< Michée 4 >
1 Mais il arrivera aux derniers jours, que la montagne de la maison de l'Eternel sera affermie au sommet des montagnes, et sera élevée par-dessus les coteaux; les peuples y aborderont.
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
2 Et plusieurs nations iront, et diront: Venez, et montons à la montagne de l'Eternel, et à la maison du Dieu de Jacob; et il nous enseignera touchant ses voies, et nous marcherons dans ses sentiers; car la Loi sortira de Sion, et la parole de l'Eternel [sortira] de Jérusalem.
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
3 Il exercera jugement parmi plusieurs peuples, et il censurera fortement les grandes nations jusqu'aux pays les plus éloignés; et de leurs épées elles forgeront des hoyaux; et de leurs hallebardes, des serpes; une nation ne lèvera plus l'épée contre l'autre, et elles ne s'adonneront plus à la guerre.
Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
4 Mais chacun s'assiéra sous sa vigne et sous son figuier, et il n'y aura personne qui les épouvante; car la bouche de l'Eternel des armées a parlé.
Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
5 Certainement tous les peuples marcheront chacun au nom de son dieu; mais nous marcherons au nom de l'Eternel notre Dieu à toujours et à perpétuité.
Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
6 En ce temps-là, dit l'Eternel, j'assemblerai la boiteuse, et je recueillerai celle qui avait été chassée, et celle que j'avais affligée.
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
7 Et je mettrai la boiteuse, pour être un résidu, et celle qui était éloignée, pour être une nation robuste; l'Eternel régnera sur eux en la montagne de Sion dès cette heure-là à toujours.
Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
8 Et toi, Tour du troupeau, Hophel, la fille de Sion viendra jusqu'à toi; et la première domination viendra, le Royaume, [dis-je], viendra à la fille de Jérusalem.
Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
9 Pourquoi t'écries-tu maintenant si fort? N'y a-t-il point de Roi au milieu de toi? Ou ton conseiller est-il péri, que la douleur t'ait saisie comme de celle qui enfante?
Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
10 Sois en travail, et crie, fille de Sion, comme celle qui enfante; car tu sortiras bientôt de la ville, et tu demeureras aux champs, et viendras jusqu'à Babylone; [mais] là tu seras délivrée; là l'Eternel te rachètera des mains de tes ennemis.
Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
11 Et maintenant se sont assemblées contre toi plusieurs nations qui disent: Qu'elle soit profanée, et que notre œil voie en Sion [ce qu'il y voudrait voir].
Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
12 Mais ils ne connaissent point les pensées de l'Eternel, et n'entendent point son conseil; car il les a assemblées comme des gerbes dans l'aire.
Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
13 Lève-toi, et foule, fille de Sion, car je ferai que ta corne sera de fer, et je ferai que tes ongles seront d'airain; et tu menuiseras plusieurs peuples, et je dédierai comme un interdit leur gain à l'Eternel, et leurs biens au Seigneur de toute la terre.
“Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.