< Luc 5 >

1 Or il arriva, comme la foule se jetait toute sur lui pour entendre la parole de Dieu, qu'il se tenait sur le bord du lac de Génézareth.
Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
2 Et voyant deux nacelles qui étaient au bord du lac, et dont les pêcheurs étaient descendus, et lavaient leurs rets, il monta dans l'une de ces nacelles, qui était à Simon.
akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
3 Et il le pria de la mener un peu loin de terre; puis s'étant assis, il enseignait les troupes de dessus la nacelle.
Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
4 Et quand il eut cessé de parler, il dit à Simon: mène en pleine eau, et lâchez vos filets pour pêcher.
Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
5 Et Simon répondant, lui dit: Maître, nous avons travaillé toute la nuit, et nous n'avons rien pris; toutefois à ta parole je lâcherai les filets.
Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
6 Ce qu'ayant fait, ils enfermèrent une si grande quantité de poissons, que leurs filets se rompaient.
Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
7 Et ils firent signe à leurs compagnons qui étaient dans l'autre nacelle, de venir les aider; et étant venus, ils remplirent les deux nacelles, tellement qu'elles s'enfonçaient.
Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
8 Et quand Simon-Pierre eut vu cela, il se jeta aux genoux de Jésus, en lui disant: Seigneur, retire-toi de moi; car je suis un homme pécheur.
Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
9 Parce que la frayeur l'avait saisi, lui et tous ceux qui étaient avec lui, à cause de la prise de poissons qu'ils venaient de faire; de même que Jacques et Jean, fils de Zébédée, qui étaient compagnons de Simon.
Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
10 Alors Jésus dit à Simon: n'aie point de peur; dorénavant tu seras un pêcheur d'hommes vivants.
Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
11 Et quand ils eurent amené les nacelles à terre, ils quittèrent tout, et le suivirent.
Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
12 Or il arriva que comme il était dans une des villes [de ce pays-là], voici, un homme plein de lèpre voyant Jésus, se jeta [en terre] sur sa face, et le pria, disant: Seigneur, si tu veux, tu peux me rendre net.
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 Et [Jésus] étendit la main, et le toucha, en disant: je le veux, sois net; et incontinent la lèpre le quitta.
Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
14 Et il lui commanda de ne le dire à personne; mais va, lui dit-il, et te montre au Sacrificateur, et offre pour ta purification ce que Moïse a commandé, pour leur servir de témoignage.
Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
15 Et sa renommée se répandait de plus en plus, tellement que de grandes troupes s'assemblaient pour l'entendre, et pour être guéries par lui de leurs maladies.
Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 Mais il se tenait retiré dans les déserts, et priait.
Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
17 Or il arriva un jour qu'il enseignait, que des Pharisiens et des Docteurs de la Loi, qui étaient venus de toutes les bourgades de Galilée, et de Judée, et de Jérusalem, étaient là assis, et la puissance du Seigneur était là pour opérer des guérisons.
Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
18 Et voici des hommes qui portaient dans un lit un homme qui était paralytique, et ils cherchaient le moyen de le porter dans la maison, et de le mettre devant lui.
Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
19 Mais ne trouvant point par quel côté ils pourraient l'introduire, à cause de la foule, ils montèrent sur la maison, et ils le descendirent par les tuiles, avec le petit lit, au milieu devant Jésus;
Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
20 Qui voyant leur foi, dit au paralytique: homme, tes péchés te sont pardonnés.
Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
21 Alors les Scribes et les Pharisiens commencèrent à raisonner en eux-mêmes, disant: qui est celui-ci qui prononce des blasphèmes? Qui est-ce qui peut pardonner les péchés, que Dieu seul?
Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
22 Mais Jésus connaissant leurs pensées, prit la parole, et leur dit: pourquoi raisonnez-vous ainsi en vous-mêmes?
Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
23 Lequel est le plus aisé, ou de dire: tes péchés te sont pardonnés; ou de dire: lève-toi, et marche?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
24 Or afin que vous sachiez que le Fils de l'homme a le pouvoir sur la terre de pardonner les péchés, il dit au paralytique: je te dis, lève-toi, charge ton petit lit, et t'en va en ta maison.
Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
25 Et à l'instant [le paralytique] s'étant levé devant eux, chargea le lit où il était couché, et s'en alla en sa maison, glorifiant Dieu.
Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
26 Et ils furent tous saisis d'étonnement, et ils glorifiaient Dieu, et étant remplis de crainte, ils disaient: certainement nous avons vu aujourd'hui des choses qu'on n'eût jamais attendues.
Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
27 Après cela il sortit, et il vit un péager nommé Lévi, assis au lieu du péage, et il lui dit: suis-moi.
Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
28 Lequel abandonnant tout, se leva, et le suivit.
Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
29 Et Lévi fit un grand festin dans sa maison, où il y avait une grosse assemblée de péagers, et d'autres gens qui étaient avec eux à table.
Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
30 Et les Scribes de ce lieu-là et les Pharisiens, murmuraient contre ses Disciples, en disant: pourquoi est-ce que vous mangez et que vous buvez avec des péagers et des gens de mauvaise vie?
Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
31 Mais Jésus prenant la parole, leur dit: ceux qui sont en santé n'ont pas besoin de médecin, mais ceux qui se portent mal.
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
32 Je ne suis point venu appeler à la repentance les justes, mais les pécheurs.
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
33 Ils lui dirent aussi: pourquoi est-ce que les disciples de Jean jeûnent souvent, et font des prières; pareillement aussi ceux des Pharisiens; mais les tiens mangent et boivent?
Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
34 Et il leur dit: pouvez-vous faire jeûner les amis de l'Epoux pendant que l'Epoux est avec eux?
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
35 Mais les jours viendront que l'Epoux leur sera ôté; alors ils jeûneront en ces jours-là.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
36 Puis il leur dit cette similitude: personne ne met une pièce d'un vêtement neuf à un vieux vêtement; autrement le neuf déchire [le vieux], et la pièce du neuf ne se rapporte point au vieux.
Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
37 Pareillement, personne ne met le vin nouveau dans de vieux vaisseaux; autrement le vin nouveau rompra les vaisseaux, et se répandra, et les vaisseaux seront perdus.
Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
38 Mais le vin nouveau doit être mis dans des vaisseaux neufs; et ainsi ils se conservent l'un et l'autre.
Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 Et il n'y a personne qui boive du vieux, qui veuille aussitôt du nouveau: car il dit: le vieux est meilleur.
Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”

< Luc 5 >