< Psaumes 104 >

1 Mon âme, bénis l'Eternel. Ô Eternel mon Dieu, tu es merveilleusement grand, tu es revêtu de majesté et de magnificence.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Il s'enveloppe de lumière comme d'un vêtement, il étend les cieux comme un voile.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Il planchéie ses hautes chambres entre les eaux; il fait des grosses nuées son chariot, il se promène sur les ailes du vent.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Il fait des vents ses Anges, et du feu brûlant ses serviteurs.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Il a fondé la terre sur ses bases, tellement qu'elle ne sera point ébranlée à perpétuité.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Tu l'avais couverte de l'abîme comme d'un vêtement, les eaux se tenaient sur les montagnes.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 Elles s'enfuirent à ta menace, [et] se mirent promptement en fuite au son de ton tonnerre.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Les montagnes s'élevèrent, et les vallées s'abaissèrent, au même lieu que tu leur avais établi.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Tu leur as mis une borne qu'elles ne passeront point, elles ne retourneront plus à couvrir la terre.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 C'est lui qui conduit les fontaines par les vallées, tellement qu'elles se promènent entre les monts.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Elles abreuvent toutes les bêtes des champs, les ânes sauvages en étanchent leur soif.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Les oiseaux des cieux se tiennent auprès d'elles, et font résonner leur voix d'entre la ramée.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Il abreuve les montagnes de ses chambres hautes; [et] la terre est rassasiée du fruit de tes œuvres.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Il fait germer le foin pour le bétail, et l'herbe pour le service de l'homme, faisant sortir le pain de la terre;
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Et le vin qui réjouit le cœur de l'homme, qui fait reluire son visage avec l'huile, et qui soutient le cœur de l'homme avec le pain.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Les hauts arbres en sont rassasiés, [et] les cèdres du Liban, qu'il a plantés,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Afin que les oiseaux y fassent leurs nids. Quant à la cigogne, les sapins [sont sa demeure].
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Les hautes montagnes sont pour les chamois [et] les rochers sont la retraite des lapins.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Il a fait la lune pour les saisons, et le soleil connaît son coucher.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Tu amènes les ténèbres, et la nuit vient, durant laquelle toutes les bêtes de la forêt trottent.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Les lionceaux rugissent après la proie, et pour demander au [Dieu] Fort leur pâture.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Le soleil se lève-t-il? ils se retirent et demeurent gisants en leurs tanières.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Alors l'homme sort à son ouvrage et à son travail, jusqu’au soir.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Ô Eternel, que tes œuvres sont en grand nombre! tu les as toutes faites avec sagesse; la terre est pleine de tes richesses.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Cette mer grande et spacieuse, où il y a sans nombre des animaux se mouvant, des petites bêtes avec des grandes!
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Là se promènent les navires, et ce Léviathan que tu as formé pour s'y ébattre.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Elles s'attendent toutes à toi, afin que tu leur donnes la pâture en leur temps.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Quand tu la leur donnes, elles la recueillent, et quand tu ouvres ta main, elles sont rassasiées de biens.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Caches-tu ta face? elles sont troublées; retires-tu leur souffle, elles défaillent, et retournent en leur poudre.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 [Mais si] tu renvoies ton Esprit, elles sont créées, et tu renouvelles la face de la terre.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Que la gloire de l'Eternel soit à toujours, que l'Eternel se réjouisse en ses œuvres!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Il jette sa vue sur la terre, et elle en tremble; il touche les montagnes, et elles en fument.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Je chanterai à l'Eternel durant ma vie; je psalmodierai à mon Dieu pendant que j'existerai.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Ma méditation lui sera agréable; [et] je me réjouirai en l'Eternel.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Que les pécheurs soient consumés de dessus la terre, et qu'il n'y ait plus de méchants! Mon âme, bénis l'Eternel; louez l'Eternel.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psaumes 104 >