< Psaumes 130 >

1 Cantique Mahaloth. Ô Éternel! je t'invoque des lieux profonds.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Seigneur, écoute ma voix! que tes oreilles soient attentives à la voix de mes supplications.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Ô Eternel! si tu prends garde aux iniquités, Seigneur, qui est-ce qui subsistera?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Mais il y a pardon par-devers toi, afin que tu sois craint.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 J'ai attendu l'Eternel; mon âme l'a attendu, et j'ai eu mon attente en sa parole.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Mon âme [attend] le Seigneur plus que les sentinelles [n'attendent] le matin, plus que les sentinelles [n'attendent] le matin.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Israël, attends-toi à l'Eternel: car l'Eternel est miséricordieux et il y a rédemption en abondance par devers lui.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Et lui-même rachètera Israël de toutes ses iniquités.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psaumes 130 >