< Luc 2 >

1 En ce temps-là parut un édit de César-Auguste, portant l'ordre de faire le recensement des habitants de toute la terre.
Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
2 Ce recensement, le premier qui eut lieu, se fit pendant que Quirinius était gouverneur de Syrie.
(Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
3 Tous allaient se faire enregistrer, chacun dans sa ville.
Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
4 Joseph aussi, qui était de la maison et de la famille de David, partit de la ville de Nazareth en Galilée, pour se rendre en Judée, dans la ville de David, appelée Bethléhem,
Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
5 afin de se faire enregistrer avec Marie, qui lui était fiancée, et qui était enceinte.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
6 Pendant qu'ils étaient à Bethléhem, le moment de la délivrance de Marie arriva:
Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
7 elle mit au monde son fils premier-né, l'emmaillota et le coucha dans une crèche, parce qu'il ne se trouvait pas de place pour eux dans l'hôtellerie.
naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
8 Il y avait, dans cette contrée, des bergers qui passaient la nuit en plein air, pour garder leurs troupeaux.
Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
9 Tout à coup un ange du Seigneur leur apparut, et, la gloire du Seigneur les enveloppant de son éclat, ils furent saisis d'une grande frayeur.
Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
10 L'ange leur dit: «Ne craignez point, car je viens vous donner une heureuse nouvelle, qui causera une grande joie à tout le peuple:
Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
11 c'est qu'aujourd'hui, dans la ville de David, il vous est né un Sauveur, qui est Messie, Seigneur;
Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
12 et voici à quel signe vous le reconnaîtrez: vous trouverez un enfant emmailloté, couché dans une crèche.»
Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
13 Soudain, il se joignit à l'ange une troupe nombreuse de l'armée céleste, qui louait Dieu et disait:
Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
14 «Gloire à Dieu dans les lieux très-hauts! Et paix sur la terre parmi les hommes de bonne volonté!»
“Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
15 Lorsque les anges les eurent quittés pour remonter au ciel, les bergers se dirent les uns aux autres: «Allons jusqu’à Bethléhem voir ce qui est arrivé, et que le Seigneur nous a fait savoir.»
Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
16 Ils s'y rendirent en toute hâte, et trouvèrent Marie, Joseph, et le nouveau-né couché dans la crèche.
Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
17 Après l'avoir vu, ils divulguèrent ce qui leur avait été dit touchant ce petit enfant,
Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
18 et tous ceux qui les entendirent, furent étonnés de ce que les bergers disaient.
Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
19 Pour Marie, elle gardait toutes ces paroles et les repassait dans son coeur.
Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
20 Les bergers s'en retournèrent, glorifiant et louant Dieu de tout ce qu'ils avaient entendu et vu, conformément à ce qui leur avait été annoncé.
Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
21 Le huitième jour, on circoncit l'enfant, et on le nomma Jésus, nom que l'ange lui avait donné, avant qu'il eût été conçu dans le sein de sa mère.
Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
22 Et quand, selon la loi de Moïse, le jour de leur purification fut arrivé, les parents le portèrent à Jérusalem, pour le présenter au Seigneur,
Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
23 selon qu'il est écrit dans la Loi: «Tout mâle premier-né sera consacré au Seigneur, »
(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
24 ainsi que pour offrir en sacrifice «une paire de tourterelles ou deux jeunes pigeons, » comme le porte la loi du Seigneur.
na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
25 Or, il y avait à Jérusalem un homme juste et pieux, nommé Syméon, qui vivait dans l'attente de la consolation d'Israël; et le Saint-Esprit reposait sur lui.
Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Il avait été averti par l'Esprit Saint qu'il ne mourrait point avant d'avoir vu l'Oint du Seigneur.
Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
27 Syméon vint au temple par un mouvement de l'Esprit, et quand les parents y apportèrent l'enfant Jésus, pour accomplir à son égard les cérémonies d'usage selon la Loi,
Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
28 il reçut l'enfant dans ses bras, bénit Dieu, et dit:
ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
29 «C'est maintenant, Maître, que, selon ta parole, tu laisses ton serviteur s'en aller en paix;
“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
30 car mes yeux ont vu ton salut,
Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
31 ce salut qui est prêt à paraître devant tous les peuples,
ulioweka tayari machoni pa watu wote,
32 comme une lumière destinée à éclairer les nations, et comme la gloire de ton peuple d'Israël.»
nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 Le père et la mère de l’enfant étaient dans l'admiration des choses qu'on disait de lui.
Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
34 Syméon les bénit, et il dit à Marie, sa mère: «Cet enfant sera cause de la chute et du relèvement de bien des gens en Israël, et il sera un prodige qui rencontrera de la contradiction,
Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
35 afin que les pensées de bien des coeurs soient dévoilées; pour toi, un glaive te traversera l'âme.»
ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
36 Il y avait aussi une prophétesse nommée Anne, fille de Phanuel, de la tribu d'Asser, qui était fort avancée en âge. Après avoir vécu sept ans mariée depuis sa virginité,
Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
37 elle était demeurée veuve, et avait atteint l'âge de quatre-vingt-quatre ans, ne quittant pas le temple, où elle servait Dieu, jour et nuit, dans le jeûne et dans la prière.
Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
38 Étant survenue, elle aussi, en ce même instant, elle se mit à louer le Seigneur, et elle parlait de l'enfant à tous ceux qui, à Jérusalem, attendaient la délivrance.
Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
39 Quand Joseph et Marie eurent achevé d'accomplir toutes les prescriptions de la loi du Seigneur, ils s'en retournèrent en Galilée, dans leur ville de Nazareth.
Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
40 Cependant l'enfant croissait et se fortifiait, rempli de sagesse; et la grâce de Dieu se répandait sur lui.
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 Son père et sa mère allaient tous les ans à Jérusalem, à la fête de Pâque.
Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
42 Quand il eut douze ans, ils y montèrent selon la coutume; et lorsqu'ils s'en retournèrent après les jours de fête,
Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 l'enfant Jésus resta à Jérusalem, sans que Joseph ni sa mère s'en fussent aperçus.
Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
44 Ils firent une journée de chemin, le croyant dans la caravane, et le cherchèrent parmi leurs parents et leurs connaissances;
Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
45 et ne l'ayant point trouvé, ils retournèrent à Jérusalem pour le chercher.
Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
46 Au bout de trois jours, ils le trouvèrent dans le temple, assis au milieu des docteurs, les écoutant et leur adressant des questions;
Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 et tous ceux qui l'entendaient étaient ravis de son intelligence et de ses réponses.
Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
48 Quand Joseph et Marie le virent, ils furent frappés d'étonnement, et sa mère lui dit: «Mon enfant, pourquoi te conduire ainsi avec nous? Nous te cherchions, ton père et moi, étant fort en peine.»
Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
49 Il leur dit: «Pourquoi me cherchiez-vous? Ne saviez-vous pas que je dois être dans la maison de mon Père?»
Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 Et ils ne comprirent point ce qu'il leur disait.
Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
51 Il descendit avec eux, allant à Nazareth. Il leur était soumis. Sa mère gardait soigneusement toutes ces choses dans son coeur;
Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
52 et Jésus croissait en sagesse, en stature et en grâce, devant Dieu et devant les hommes.
Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

< Luc 2 >