< Psaumes 96 >
1 Chantez à l'Eternel un nouveau cantique; vous toute la terre chantez à l'Eternel.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Chantez à l'Eternel, bénissez son Nom, prêchez de jour en jour sa délivrance.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Racontez sa gloire parmi les nations, [et] ses merveilles parmi tous les peuples.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 Car l'Eternel [est] grand, et digne d'être loué; il [est] redoutable par-dessus tous les dieux;
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 Car tous les dieux des peuples [ne sont que des] idoles; mais l'Eternel a fait les cieux.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 La majesté et la magnificence [marchent] devant lui; la force et l'excellence sont dans son sanctuaire.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Familles des peuples rendez à l'Eternel, rendez à l'Eternel la gloire et la force.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Rendez à l'Eternel la gloire due à son Nom; apportez l'oblation, et entrez dans ses parvis.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Prosternez-vous devant l'Eternel avec une sainte magnificence; vous tous les habitants de la terre tremblez tout étonnés, à cause de la présence de sa face.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Dites parmi les nations: l'Eternel règne; même la terre habitable est affermie, [et] elle ne sera point ébranlée; il jugera les peuples en équité.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Que les cieux se réjouissent, et que la terre s'égaye! Que la mer et ce qui est contenu en elle bruie!
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Que les champs s'égayent, avec tout ce qui est en eux. Alors tous les arbres de la forêt chanteront de joie,
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Au-devant de l'Eternel, parce qu'il vient, parce qu'il vient pour juger la terre; il jugera en justice le monde habitable, et les peuples selon sa fidélité.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.