< Apocalypse 2 >

1 Ecris à l'Ange de l'Eglise d'Ephèse: celui qui tient les sept étoiles en sa main droite, et qui marche au milieu des sept chandeliers d'or, dit ces choses:
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
2 Je connais tes œuvres, ton travail et ta patience, et [je sais] que tu ne peux souffrir les méchants, et que tu as éprouvé ceux qui se disent être apôtres, et ne le sont point, et que tu les as trouvés menteurs.
Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
3 Et que tu as souffert, et que tu as eu patience, et que tu as travaillé pour mon Nom, et que tu ne t'es point lassé.
Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
4 Mais j'ai [quelque chose] contre toi, c'est que tu as abandonné ta première charité.
“Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
5 C'est pourquoi souviens-toi d'où tu es déchu, et t'en repens, et fais les premières œuvres; autrement je viendrai à toi bientôt, et j'ôterai ton chandelier de son lieu, si tu ne te repens.
Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
6 Mais pourtant tu as ceci [de bon] que tu hais les actions des Nicolaïtes, lesquelles je hais moi aussi.
Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
7 Que celui qui a des oreilles, écoute ce que l'Esprit dit aux Eglises. A celui qui vaincra je lui donnerai à manger de l'arbre de vie, qui est au milieu du paradis de Dieu.
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
8 Ecris aussi à l'Ange de l'Eglise de Smyrne: Le premier et le dernier, qui a été mort, et qui est retourné en vie, dit ces choses:
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
9 Je connais tes œuvres, ton affliction et ta pauvreté (mais tu es riche), et le blasphème de ceux qui se disent être Juifs, et qui ne le sont point, mais [qui sont] la Synagogue de satan.
Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
10 Ne crains rien des choses que tu as à souffrir. Voici, il arrivera que le Démon mettra quelques-uns de vous en prison, afin que vous soyez éprouvés; et vous aurez une affliction de dix jours. Sois fidèle jusques à la mort, et je te donnerai la couronne de vie.
Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
11 Que celui qui a des oreilles, écoute ce que l'Esprit dit aux Eglises. Celui qui vaincra sera mis à couvert de la mort seconde.
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
12 Ecris aussi à l'Ange de l'Eglise de Pergame: Celui qui a l'épée aiguë à deux tranchants, dit ces choses.
“Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
13 Je connais tes œuvres, et où tu habites, [savoir] là où est le siège de satan, et que cependant tu retiens mon Nom, et que tu n'as point renoncé ma foi, non pas même lorsqu'Antipas, mon fidèle martyr, a été mis à mort entre vous, là où satan habite.
Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
14 Mais j'ai quelque peu de chose contre toi: c'est que tu en as là qui retiennent la doctrine de Balaam, lequel enseignait Balac à mettre un scandale devant les enfants d'Israël, afin qu'ils mangeassent des choses sacrifiées aux idoles, et qu'ils se livrassent à la fornication.
“Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
15 Ainsi tu en as, toi aussi, qui retiennent la doctrine des Nicolaïtes; ce que je hais.
Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
16 Repens-toi: autrement je viendrai à toi bientôt; et je combattrai contre eux par l'épée de ma bouche.
Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
17 Que celui qui a des oreilles, écoute ce que l'Esprit dit aux Eglises. A celui qui vaincra je lui donnerai à manger de la manne qui est cachée, et je lui donnerai un caillou blanc, et sur [ce] caillou sera écrit un nouveau nom, que nul ne connaît, sinon celui qui le reçoit.
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
18 Ecris aussi à l'Ange de l'Eglise de Thyatire: Le Fils de Dieu, qui a ses yeux comme une flamme de feu, et dont les pieds sont semblables à de l'airain très luisant, dit ces choses.
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
19 Je connais tes œuvres, [ta] charité, ton ministère, ta foi, ta patience, et que tes dernières œuvres surpassent les premières;
Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
20 Mais j'ai quelque peu de chose contre toi: c'est que tu souffres que [cette] femme Jézabel, qui se dit prophétesse, enseigne, et qu'elle séduise mes serviteurs, pour les porter à la fornication, et pour [leur faire] manger des choses sacrifiées aux idoles.
“Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
21 Et je lui ai donné du temps, afin qu'elle se repentit de sa prostitution; mais elle ne s'est point repentie.
Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
22 Voici, je vais la réduire au lit, et [mettre] dans une grande affliction ceux qui commettent adultère avec elle, s'ils ne se repentent de leurs œuvres;
Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
23 Et je ferai mourir de mort ses enfants; et toutes les Eglises connaîtront que je suis celui qui sonde les reins et les cœurs; et je rendrai à chacun de vous selon ses œuvres.
Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
24 Mais je vous dis à vous et aux autres qui sont à Thyatire, à tous ceux qui n'ont point cette doctrine, et qui n'ont point connu les profondeurs de satan, comme ils parlent, que je ne mettrai point sur vous d'autre charge.
Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
25 Mais retenez ce que vous avez, jusqu'à ce que je vienne.
Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
26 Car à celui qui aura vaincu, et qui aura gardé mes œuvres jusqu'à la fin, je lui donnerai puissance sur les nations:
“Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
27 Et il les gouvernera avec une verge de fer, et elles seront brisées comme les vaisseaux d'un potier, selon que je l'ai aussi reçu de mon Père.
“‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
28 Et je lui donnerai l'étoile du matin.
Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
29 Que celui qui a des oreilles, écoute ce que l'Esprit dit aux Eglises.
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.

< Apocalypse 2 >