< Psaumes 91 >

1 Celui qui se tient dans la demeure du Souverain, se loge à l'ombre du Tout-Puissant.
Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2 Je dirai à l'Eternel: Tu es ma retraite, et ma forteresse, tu es mon Dieu en qui je m'assure.
Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 Certes il te délivrera du filet du chasseur; [et] de la mortalité malheureuse.
Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 Il te couvrira de ses plumes, et tu auras retraite sous ses ailes; sa vérité [te servira de] rondache et de bouclier.
Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 Tu n'auras point peur de ce qui épouvante de nuit, ni de la flèche qui vole de jour.
Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 Ni de la mortalité qui marche dans les ténèbres; ni de la destruction qui fait le dégât en plein midi.
wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 Il en tombera mille à ton côté, et dix mille à ta droite; mais la [destruction] n'approchera point de toi.
Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Seulement tu contempleras de tes yeux, et tu verras la récompense des méchants.
Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 Car tu es ma retraite, ô Eternel! tu as établi le Souverain pour ton domicile.
Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 Aucun mal ne te rencontrera, et aucune plaie n'approchera de ta tente.
Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 Car il donnera charge de toi à ses Anges, afin qu'ils te gardent en toutes tes voies.
Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 Ils te porteront dans leurs mains, de peur que ton pied ne heurte contre la pierre.
Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 Tu marcheras sur le lion et sur l'aspic, [et] tu fouleras le lionceau et le dragon.
Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 Puisqu'il m'aime avec affection, [dit le Seigneur], je le délivrerai; je le mettrai en une haute retraite, parce qu'il connaît mon Nom.
Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
15 Il m'invoquera, et je l'exaucerai; je serai avec lui dans la détresse, je l'en retirerai, et le glorifierai.
Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
16 Je le rassasierai de jours, et je lui ferai voir ma délivrance.
Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.

< Psaumes 91 >