< Actes 20 >

1 Lorsque le tumulte eut cessé, Paul, ayant réuni les disciples et les ayant embrassés, partit pour aller en Macédoine.
Baada ya ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha kuwaaga na akaondoka kwenda Makedonia.
2 Il parcourut cette province en adressant aux disciples de nombreuses exhortations, et se rendit en Grèce.
Naye akiishakupita mikoa hiyo na alikuwa akiwatia moyo waamuni, akaingia Uyunani.
3 Après un séjour de trois mois, il se disposait à s'embarquer pour la Syrie, mais, les Juifs lui ayant dressé des embûches, il prit le parti de s'en retourner par la Macédoine.
Baada ya yeye kuwa pale kwa muda wa miezi mitatu, njama ziliundwa dhidi yake na Wayahudi alipokuwa akikaribia kusafiri kwa njia ya bahari kuelekea Shamu, hivyo aliazimu kurudi kupitia Makedonia.
4 Sopater, fils de Pyrrhus, de Bérée, raccompagna jusqu'en Asie, avec Aristarque et Secundus de Thessalonique, Caïus de Derbe et Timothée, Tychique et Trophime d'Asie;
Walioandamana naye hadi Asia walikuwa Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea; Aristariko na Sekundo, wote kutoka waamini wa Wathesalonike; Gayo wa Derbe; Timotheo; Tikiko na Trofimo kutoka Asia.
5 ceux-ci ayant pris les devants, nous attendirent à Troas.
Lakini watu hawa wamekwisha tangulia na walikuwa wanatungojea kule Troa.
6 Pour nous, nous partîmes de Philippes après les jours des pains sans levain, et au bout de cinq jours de navigation, nous les rejoignîmes à Troas, et nous y demeurâmes sept jours.
kwa njia ya Bahari kutoka Filipi baada ya siku za mikate isiyotiwa chachu, na katika siku tano tukawafikia huko Troa. Tulikaa huko kwa siku saba.
7 Le premier jour de la semaine, comme nous étions assemblés pour rompre le pain, Paul, qui devait partir le lendemain, s'entretint avec les disciples, et prolongea son discours jusqu’à minuit.
Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekusanyika pamoja ili kuumega mkate, Paulo alizungumza na Waamini. Alikuwa akipanga kuondoka kesho yake, hivyo akaendelea kuongea hadi usiku wa manane.
8 Il y avait beaucoup de lampes dans la salle haute où nous étions assemblés.
Kulikuwa na taa nyingi katika chumba cha juu ambapo tulikuwa tumekusanyika pamoja.
9 Un jeune homme nommé Eutyche, qui était assis sur la fenêtre, succomba à un profond sommeil, parce que Paul parlait fort longtemps, et, entraîné par le sommeil, il tomba du troisième étage en bas: on le releva mort.
Katika dirisha alikuwa amekaa kijana mmoja jina lake Utiko, ambaye alielemewa na usingizi mzito. Hata Paulo alipokuwa akihutubu kwa muda mrefu, kijana huyu, akiwa amelala, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu na aliokotwa akiwa amekufa.
10 Mais Paul, étant descendu, s'étendit sur lui, et, après l'avoir tenu embrassé, il dit: «Cessez vos cris, car la vie est en lui.»
Lakini Paulo alishuka chini, alijinyoosha yeye mwenyewe juu yake, akamkumbatia. Kisha akasema, “Msikate tamaa, kwa kuwa yu hai.”
11 Puis étant remonté, il rompit le pain, mangea et conversa assez longtemps, jusqu’à l'aube; et il partit.
Kisha akapanda tena ghorofani na akaumega mkate, akala. Baada ya kuzungumza nao kwa muda mrefu hadi alfajiri, akaondoka.
12 Quant au jeune homme, on l'amena vivant, ce qui fut une immense consolation.
Wakamleta yule kijana akiwa hai wakafarijika sana.
13 Pour nous, ayant pris les devants par mer, nous fîmes voile vers Assos, où nous devions reprendre Paul, car c'est ainsi qu'il l'avait ordonné: il devait, lui, aller à pied.
Sisi wenyewe tulitangulia mbele ya Paul kwa meli na tukaelekea Aso, ambapo sisi tulipanga kumchukua Paul huko. Hiki ndicho yeye mwenyewe alitaka kufanya, kwa sababu alipanga kwenda kupitia nchi kavu.
14 Lorsqu'il nous eut rejoints à Assos, nous le prîmes avec nous, et nous gagnâmes Mytilène.
Alipotufikia huko Aso, tukampakia kwenye Meli tukaenda Mitilene.
15 Nous partîmes de là, et nous arrivâmes le jour suivant en face de Chio, le troisième jour nous touchâmes Samos, puis, après avoir relâché à Trogylle, nous abordâmes le lendemain à Milet.
Kisha sisi tukatweka kutoka huko na siku ya pili tulifika upande wa pili wa kisiwa cha Kio. Siku iliyofuata, tukawasili kisiwa cha Samo, na kesho yake tukafika mji wa Mileto.
16 Paul avait jugé bon de dépasser Éphèse, pour ne pas perdre de temps en Asie, car il se hâtait, afin d'arriver, s'il était possible, le jour de la Pentecôte à Jérusalem.
Kwa sababu Paulo alikuwa ameamua kusafiri kupitia Efeso, ili kwamba asitumie muda wowote katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka ya kuwahi Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pentekoste, kama ingeliwezekana yeye kufanya hivyo.
17 Cependant il envoya de Milet à Éphèse, pour mander les anciens de l'église.
Kutoka Mileto akatuma watu hadi Efeso na akawaita wazee wa Kanisa.
