< Psaumes 112 >

1 Louez l'Eternel. [Aleph.] Bienheureux est l'homme qui craint l'Eternel, [Beth.] et qui prend un singulier plaisir en ses commandements!
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 [Guimel.] Sa postérité sera puissante en la terre, [ Daleth.] la génération des hommes droits sera bénie.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 [ He.] Il y aura des biens et des richesses en sa maison; [Vau.] et sa justice demeure à perpétuité.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 [Zaïn.] La lumière s'est levée dans les ténèbres à ceux qui sont justes; [Heth.] il est pitoyable, miséricordieux et charitable.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 [Teth.] L'homme de bien fait des aumônes, et prête; [Jod.] Il dispense ses affaires avec droiture.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 [Caph.] Même il ne sera jamais ébranlé. [Lamed.] Le juste sera en mémoire perpétuelle.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 [Mem.] Il n'aura peur d'aucun mauvais rapport; [Nun.] Son cœur est ferme s'assurant en l'Eternel.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 [Samech.] Son cœur est bien appuyé, il ne craindra point, [Hajin.] jusqu’à ce qu'il ait vu en ses adversaires [ce qu'il désire].
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 [Pe.] Il a répandu, il a donné aux pauvres; [Tsade.] sa justice demeure à perpétuité; [Koph.] sa corne sera élevée en gloire.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 [Resch.] Le méchant le verra, et en aura du dépit. [Sein.] Il grincera les dents, et se fondra; [Thau.] le désir des méchants périra.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

< Psaumes 112 >