< Psaumes 48 >

1 Cantique de Psaume, des enfants de Coré. L'Eternel est grand, et fort louable en la ville de notre Dieu, en la montagne de sa Sainteté.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Le plus beau de la contrée, la joie de toute la terre, c'est la montagne de Sion au fond de l'Aquilon; c'est la ville du grand Roi.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 Dieu est connu en ses palais pour une haute retraite.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 Car voici, les Rois s'étaient donné assignation, ils avaient passé outre tous ensemble.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 L'ont-ils vue? ils en ont été aussitôt étonnés; ils ont été tout troublés, ils s'en sont fuis à l'étourdie.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Là le tremblement les a saisis, [et] une douleur comme de celle qui enfante.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 [Ils ont été chassés comme] par le vent d'Orient [qui] brise les navires de Tarsis.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Comme nous l'avions entendu, ainsi l'avons-nous vu dans la ville de l'Eternel des armées, dans la ville de notre Dieu, laquelle Dieu maintiendra à toujours; (Sélah)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 Ô Dieu! nous avons entendu ta gratuité au milieu de ton Temple.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 Ô Dieu! tel qu'est ton Nom, telle [est] ta louange jusqu'aux bouts de la terre; ta droite est pleine de justice.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 La montagne de Sion se réjouira, et les filles de Juda auront de la joie, à cause de tes jugements.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Environnez Sion, et l'entourez, [et] comptez ses tours.
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Prenez bien garde à son avant-mur, et considérez ses palais; afin que vous le racontiez à la génération à venir.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 Car c'est le Dieu qui est notre Dieu à toujours et à perpétuité; il nous accompagnera jusques à la mort.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< Psaumes 48 >