< Lévitique 14 >

1 L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
Bwana akamwambia Mose,
2 C'est ici la loi du lépreux pour le jour de la purification; il sera amené au Sacrificateur.
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 Et le Sacrificateur sortira hors du camp, et le regardera; et s'il aperçoit que la plaie de la lèpre soit guérie au lépreux,
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 Le Sacrificateur commandera qu'on prenne pour celui qui doit être nettoyé, deux passereaux vivants [et] nets, avec du bois de cèdre, et du cramoisi, et de l'hysope,
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 Et le Sacrificateur commandera qu'on coupe la gorge à l'un des passereaux sur un vaisseau de terre, sur de l'eau vive.
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 Puis il prendra le passereau vivant, le bois de cèdre, le cramoisi, et l'hysope; et il trempera [toutes ces choses] avec le passereau vivant, dans le sang de l'autre passereau qui aura été égorgé sur de l'eau vive.
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 Et il en fera aspersion par sept fois sur celui qui doit être nettoyé de la lèpre, et le nettoiera, et il laissera aller par les champs, le passereau vivant.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 Et celui qui doit être nettoyé lavera ses vêtements, et rasera tout son poil, et se lavera dans l'eau, et il sera net, et ensuite il entrera au camp, mais il demeurera sept jours hors de sa tente.
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 Et au septième jour il rasera tout son poil, sa tête, sa barbe, les sourcils de ses yeux, tout son poil; il rasera, [dis-je], tout son poil; puis il lavera ses vêtements et sa chair, et il sera net.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 Et au huitième jour il prendra deux agneaux sans tare, et une brebis d'un an sans tare, et trois dixièmes de fine farine à faire le gâteau, pétrie à l'huile, et un log d'huile.
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 Et le Sacrificateur qui fait la purification, présentera celui qui doit être nettoyé, et ces choses-là, devant l'Eternel à l'entrée du Tabernacle d'assignation.
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 Puis le Sacrificateur prendra l'un des agneaux, et l'offrira en offrande pour le délit avec un log d'huile, et tournoiera ces choses devant l'Eternel, en oblation tournoyée.
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 Et il égorgera l'agneau au lieu où l'on égorge [l'offrande] pour le péché, et l'holocauste, dans le lieu saint; car [l'offrande pour] le délit appartient au Sacrificateur, comme [l'offrande pour] le péché; c'est une chose très-sainte.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 Et le Sacrificateur prendra du sang [de l'offrande pour] le délit, et le mettra sur le mol de l'oreille droite de celui qui doit être nettoyé, et sur le pouce de sa main droite, et sur le gros orteil de son pied droit.
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 Puis le Sacrificateur prendra de l'huile du log, et en versera dans la paume de sa main gauche.
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 Et le Sacrificateur trempera le doigt de sa main droite en l'huile qui est dans sa paume gauche, et fera aspersion de l'huile avec son doigt sept fois devant l'Eternel.
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 Et du reste de l'huile qui sera dans sa paume, le Sacrificateur en mettra sur le mol de l'oreille droite de celui qui doit être nettoyé, et sur le pouce de sa main droite, et sur le gros orteil de son pied droit, sur le sang pris de [l'offrande pour le] délit.
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 Mais ce qui restera de l'huile sur la paume du Sacrificateur, il le mettra sur la tête de celui qui doit être nettoyé; et ainsi le Sacrificateur fera propitiation pour lui devant l'Eternel.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 Ensuite le Sacrificateur offrira [l'offrande pour] le péché, et fera propitiation pour celui qui doit être nettoyé de sa souillure; puis il égorgera l'holocauste.
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 Et le Sacrificateur offrira l'holocauste et le gâteau sur l'autel, et fera propitiation pour celui qui doit être nettoyé; et il sera net.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 Mais s'il est pauvre, et s'il n'a pas le moyen de fournir ces choses, il prendra un agneau en offrande tournoyée pour le délit, afin de faire propitiation pour soi, et un dixième de fine farine pétrie à l'huile, pour le gâteau, avec un log d'huile;
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 Et deux tourterelles ou deux pigeonneaux, selon qu'il pourra fournir, dont l'un sera pour le péché, et l'autre pour l'holocauste.
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 Et le huitième jour de sa purification il les apportera au Sacrificateur à l'entrée du Tabernacle d'assignation, devant l'Eternel.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 Et le Sacrificateur recevra l'agneau [de l'offrande pour] le délit, et le log d'huile, et les tournoiera devant l'Eternel en offrande tournoyée.
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Et il égorgera l'agneau de [l'offrande pour le] délit; puis le Sacrificateur prendra du sang de [l'offrande pour le] délit, et le mettra sur le mol de l'oreille droite de celui qui doit être nettoyé, et sur le pouce de sa main droite, et sur le gros orteil de son pied droit.
