Shuali.
29 A Bilha, à Etsem, à Tholad,
Pia waliishi Bilha, Ezemu, Toladi,
30 A Béthuel, à Horma, à Tsiklag,
Bethueli, Horma, Zikilagi,
31 A Beth-Marcaboth, à Hatsar-Susim, à Beth-Biréï et à Shaaraïm. Ce furent là leurs villes jusqu'au règne de David.
Bethi Markabothi, Hazari Susimi, Bethi Biri, na Shaaraimu. Hii ilikua miji yao mpaka utawala wa Daudi.
32 Et leurs villages furent Etam, Aïn, Rimmon, Thoken et Assan, cinq villes;
Vijiji vyao vitano vilikua Etamu, Aini, Tocheni, na Ashani,
33 Et tous leurs villages, qui étaient autour de ces villes, jusqu'à Baal. Ce sont là leurs habitations et leur enregistrement généalogique.
pamoja na mipaka ya vijiji kwa umbali wa Baali. Haya yalikua makazi yao, na walitunza kumbukumbu za uzao wao.
34 Meshobab, Jamlec, Josha, fils d'Amats;
Viongozi wa ukoo walikua Meshobabu, Yamileki, Yoshahi mwana wa Amazia,
35 Joël, Jéhu, fils de Joshbia, fils de Séraja, fils d'Asiel;
Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraia mwana wa Asieli,
36 Éljoénaï, Jaakoba, Jeshochaïa, Asaja, Adiel, Jésimiel, Bénaja;
Elioenai, Yaakoba, Yeshohaia, Asaia, Adieli, Yesimieli, Benaia,
37 Ziza, fils de Shiphéï, fils d'Allon, fils de Jédaja, fils de Shimri, fils de Shémaja.
na Ziza mwana wa Shifi mwana wa Aloni mwana wa Yedaia mwana wa Shimiri mwana wa Shemaia.
38 Ceux-là, désignés par leurs noms, étaient princes dans leurs familles, et les maisons de leurs pères se répandirent beaucoup.
Hawa walio orodheshwa kwa majina walikua viongozi wa koo zao, na koo zao ziliongezeka sana.
39 Ils allèrent vers Guédor, jusqu'à l'orient de la vallée, cherchant des pâturages pour leurs troupeaux.
Walienda karibu na Gedori, mashariki mwa bonde, kutafuta malisho ya mifugo yao.
40 Ils trouvèrent des pâturages gras et bons, et une contrée spacieuse en tous sens, tranquille et sûre; car ceux qui habitaient là auparavant descendaient de Cham.
Walipata malisho mengi na mazuri. Nchi ilikua tambarare, tulivu na ya amani. Wahamu waliishi hapo awali.
41 Ces hommes inscrits par leurs noms, vinrent du temps d'Ézéchias, roi de Juda, et frappèrent leurs tentes et les Maonites qui se trouvaient là; ils les vouèrent à l'interdit jusqu'à ce jour, et ils habitèrent à leur place, car il y avait là des pâturages pour leurs troupeaux.
Hao walio orodheshwa hapo kwa majina walikuja katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda, na wakashambulia makazi ya Wahamu na Wameuni, ambao pia walikua hapo. Waliwaangamiza kabisa na kuishi hapo sababu walipata malisho kwa ajili ya mifugo yao.
42 Cinq cents hommes d'entre eux, des enfants de Siméon, s'en allèrent à la montagne de Séir, ayant à leur tête Pélatia, Néaria, Réphaja et Uziel, enfants de Jisheï.
Wanaume mia tano wa kabila la Simeoni walienda katika mlima Seiri, na viongozi wao Pelatia, Nearia, Refaia, na Uzieli, wana wa Ishi.
43 Ils frappèrent le reste des réchappés d'Amalek, et ils ont habité là jusqu'à ce jour.
Waliwashinda wakimbizi wa Waamaleki waliobakia, na wakaishi hapo hadi siku hii.

< 1 Chroniques 4 >