< Luc 19 >

1 Et [Jésus] étant entré dans Jéricho, allait par la ville.
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 Et voici un homme appelé Zachée, qui était principal péager, et qui était riche,
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 Tâchait de voir lequel était Jésus, mais il ne pouvait à cause de la foule, car il était petit.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 C'est pourquoi il accourut devant, et monta sur un sycomore pour le voir; car il devait passer par là.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 Et quand Jésus fut venu à cet endroit-là, regardant en haut, il le vit, et lui dit: Zachée, descends promptement; car il faut que je demeure aujourd'hui dans ta maison.
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 Et il descendit promptement, et le reçut avec joie.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 Et tous voyant cela murmuraient, disant qu'il était entré chez un homme de mauvaise vie pour y loger.
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 Et Zachée se présentant là, dit au Seigneur: Voici, Seigneur, je donne la moitié de mes biens aux pauvres; et si j'ai fait tort à quelqu'un en quelque chose, j'en rends le quadruple.
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 Et Jésus lui dit: aujourd'hui le salut est entré dans cette maison; parce que celui-ci aussi est fils d'Abraham.
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 Car le Fils de l'homme est venu chercher et sauver ce qui était perdu.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 Et comme ils entendaient ces choses, Jésus poursuivit son discours, et proposa une parabole, parce qu'il était près de Jérusalem, et qu'ils pensaient qu'à l'instant le Règne de Dieu devait être manifesté.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 Il dit donc: un homme noble s'en alla dans un pays éloigné, pour se mettre en possession d'un Royaume, mais dans la vue de revenir.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 Et ayant appelé dix de ses serviteurs, il leur donna dix marcs d'argent et leur dit: Faites-les valoir jusqu'à ce que je vienne.
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 Or ses citoyens le haïssaient: c'est pourquoi ils envoyèrent après lui une députation, pour dire: nous ne voulons pas que celui-ci règne sur nous.
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 Il arriva donc après qu'il fut retourné, et qu'il se fut mis en possession du Royaume, qu'il commanda qu'on lui appelât ces serviteurs à qui il avait confié [son] argent, afin qu'il sût combien chacun aurait gagné par son trafic.
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 Alors le premier vint, disant: Seigneur, ton marc a produit dix autres marcs.
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 Et il lui dit: cela va bien, bon serviteur; parce que tu as été fidèle en peu de chose, aie puissance sur dix villes.
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 Et un autre vint, disant: Seigneur, ton marc en a produit cinq autres.
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 Et il dit aussi à celui-ci: et toi, sois établi sur cinq villes.
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 Et un autre vint, disant: Seigneur, voici ton marc que j'ai tenu enveloppé dans un linge;
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 Car je t'ai craint, parce que tu es un homme sévère; tu prends ce que tu n'as point mis, et tu moissonnes ce que tu n'as point semé.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 Et il lui dit: méchant serviteur, je te jugerai par ta propre parole: tu savais que je suis un homme sévère, prenant ce que je n'ai point mis, et moissonnant ce que je n'ai point semé;
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 Pourquoi donc n'as-tu pas mis mon argent à la banque, et à mon retour je l'eusse retiré avec l'intérêt?
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 Alors il dit à ceux qui étaient présents: Otez-lui le marc, et donnez-le à celui qui a les dix.
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 Et ils lui dirent: Seigneur, il a dix marcs.
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 Ainsi je vous dis, qu'à chacun qui aura, il sera donné; et à celui qui n'a rien, cela même qu'il a, lui sera ôté.
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Au reste, amenez ici ces ennemis qui n'ont pas voulu que je régnasse sur eux, et tuez-les devant moi.
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 Et ayant dit ces choses, il allait devant [eux], montant à Jérusalem.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 Et il arriva comme il approchait de Bethphagé et de Béthanie, vers la montagne appelée des oliviers, qu'il envoya deux de ses Disciples,
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 En leur disant: allez à la bourgade qui est vis-à-vis de vous, et y étant entrés, vous trouverez un ânon attaché, sur lequel jamais homme n'est monté; détachez-le, et amenez-le-moi.
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 Que si quelqu'un vous demande pourquoi vous le détachez, vous lui direz ainsi: c'est parce que le Seigneur en a besoin.
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 Et ceux qui étaient envoyés s'en allèrent, et trouvèrent [l'ânon] comme il le leur avait dit.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 Et comme ils détachaient l'ânon, les maîtres leur dirent: pourquoi détachez-vous cet ânon?
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 Ils répondirent: le Seigneur en a besoin.
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 Ils l'emmenèrent donc à Jésus, et ils jetèrent leurs vêtements sur l'ânon; puis ils mirent Jésus dessus.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 En même temps qu'il marchait, ils étendaient leurs vêtements par le chemin.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 Et lorsqu'il fut proche de la descente de la montagne des oliviers, toute la multitude des Disciples se réjouissant, se mit à louer Dieu à haute voix, pour tous les miracles qu'ils avaient vus;
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 Disant: béni soit le Roi qui vient au Nom du Seigneur; que la paix soit dans le ciel, et la gloire dans les lieux très-hauts.
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 Et quelques-uns d'entre les Pharisiens de la troupe lui dirent: Maître, reprends tes Disciples.
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 Et Jésus répondant, leur dit: je vous dis que si ceux-ci se taisent, les pierres mêmes crieront.
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 Et quand il fut proche, voyant la ville, il pleura sur elle, en disant:
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 O! si toi aussi eusses connu, au moins en cette tienne journée, les choses qui appartiennent à ta paix! mais maintenant elles sont cachées devant tes yeux.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Car les jours viendront sur toi que tes ennemis t'environneront de tranchées, ils t'enfermeront, et t'enserreront de tous côtés;
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 Et te raseront, toi et tes enfants qui sont au-dedans de toi, et ils ne laisseront en toi pierre sur pierre, parce que tu n'as point connu le temps de ta visitation.
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 Puis étant entré au Temple, il commença à chasser dehors ceux qui y vendaient et qui y achetaient.
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 Leur disant: il est écrit: ma Maison est la Maison de prière; mais vous en avez fait une caverne de voleurs.
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 Et il était tous les jours enseignant dans le Temple, et les principaux Sacrificateurs et les Scribes, tâchaient de le faire mourir.
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 Mais ils ne trouvaient rien qu'ils lui pussent faire; car tout le peuple était fort attentif à l'écouter.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luc 19 >