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 Puis le Sacrificateur versera de l'huile dans la paume de sa main gauche.
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 Et avec le doigt de sa main droite il fera aspersion de l'huile qui est dans sa main gauche, sept fois devant l'Eternel.
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 Et il mettra de cette huile qui est dans sa paume, sur le mol de l'oreille droite de celui qui doit être nettoyé, et sur le pouce de sa main droite, et sur le gros orteil de son pied droit, sur le lieu du sang pris de [l'offrande pour le] délit.
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 Après il mettra le reste de l'huile qui est dans sa paume sur la tête de celui qui doit être nettoyé, afin de faire propitiation pour lui devant l'Eternel.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 Puis il sacrifiera l'une des tourterelles, ou l'un des pigeonneaux, selon ce qu'il aura pu fournir.
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 De ce donc qu'il aura pu fournir, l'un sera pour le péché, et l'autre pour l'holocauste, avec le gâteau; ainsi le Sacrificateur fera propitiation devant l'Eternel pour celui qui doit être nettoyé.
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 Telle est la loi de celui auquel il y a une plaie de lèpre, et qui n'a pas le moyen de fournir à sa purification.
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 Puis l'Eternel parla à Moïse et à Aaron, en disant:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 Quand vous serez entrés au pays de Canaan, que je vous donne en possession, si j'envoie une plaie de lèpre en quelque maison du pays que vous posséderez;
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 Celui à qui la maison appartiendra viendra, et le fera savoir au Sacrificateur, en disant: Il me semble que j'aperçois comme une plaie en ma maison.
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 Alors le Sacrificateur commandera qu'on vide la maison avant qu'il y entre pour regarder la plaie; afin que rien de ce qui est dans la maison ne soit souillé, puis le Sacrificateur entrera pour voir la maison.
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 Et il regardera la plaie, et s'il aperçoit que la plaie qui est aux parois de la maison, ait quelques fossettes tirant sur le vert, ou roussâtres, qui soient, à les voir, plus enfoncées que la paroi;
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 Le Sacrificateur sortira de la maison, à l'entrée, et fera fermer la maison pendant sept jours.
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 Et au septième jour le Sacrificateur retournera, et la regardera, et s'il aperçoit que la plaie se soit étendue sur les parois de la maison;
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 Alors il commandera d'arracher les pierres, auxquelles est la plaie, et de les jeter hors de la ville dans un lieu souillé.
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 Il fera aussi racler l'enduit de la maison par dedans tout à l'entour, et l'enduit qu'on aura raclé, on le jettera hors de la ville en un lieu souillé.
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 Puis on prendra d'autres pierres, et on les apportera au lieu des [premières] pierres, et on prendra d'autre mortier pour r'enduire la maison.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 Mais si la plaie retourne et boutonne en la maison, après qu'on aura arraché les pierres, et après qu'on l'aura raclée, et r'enduite,
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 Le Sacrificateur y entrera, et la regardera, et s'il aperçoit que la plaie soit accrue en la maison, c'est une lèpre rongeante en la maison; elle est souillée.
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 On démolira donc la maison, ses pierres, et son bois, avec tout son mortier, et on les transportera hors de la ville en un lieu souillé.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 Et si quelqu'un est entré dans la maison, pendant tout le temps que le Sacrificateur l'avait faite fermer, il sera souillé jusqu'au soir.
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 Et celui qui dormira dans cette maison lavera ses vêtements; celui aussi qui mangera dans cette maison lavera ses vêtements.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 Mais quand le Sacrificateur y sera entré, et qu'il aura aperçu que la plaie n'a point crû en cette maison, après l'avoir faite r'enduire, il jugera la maison nette; car sa plaie est guérie.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 Alors il prendra pour purifier la maison, deux passereaux, du bois de cèdre, du cramoisi, et de l'hysope.
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 Et il coupera la gorge à l'un des passereaux sur un vaisseau de terre, sur de l'eau vive.
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 Et il prendra le bois de cèdre, l'hysope, le cramoisi, et le passereau vivant, et trempera le tout dans le sang du passereau qu'on aura égorgé, et dans l'eau vive; puis il fera aspersion dans la maison par sept fois.
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 Il purifiera donc la maison avec le sang du passereau, et avec l'eau vive, et avec le passereau vivant, le bois de cèdre, l'hysope, et le cramoisi.
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 Puis il laissera aller hors de la ville par les champs le passereau vivant, et il fera propitiation pour la maison; et elle sera nette.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 Telle est la loi de toute plaie de lèpre, et de teigne;
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 De lèpre de vêtement, et de maison;
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 De tumeur, de gâle, et de bouton;
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 Pour enseigner en quel temps une chose est souillée, et en quel temps elle est nette; telle est la loi de la lèpre.
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Lévitique 14 >