18 Lorsqu'ils furent venus vers lui, il leur dit: «Vous savez comment, depuis le premier jour que j'ai mis le pied en Asie,
Walipofika kwake, akawaambia, ninyi wenyewe mwajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu muda wote.
19 je me suis toujours comporté avec vous, servant le Seigneur en toute humilité, au milieu des larmes et des épreuves, auxquelles m'ont exposé les embûches des Juifs.
Nimemtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi, na mateso yaliyonipata mimi kwa hila za Wayahudi.
20 Vous savez que je vous ai annoncé l’évangile, et que je vous ai instruits en public et en particulier, sans vous rien cacher de ce qui pouvait vous être avantageux:
Mwajua jinsi ambavyo sikujizuia kutangaza kwenu kitu chochote ambacho kilikuwa muhimu, na jinsi mimi nilivyowafundisha wazi wazi na pia kwenda nyumba kwa nyumba.
21 je n'ai pas cessé d'enseigner aux Juifs et aux Grecs la repentance envers Dieu, et la foi en notre Seigneur Jésus-Christ.
Mnajua jinsi mimi nilivyoendelea kuwaonya Wayahudi na Wayunani juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.
22 Maintenant, je m'en vais à Jérusalem, m'y sentant obligé intérieurement, sans que je sache ce qui doit m'y arriver;
Na sasa, angalieni, mimi, nikiwa ninamtii Roho Mtakatifu kuelekea Yerusalemu, nisiyajue mambo ambayo yatanitokea mimi huko,
23 seulement, de ville en ville, le Saint-Esprit ne cesse de m'assurer que des chaînes et des malheurs m'attendent.
ila kwa kuwa Roho Mtakatifu hunishuhudia mimi katika kila mji na anasema kwamba minyororo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
24 Mais je n'en tiens aucun compte, et je n'attache pour moi-même aucun prix à la vie, pourvu que je fournisse ma carrière, et que j'accomplisse le ministère que j'ai reçu du Seigneur Jésus, d'enseigner la bonne nouvelle de la grâce de Dieu.
Lakini mimi si kufikiria kwamba maisha yangu ni kwa njia yoyote ya thamani kwangu, ili niweze kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kuishuhudia injili ya neema ya Mungu.
25 Pour moi, je sais que vous ne verrez plus mon visage, vous tous parmi lesquels je suis venu prêcher le royaume;
Na sasa, tazama, najua kwamba wote, miongoni mwa wale nilioenda kuwahubiri Ufalme, hamtaniona uso tena.
26 en conséquence je proteste aujourd'hui devant vous que je suis net du sang de tous;
Kwa hiyo nawashuhudia leo hii, kwamba sina hatia kwa damu ya mtu yeyote.
27 car je vous ai annoncé tout le conseil de Dieu, sans vous en rien cacher.
Kwa maana sikujizuia kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
28 Prenez donc garde à vous-mêmes, et à tout le troupeau sur lequel le Saint-Esprit vous a établis évêques, pour paître l'église que le Seigneur s'est acquise par son propre sang.
Kwa hiyo iweni waangalifu juu yenu ninyi wenyewe, na juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe.
29 Je sais qu'après mon départ, il s'introduira parmi vous des loups terribles, qui n'épargneront point le troupeau,
Najua kwamba baada ya kuondoka kwangu, mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.
30 et qu'il s'élèvera dans votre propre sein des hommes professant des doctrines perverses, pour s'attirer des disciples.
Najua kwamba hata miongoni mwenu wenyewe baadhi ya watu watakuja na kusema mambo mapotovu, ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao.
31 Veillez donc, vous souvenant que durant trois années, je n'ai cessé, ni jour ni nuit, d'avertir avec larmes chacun de vous.
Kwa hiyo muwe macho. Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuweza kuacha kuwafundisha kila mmoja wenu kwa machozi usiku na mchana.
32 Et maintenant, je vous recommande à Dieu et à la parole de sa grâce, à celui qui peut édifier et vous donner une part avec tous les sanctifiés.
Na sasa mimi nawakabidhi kwa Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliowekwa wakfu kwa Mungu.
33 Je n'ai désiré ni l'argent, ni l'or, ni les vêtements de personne.
Sikutamani fedha, dhahabu, au mavazi.
34 Vous savez vous-mêmes que ces mains ont pourvu à mes besoins et à ceux de mes compagnons;
Mnajua ninyi wenyewe kwamba mikono hii imenipatia mahitaji yangu mwenyewe na mahitaji ya wale waliokuwa pamoja nami.
35 je vous ai montré de toutes manières que c'est en travaillant ainsi, que l'on doit accueillir les faibles, et se souvenir des paroles du Seigneur, qui a dit lui-même: «Il y a plus de bonheur à donner qu'à recevoir.»
Katika mambo yote niliwapa mfano wa jinsi inavyopasa kuwasaidia wanyonge kwa kufanya kazi, na jinsi mnavyopaswa kukumbuka maneno ya Bwana Yesu, maneno ambayo yeye mwenyewe alisema: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.”
36 Après avoir ainsi parlé, il se mit à genoux, et pria avec eux tous.
Baada ya kusema namna hii, alipiga magoti akaomba pamoja nao.
37 Ils fondirent tous en larmes, et, se jetant au cou de Paul,
Wote wakalia sana na kumwangukia Paulo shingoni na kumbusu.
38 ils l'embrassaient, navrés surtout de ce qu'il leur avait dit qu'ils ne verraient plus son visage. Puis ils l'accompagnèrent jusqu'au vaisseau.
Walihuzunika zaidi ya yote kwa sababu ya kile ambacho alikuwa amesema, kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Kisha wakamsindikiza merikebuni.

< Actes 20 >