< Marc 10 >

1 Puis étant parti de là, il vint sur les confins de la Judée, au delà du Jourdain, et les troupes s'étant encore assemblées auprès de lui, il les enseignait comme il avait accoutumé.
Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
2 Alors des Pharisiens vinrent à lui, et pour l'éprouver ils lui demandèrent: est-il permis à un homme de répudier sa femme?
Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 Il répondit, et leur dit: qu'est-ce que Moïse vous a commandé?
Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
4 Ils dirent: Moïse a permis d'écrire la Lettre de divorce, et de répudier [ainsi sa femme].
Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 Et Jésus répondant leur dit: il vous a donné ce commandement à cause de la dureté de votre cœur.
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 Mais au commencement de la création, Dieu fit un homme et une femme.
Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
7 C'est pourquoi l'homme laissera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme;
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
8 Et les deux seront une seule chair: ainsi ils ne sont plus deux, mais une seule chair.
Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9 Que l'homme donc ne sépare pas ce que Dieu a joint.
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 Puis ses Disciples l'interrogèrent encore sur cela même dans la maison.
Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
11 Et il leur dit: quiconque laissera sa femme, et se mariera à une autre, il commet un adultère contre elle.
Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
12 Pareillement si la femme laisse son mari, et se marie à un autre, elle commet un adultère.
Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
13 Et on lui présenta de petits enfants, afin qu'il les touchât; mais les Disciples reprenaient ceux qui les présentaient;
Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
14 Et Jésus voyant cela, en fut indigné, et il leur dit: laissez venir à moi les petits enfants, et ne les en empêchez point; car le Royaume de Dieu appartient à ceux qui leur ressemblent.
Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
15 En vérité, je vous dis, que quiconque ne recevra pas comme un petit enfant le Royaume de Dieu, il n'y entrera point.
Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
16 Après les avoir donc pris entre ses bras, il les bénit, en posant les mains sur eux.
Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
17 Et comme il sortait pour se mettre en chemin, un homme accourut, et se mit à genoux devant lui, et lui fit cette demande: Maître qui es bon, que ferai-je pour hériter la vie éternelle? (aiōnios g166)
Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
18 Et Jésus lui répondit: pourquoi m'appelles-tu bon? il n'y a nul être qui soit bon que Dieu.
Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 Tu sais les Commandements: Ne commets point adultère. Ne tue point. Ne dérobe point. Ne dis point de faux témoignage. Ne fais aucun tort à personne. Honore ton père et ta mère.
Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
20 Il répondit, et lui dit: Maître, j'ai gardé toutes ces choses dès ma jeunesse.
Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 Et Jésus ayant jeté l'œil sur lui, l'aima, et lui dit: il te manque une chose; va, et vends tout ce que tu as, et le donne aux pauvres, et tu auras un trésor au ciel; puis viens, et me suis, ayant chargé la croix.
Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 Mais il fut fâché de ce mot, et s'en alla tout triste, parce qu'il avait de grands biens.
Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Alors Jésus ayant regardé alentour, dit à ses Disciples: combien difficilement ceux qui ont des richesses entreront-ils dans le Royaume de Dieu.
Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
24 Et ses Disciples s'étonnèrent de ces paroles; mais Jésus prenant encore la parole, leur dit: mes enfants, qu'il est difficile à ceux qui se confient aux richesses d'entrer dans le Royaume de Dieu!
Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
25 Il est plus aisé qu'un chameau passe par le trou d'une aiguille, qu'il ne l'est qu'un riche entre dans le Royaume de Dieu.
Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 Et ils s'en étonnèrent encore davantage, disant entre eux: et qui peut être sauvé?
Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
27 Mais Jésus les ayant regardés, leur dit: cela est impossible quant aux hommes, mais non pas quant à Dieu; car toutes choses sont possibles à Dieu.
Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
28 Alors Pierre se mit à lui dire: voici, nous avons tout quitté, et t'avons suivi.
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
29 Et Jésus répondant, dit: en vérité je vous dis, qu’il n'y a personne qui ait laissé ou maison, ou frères, ou sœurs, ou père, ou mère, ou femme, ou enfants, ou champs, pour l'amour de moi, et de l’Evangile,
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
30 Qui n'en reçoive maintenant en ce temps-ci cent fois autant, maisons, et frères, et sœurs, et mère, et enfants, et champs, avec des persécutions; et dans le siècle à venir, la vie éternelle. (aiōn g165, aiōnios g166)
ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Mais plusieurs qui sont les premiers, seront les derniers; et les derniers seront les premiers.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 Or ils étaient en chemin, montant à Jérusalem, et Jésus allait devant eux; et ils étaient épouvantés, et craignaient en le suivant, parce que Jésus ayant encore pris à l'écart les douze, s'était mis à leur déclarer les choses qui lui devaient arriver;
Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
33 [Disant]: voici, nous montons à Jérusalem; et le Fils de l'homme sera livré aux principaux Sacrificateurs, et aux Scribes; et ils le condamneront à mort, et le livreront aux Gentils;
Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
34 Qui se moqueront de lui, et le fouetteront, et cracheront contre lui, puis ils le feront mourir; mais il ressuscitera le troisième jour.
ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
35 Alors Jacques et Jean, fils de Zébédée, vinrent à lui, en lui disant: Maître, nous voudrions que tu fisses pour nous ce que nous te demanderons.
Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
36 Et il leur dit: que voulez-vous que je fasse pour vous?
Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
37 Et ils lui dirent: accorde-nous que dans ta gloire nous soyons assis l'un à ta droite, et l'autre à ta gauche.
Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
38 Et Jésus leur dit: vous ne savez ce que vous demandez; pouvez-vous boire la coupe que je dois boire; et être baptisés du Baptême dont je dois être baptisé?
Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
39 Ils lui répondirent: nous le pouvons. Et Jésus leur dit: il est vrai que vous boirez la coupe que je dois boire, et que vous serez baptisés du Baptême dont je dois être baptisé;
Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
40 Mais d'être assis à ma droite et à ma gauche, ce n'est pas à moi de le donner; mais [il sera donné] à ceux à qui il est préparé.
lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
41 Ce que les dix [autres] ayant ouï, ils conçurent de l'indignation contre Jacques et Jean.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 Et Jésus les ayant appelés, leur dit: vous savez que ceux qui dominent sur les nations les maîtrisent, et que les Grands d'entre eux usent d'autorité sur elles.
Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
43 Mais il n'en sera pas ainsi entre vous; mais quiconque voudra être le plus grand entre vous, sera votre serviteur.
Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
44 Et quiconque d'entre vous voudra être le premier, sera le serviteur de tous.
na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
45 Car aussi le Fils de l'homme n'est pas venu pour être servi, mais pour servir, et pour donner sa vie en rançon pour plusieurs.
Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
46 Puis ils arrivèrent à Jéricho; et comme il partait de Jéricho avec ses Disciples et une grande troupe, un aveugle, [appelé] Bartimée, [c'est-à-dire], fils de Timée, était assis sur le chemin, et mendiait.
Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
47 Et ayant entendu que c'était Jésus le Nazarien, il se mit à crier, et à dire: Jésus, Fils de David, aie pitié de moi.
Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Et plusieurs le censuraient fortement, afin qu'il se tût; mais il criait encore plus fort: Fils de David, aie pitié de moi!
Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Et Jésus s'étant arrêté, dit qu'on l'appelât. On l'appela donc, en lui disant: prends courage, lève-toi, il t'appelle.
Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
50 Et jetant bas son manteau, il se leva, et s'en vint à Jésus.
Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
51 Et Jésus prenant la parole, lui dit: que veux-tu que je te fasse? Et l'aveugle lui dit: Maître, que je recouvre la vue.
Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
52 Et Jésus lui dit: Va, ta foi t'a sauvé. Et sur-le-champ il recouvra la vue, et il suivit Jésus par le chemin.
Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.

< Marc 10 >