< 1 Chroniques 18 >

1 Il arriva, après cela, que David battit les Philistins et les humilia; et il prit Gath et les villes de son ressort, d'entre les mains des Philistins.
Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
2 Il battit aussi les Moabites; et les Moabites furent assujettis à David, lui payant un tribut.
Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
3 David battit aussi Hadarézer, roi de Tsoba, vers Hamath, lorsqu'il alla établir sa domination sur le fleuve d'Euphrate.
Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
4 David lui prit mille chars, sept mille cavaliers, et vingt mille hommes de pied; il coupa les jarrets des chevaux de tous les chars; mais il en réserva cent chars.
Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
5 Or les Syriens de Damas vinrent au secours de Hadarézer, roi de Tsoba, et David battit vingt-deux mille Syriens.
Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
6 Puis David mit garnison dans la Syrie de Damas; et les Syriens furent assujettis à David, lui payant un tribut. Et l'Éternel gardait David partout où il allait.
Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
7 Et David prit les boucliers d'or qui étaient aux serviteurs de Hadarézer, et les apporta à Jérusalem.
Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
8 Il emporta aussi de Tibechath et de Cun, villes de Hadarézer, une grande quantité d'airain; Salomon en fit la mer d'airain, les colonnes et les ustensiles d'airain.
Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
9 Or, Thohu, roi de Hamath, apprit que David avait défait toute l'armée de Hadarézer, roi de Tsoba;
Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
10 Et il envoya Hadoram, son fils, vers le roi David, pour le saluer et le féliciter de ce qu'il avait combattu Hadarézer, et l'avait défait; car Hadarézer était dans une guerre continuelle avec Thohu. Il envoya aussi toutes sortes de vases d'or, d'argent et d'airain.
Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 Le roi David les consacra aussi à l'Éternel, avec l'argent et l'or qu'il avait emporté de toutes les nations, des Iduméens, des Moabites, des enfants d'Ammon, des Philistins et des Amalécites.
Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
12 Abishaï, fils de Tséruja, battit aussi dix-huit mille Iduméens dans la vallée du Sel.
Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
13 Il mit des garnisons dans l'Idumée, et tous les Iduméens furent assujettis à David; et l'Éternel gardait David partout où il allait.
Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
14 Et David régna sur tout Israël, rendant la justice et le droit à tout son peuple.
Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
15 Joab, fils de Tséruja, commandait l'armée; Joshaphat, fils d'Achilud, était archiviste;
Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
16 Tsadok, fils d'Achitub, et Abimélec, fils d'Abiathar, étaient sacrificateurs, et Shavsha était secrétaire;
Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
17 Bénaja, fils de Jéhojada, était chef des Kéréthiens et des Péléthiens; et les fils de David étaient les premiers auprès du roi.
Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.

< 1 Chroniques 18 >