< Psaumes 113 >
1 Louez l'Eternel. Louez, vous serviteurs de l'Eternel, louez le Nom de l’Eternel.
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Le Nom de l’Eternel soit béni dès maintenant et à toujours.
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 Le Nom de l’Eternel est digne de louange depuis le soleil levant jusqu’au soleil couchant.
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 L'Eternel est élevé par-dessus toutes les nations, sa gloire est par-dessus les cieux.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 Qui est semblable à l'Eternel notre Dieu, lequel habite aux lieux très-hauts?
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 Lequel s'abaisse pour regarder aux cieux, et en la terre.
atazamaye chini angani na duniani?
7 Lequel relève l'affligé de la poudre, et retire le pauvre de dessus le fumier,
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 Pour le faire asseoir avec les principaux, avec les principaux, [dis-je], de son peuple;
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Lequel donne une famille à la femme qui était stérile, [la rendant] mère d'enfants, [et] joyeuse. Louez l'Eternel.
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!