< Psaumes 36 >

1 Psaume de David, serviteur de l'Eternel, [donné] au maître chantre. La transgression du méchant me dit au-dedans du cœur, qu'il n'y a point de crainte de Dieu devant ses yeux.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 Car il se flatte en soi-même quand son iniquité se présente pour être haïe.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 Les paroles de sa bouche ne sont qu'injustice et que fraude, il se garde d'être attentif à bien faire.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 Il machine sur son lit les moyens de nuire; il s'arrête au chemin qui n'est pas bon; il n'a point en horreur le mal.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Eternel, ta gratuité atteint jusqu'aux cieux, ta fidélité jusqu'aux nues.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Ta justice est comme de hautes montagnes, tes jugements sont un grand abîme. Eternel, tu conserves les hommes et les bêtes.
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 Ô Dieu! combien est précieuse ta gratuité! aussi les fils des hommes se retirent sous l'ombre de tes ailes.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Ils seront abondamment rassasiés de la graisse de ta maison, et tu les abreuveras au fleuve de tes délices.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 Car la source de la vie est par-devers toi, [et] par ta clarté nous voyons clair.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Continue ta gratuité sur ceux qui te connaissent, et ta justice sur ceux qui sont droits de cœur.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Que le pied de l'orgueilleux ne s'avance point sur moi, et que la main des méchants ne m'ébranle point.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 Là sont tombés les ouvriers d'iniquité, ils ont été renversés, et n'ont pu se relever.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< Psaumes 36 >