< Néhémie 9 >

1 Et le vingt-quatrième jour du même mois, les enfants d'Israël s'assemblèrent, jeûnant, revêtus de sacs, et ayant de la terre sur eux.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 Et la race d'Israël se sépara de tous les étrangers, et ils se présentèrent, confessant leurs péchés et les iniquités de leurs pères.
Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 Ils se levèrent donc en leur place, et on lut au Livre de la Loi de l'Eternel, leur Dieu pendant la quatrième partie du jour, et pendant une [autre] quatrième partie, ils faisaient confession [de leurs péchés], et se prosternaient devant l'Eternel leur Dieu.
Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
4 Et Jésuah, Bani, Kadmiel, Sébania, Bunni, Sérebia, Bani et Kenani se levèrent sur le lieu qu'on avait élevé pour les Lévites, et crièrent à haute voix à l'Eternel leur Dieu.
Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
5 Et les Lévites, [savoir], Jésuah, Kadmiel, Bani, Hasabnéja, Sérebia, Hodija, Sébania et Péthahia, dirent: Levez-vous, bénissez l'Eternel votre Dieu de siècle en siècle; et qu'on bénisse, [ô Dieu!] le Nom de ta gloire; et qu'il soit élevé au-dessus de toute bénédiction et louange!
Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 Tu es toi seul l'Eternel, tu as fait les cieux, les cieux des cieux, et toute leur armée; la terre, et tout ce qui y est; les mers, et toutes les choses qui y sont. Tu vivifies toutes ces choses, et l'armée des cieux se prosterne devant toi.
Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 Tu es l'Eternel Dieu, qui choisis Abram, et qui le tiras hors d'Ur des Chaldéens, et lui imposas le nom d'Abraham.
“Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
8 Tu trouvas son cœur fidèle devant toi, et tu traitas avec lui cette alliance, que tu donnerais le pays des Cananéens, des Héthiens, des Amorrhéens, des Phéréziens, des Jébusiens, et des Guirgasiens, que tu le donnerais à sa postérité; et tu as accompli ce que tu as promis, parce que tu es juste.
Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 Car tu as regardé l'affliction de nos pères en Egypte, et tu as ouï leur cri près de la mer Rouge;
“Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 Et tu as fait des prodiges et des miracles sur Pharaon et sur tous ses serviteurs, et sur tout le peuple de son pays; parce que tu connus qu'ils s'étaient fièrement élevés contre eux, et tu t'es acquis un nom, tel qu'[il paraît] aujourd'hui.
Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 Tu fendis aussi la mer devant eux, et ils passèrent par le sec au travers de la mer; et tu jetas au fond [des abîmes] ceux qui les poursuivaient, comme une pierre dans les eaux violentes.
Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 Tu les as même conduits de jour par la colonne de nuée, et de nuit par la colonne de feu, pour les éclairer dans le chemin par où ils devaient aller.
Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 Tu descendis aussi sur la montagne de Sinaï, tu parlas avec eux des cieux, tu leur donnas des ordonnances droites, et des lois véritables, des statuts et des commandements justes.
“Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
14 Tu leur enseignas ton saint Sabbat; et tu leur donnas les commandements, les statuts, et la Loi par le moyen de Moïse ton serviteur.
Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
15 Tu leur donnas aussi des cieux du pain pour leur faim, et tu fis sortir l'eau du rocher pour leur soif, et tu leur dis qu'ils entrassent, et qu'ils possédassent le pays au sujet duquel tu avais levé ta main que tu le leur donnerais.
Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 Mais eux et nos pères se sont fièrement élevés et ont roidi leur cou, et n'ont point écouté tes commandements.
“Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 Ils refusèrent d'écouter, et ne se souvinrent point des merveilles que tu avais faites en leur faveur; mais ils roidirent leur cou, et par leur rébellion ils se proposèrent de s'établir un Chef pour retourner à leur servitude. Mais comme tu es un Dieu qui pardonne, miséricordieux, pitoyable, tardif à la colère, et abondant en gratuité, tu ne les abandonnas point.
Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 Et quand ils se firent un veau de fonte, et qu'ils dirent: Voici ton Dieu qui t'a fait monter hors d'Egypte, et qu'ils [te] firent de grands outrages;
hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
19 Tu ne les abandonnas pourtant point dans le désert par tes grandes miséricordes; la colonne de nuée ne se retira point de dessus eux de jour, pour les conduire par le chemin, ni la colonne de feu de nuit, pour les éclairer dans le chemin par lequel ils devaient aller.
“Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 Et tu leur donnas ton bon Esprit pour les rendre sages; et tu ne retiras point ta Manne loin de leur bouche, et tu leur donnas de l'eau pour leur soif.
Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 Ainsi tu les nourris quarante ans au désert, en sorte que rien ne leur manqua. Leurs vêtements ne s'envieillirent point, et leurs pieds ne furent point foulés.
Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 Et tu leur donnas les Royaumes et les peuples, et les leur partageas par contrées; car ils ont possédé le pays de Sihon, [savoir] le pays du Roi de Hesbon, et le pays de Hog, Roi de Basan.
“Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 Et tu multiplias leurs enfants comme les étoiles des cieux, et les introduisis au pays duquel tu avais dit à leurs pères, qu'ils [y] entreraient pour [le] posséder.
Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 Ainsi leurs enfants y entrèrent, et possédèrent le pays; et tu abaissas devant eux les Cananéens, habitants du pays, et les livras entre leurs mains, eux et leurs Rois, et les peuples du pays, afin qu'ils les traitassent selon leur volonté.
Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 De sorte qu'ils prirent les villes fermées et la terre grasse, et possédèrent les maisons pleines de tous biens, les puits qu'on avait creusés, les vignes, les oliviers, et les arbres fruitiers en abondance, desquels ils ont mangé, et ont été rassasiés; ils ont été engraissés, et ils se sont délicieusement traités de tes grands biens.
Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 Mais ils t'ont irrité, et se sont rebellés contre toi; ils ont jeté ta Loi derrière leur dos, ils ont tué les Prophètes qui les sommaient pour les ramener à toi, et ils t'ont fait de grands outrages.
“Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
27 C'est pourquoi tu les as livrés entre les mains de leurs ennemis, qui les ont affligés; mais au temps de leur angoisse ils ont crié à toi, et tu les as exaucés des cieux, et, selon tes grandes miséricordes tu leur as donné des libérateurs, qui les ont délivrés de la main de leurs ennemis.
Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 Mais dès qu'ils avaient du repos ils retournaient à mal faire en ta présence; c'est pourquoi tu les abandonnais entre les mains de leurs ennemis qui dominaient sur eux. Puis ils retournaient et criaient vers toi, et tu les exauçais des cieux. Ainsi tu les as délivrés selon tes miséricordes, plusieurs fois, et en divers temps.
“Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 Et tu les as sommés pour les ramener à ta Loi, mais ils se sont fièrement élevés, et n'ont point obéi à tes commandements; mais ils ont péché contre tes ordonnances, lesquelles si l'homme accomplit, il vivra par elles. Ils ont toujours tiré l'épaule en arrière, et ont roidi leur cou, et n'ont pas écouté.
“Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 Et tu les as attendus patiemment plusieurs années, et tu les as sommés par ton Esprit par le ministère de tes Prophètes; mais ils ne leur ont point prêté l'oreille; c'est pourquoi tu les as livrés entre les mains des peuples des pays [étrangers.]
Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 Néanmoins par tes grandes miséricordes, tu ne les as point détruits, ni tu ne les as point entièrement abandonnés; car tu es le [Dieu] Fort, miséricordieux, et pitoyable.
Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 Maintenant donc, ô notre Dieu! Le fort, le grand, le puissant et le terrible, gardant l'alliance et la gratuité; Que cette affliction qui nous est arrivée, à nous, à nos Rois, à nos principaux, à nos Sacrificateurs, à nos Prophètes, à nos pères et à tout ton peuple, depuis le temps des Rois d'Assyrie, jusqu'à aujourd'hui, ne soit point réputée petite devant toi.
“Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 Certainement tu es juste en toutes les choses qui nous sont arrivées; car tu as agi selon la vérité, mais nous, nous avons agi criminellement.
Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 Ni nos Rois, ni nos principaux, ni nos Sacrificateurs, ni nos pères n'ont point mis en effet ta Loi, et n'ont point été attentifs à tes commandements, ni à tes sommations par lesquelles tu les as sommés.
Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 Car ils ne t'ont point servi durant leur règne, ni durant les grands biens que tu leur as faits, même dans le pays spacieux et gras que tu leur avais donné pour être à leur disposition, et ils ne se sont point détournés de leurs mauvaises œuvres.
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 Voici, nous sommes aujourd'hui esclaves, même dans le pays que tu as donné à nos pères pour en manger le fruit et les biens; voici, nous y sommes esclaves.
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 Et il rapporte en abondance pour les Rois que tu as établis sur nous à cause de nos péchés, et qui dominent sur nos corps; et sur nos bêtes, à leur volonté; de sorte que nous sommes dans une grande angoisse.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 C'est pourquoi, à cause de toutes ces choses nous contractons une ferme alliance, et nous l'écrivons; et les principaux d'entre nous, nos Lévites, et nos Sacrificateurs y apposent leurs seings.
“Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”

< Néhémie 9 >