< Nombres 1 >

1 Or l'Eternel parla à Moïse au désert de Sinaï, dans le Tabernacle d'assignation, le premier jour du second mois de la seconde année, après qu'ils furent sortis du pays d'Egypte, en disant:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Faites le dénombrement de toute l'assemblée des enfants d'Israël, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant nom par nom, [savoir] tous les mâles, chacun par tête;
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 Depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux d'Israël qui peuvent aller à la guerre, vous les compterez suivant leurs troupes, toi et Aaron.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 Et il y aura avec vous un homme de chaque Tribu, [savoir] celui qui [est] le chef de la maison de ses pères.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 Et ce sont ici les noms de ces hommes qui vous assisteront. Pour la Tribu de Ruben, Elitsur fils de Sédéur.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Pour celle de Siméon, Sélumiel, fils de Tsurisaddaï.
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Pour celle de Juda, Nahasson, fils de Hamminadab.
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Pour celle d'Issacar, Nathanaël, fils de Tsuhar.
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Pour celle de Zabulon, Eliab, fils de Hélon.
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 des enfants de Joseph, pour la Tribu d'Ephraïm, Elisamah, fils de Hammiud; pour celle de Manassé, Gamaliel fils de Pédatsur.
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Pour la Tribu de Benjamin, Abidan, fils de Guidhoni.
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Pour celle de Dan, Ahihézer, fils de Hammisaddaï.
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Pour celle d'Aser, Paghiel, fils de Hocran.
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Pour celle de Gad, Eliasaph, fils de Déhuël.
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Pour celle de Nephthali, Ahirah, fils de Hénan.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 C'étaient là ceux qu'on appelait pour tenir l'assemblée; ils étaient les principaux des Tribus de leurs pères, chefs des milliers d'Israël.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Alors Moïse et Aaron prirent ces hommes-là qui avaient été nommés par leurs noms;
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 Et ils convoquèrent toute l'assemblée, le premier jour du second mois, et on enregistra chacun selon leurs familles, [et] selon la maison de leurs pères, les enregistrant, nom par nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, chacun par tête;
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 Comme l'Eternel l'avait commandé à Moïse, il les dénombra au désert de Sinaï.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 Les enfants donc de Ruben, premier-né d'Israël, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dont on fit le dénombrement par leur nom, [et] par tête, [savoir] tous les mâles de l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Ruben, qui furent dénombrés, furent quarante-six mille cinq cents.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Des enfants de Siméon, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, ceux qui furent dénombrés par leur nom et par tête, [savoir] tous les mâles de l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Siméon, qui furent dénombrés, furent cinquante-neuf mille trois cents.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Des enfants de Gad, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 Ceux, [ dis-je], de la Tribu de Gad, qui furent dénombrés, furent quarante-cinq mille six cent cinquante.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Des enfants de Juda, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Juda, qui furent dénombrés, furent soixante et quatorze mille six cents.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Des enfants d'Issacar, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 Ceux, [dis-je], de la Tribu d'Issacar, qui furent dénombrés, furent cinquante-quatre mille quatre cents.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Des enfants de Zabulon, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Zabulon, qui furent dénombrés, furent cinquante-sept mille quatre cents.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Quant aux enfants de Joseph; les enfants d'Ephraïm, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 Ceux, [dis-je], de la Tribu d'Ephraïm, qui furent dénombrés, furent quarante mille cinq cents.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Des enfants de Manassé, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Manassé, qui furent dénombrés, furent trente-deux mille deux cents.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Des enfants de Benjamin, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Benjamin, qui furent dénombrés, furent trente-cinq mille quatre cents.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Des enfants de Dan, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Dan, qui furent dénombrés, furent soixante-deux mille sept cents.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Des enfants d'Aser, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 Ceux, [dis-je], de la Tribu d'Aser, qui furent dénombrés, furent quarante et un mille cinq cents.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 [Des] enfants de Nephthali, selon leurs générations, leurs familles, et les maisons de leurs pères, dénombrés chacun par leur nom, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre;
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 Ceux, [dis-je], de la Tribu de Nephthali, qui furent dénombrés, furent cinquante-trois mille quatre cents.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Ce sont là ceux dont Moïse et Aaron firent le dénombrement, les douze principaux [d'entre les enfants] d'Israël y étant, un pour chaque maison de leurs pères.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 Ainsi tous ceux des enfants d'Israël, dont on fit le dénombrement, selon les maisons de leurs pères, depuis l'âge de vingt ans, et au dessus, tous ceux d'entre les Israélites, qui pouvaient aller à la guerre;
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 Tous ceux, [dis-je], dont on fit le dénombrement, furent six cent trois mille cinq cent cinquante.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Mais les Lévites ne furent point dénombrés avec eux, selon la Tribu de leurs pères.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Car l'Eternel avait parlé à Moïse, en disant:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Tu ne feras aucun dénombrement de la Tribu de Lévi, et tu n'en lèveras point la somme avec les [autres] enfants d'Israël.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Mais tu donneras aux Lévites la charge du pavillon du Témoignage, et de tous ses ustensiles, et de tout ce qui lui appartient; ils porteront le pavillon, et tous ses ustensiles; ils y serviront, et camperont autour du pavillon.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 Et quand le pavillon partira, les Lévites le désassembleront, et quand le pavillon campera, ils le dresseront. Que si quelque étranger en approche, on le fera mourir.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 Or les enfants d'Israël camperont chacun en son quartier, et chacun sous son enseigne, selon leurs troupes.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Mais les Lévites camperont autour du pavillon du Témoignage, afin qu'il n'y ait point d'indignation sur l'assemblée des enfants d'Israël, et ils prendront en leur charge le pavillon du Témoignage.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Et les enfants d'Israël firent selon toutes les choses que l'Eternel avait commandées à Moïse; ils le firent ainsi.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Nombres 1 >