< Psaumes 56 >
1 Mictam de David, [donné] au maître chantre, [pour le chanter] sur Jonathelem-rehokim, touchant ce que les Philistins le prirent dans Gath. Ô Dieu! aie pitié de moi, car l'homme [mortel] m'engloutit [et] m'opprime, me faisant tout le jour la guerre.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 Mes espions m'ont englouti tout le jour; car, ô Très-haut! Plusieurs me font la guerre.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 Le jour auquel je craindrai je me confierai en toi.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 Je louerai en Dieu sa parole, je me confie en Dieu, je ne craindrai rien; que me fera la chair?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Tout le jour ils tordent mes propos, et toutes leurs pensées tendent à me nuire.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 Ils s'assemblent, ils se tiennent cachés, ils observent mes talons, attendant [comment ils surprendront] mon âme.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Leur moyen d'échapper c'est par outrage; ô Dieu, précipite les peuples en ta colère!
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Tu as compté mes allées et venues; mets mes larmes dans tes vaisseaux; ne sont-elles pas écrites dans ton registre?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Le jour auquel je crierai à toi, mes ennemis retourneront en arrière; je sais que Dieu est pour moi.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 Je louerai en Dieu sa parole, je louerai en l'Eternel sa parole.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 Je me confie en Dieu, je ne craindrai rien; que me fera l'homme?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Ô Dieu, tes vœux seront sur moi; je te rendrai des actions de grâces.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 Puisque tu as délivré mon âme de la mort, ne [garderais-tu] pas mes pieds de broncher, afin que je marche devant Dieu en la lumière des vivants?
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.