< Psaumes 17 >

1 Requête de David. Eternel! écoute ma juste cause, sois attentif à mon cri, prête l'oreille à ma requête, [laquelle je te fais] sans qu'il y ait de fraude en mes lèvres.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 Que mon droit sorte de ta présence, que tes yeux regardent à la justice.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Tu as sondé mon cœur, tu [l']as visité de nuit, tu m'as examiné, tu n'as rien trouvé; ma pensée ne va point au-delà de ma parole.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 Quant aux actions des hommes, selon la parole de tes lèvres, je me suis donné garde de la conduite de l'homme violent.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Ayant affermi mes pas en tes sentiers, les plantes de mes pieds n'ont point chancelé.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 Ô [Dieu] Fort! je t'invoque, parce que tu as accoutumé de m'exaucer; incline ton oreille vers moi, écoute mes paroles.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Rends admirables tes gratuités, toi qui délivres ceux qui se retirent vers toi de devant ceux qui s'élèvent contre ta droite.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Garde-moi comme la prunelle de l'œil, [et] me cache sous l'ombre de tes ailes;
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 De devant ces méchants qui m'ont pillé; et de mes ennemis mortels, qui m'environnent.
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 La graisse leur cache le visage; ils parlent fièrement de leur bouche.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 Maintenant, ils nous environnent à chaque pas que nous faisons; ils jettent leur regard pour nous étendre par terre.
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Il ressemble au lion qui ne demande qu'à déchirer, et au lionceau qui se tient dans les lieux cachés.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Lève-toi, ô Eternel, devance-le, renverse-le; délivre mon âme du méchant [par] ton épée.
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 Eternel, [délivre-moi par] ta main de ces gens, des gens du monde, desquels le partage est en cette vie, et dont tu remplis le ventre de tes provisions; leurs enfants sont rassasiés, et ils laissent leurs restes à leurs petits enfants.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 [Mais] moi, je verrai ta face en justice, et je serai rassasié de ta ressemblance, quand je serai réveillé.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Psaumes 17 >