< Juges 1 >
1 Or il arriva qu'après la mort de Josué les enfants d'Israël consultèrent l'Eternel, en disant: Qui de nous montera le premier contre les Cananéens pour leur faire la guerre?
Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
2 Et l'Eternel répondit: Juda montera; voici, j'ai livré le pays entre ses mains.
Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
3 Et Juda dit à Siméon son frère: Monte avec moi en mon partage, et nous ferons la guerre aux Cananéens; et j'irai aussi avec toi en ton partage. Ainsi Siméon alla avec lui.
Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
4 Juda donc monta, et l'Eternel livra les Cananéens et les Phérésiens entre leurs mains; et ils battirent en Bézec dix mille hommes.
Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
5 Or ayant trouvé Adoni-bézec en Bézec, ils combattirent contre lui, et frappèrent les Cananéens et les Phérésiens.
Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
6 Et Adoni-bézec s'enfuit, mais ils le poursuivirent; et l'ayant pris, ils lui coupèrent les pouces de ses mains et de ses pieds.
Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
7 Alors Adoni-bézec dit: Soixante et dix Rois, dont les pouces des mains et des pieds avaient été coupés, ont recueilli [du pain] sous ma table; comme j'ai fait, Dieu m'a ainsi rendu; et ayant été amené à Jérusalem, il y mourut.
Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
8 Or les enfants de Juda avaient fait la guerre contre Jérusalem, et l'avaient prise, et ils avaient fait passer [ses habitants] au tranchant de l'épée, et mis la ville en feu.
Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
9 Puis les enfants de Juda étaient descendus pour faire la guerre aux Cananéens, qui habitaient dans les montagnes, et au Midi, et dans la plaine.
Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
10 Juda donc s'en était allé contre les Cananéens qui habitaient à Hébron; or le nom d'Hébron était auparavant Kirjath-Arbah; et il avait frappé Sesaï, Ahiman et Talmaï.
Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
11 Et de là il était allé contre les habitants de Débir, le nom de laquelle était auparavant Kirjath-sépher.
Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
12 Et Caleb avait dit: Qui frappera Kirjath-sépher et la prendra, je lui donnerai ma fille Hacsa pour femme.
Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
13 Et Hothniël, fils de Kénas, frère puîné de Caleb, la prit; et [Caleb] lui donna sa fille Hacsa pour femme.
Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
14 Et il arriva que comme elle s'en allait, elle l'incita à demander à son père un champ; puis elle descendit impétueusement de dessus son âne; et Caleb lui dit: Qu'as-tu?
Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
15 Et elle lui répondit: Donne-moi un présent; puisque tu m'as donné une terre sèche, donne-moi aussi des sources d'eaux. Et Caleb lui donna les fontaines [du quartier] de dessus, et les fontaines [du quartier] de dessous.
Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
16 Or les enfants du Kénien, beau-père de Moïse, étaient montés de la ville des palmes avec les enfants de Juda, au désert de Juda, qui est au Midi de Harad; parce qu'ils avaient marché et demeuré avec le peuple.
Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
17 Puis Juda s'en alla avec Siméon son frère, et ils frappèrent les Cananéens qui habitaient à Tsephath, et la détruisirent à la façon de l'interdit, c'est pourquoi on appela la ville du nom de Horma.
Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
18 Juda prit aussi Gaza avec ses confins; Askelon avec ses confins; et Hékron avec ses confins.
Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
19 Et l'Eternel fut avec Juda, et ils dépossédèrent [les habitants] de la montagne: mais ils ne dépossédèrent point les habitants de la vallée, parce qu'ils avaient des chariots de fer.
Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
20 Et on donna, selon que Moïse l'avait dit, Hébron à Caleb; qui en déposséda les trois fils de Hanak.
Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
21 Quant aux enfants de Benjamin, ils ne dépossédèrent point le Jébusien qui habitait à Jérusalem; c'est pourquoi le Jébusien a habité avec les enfants de Benjamin à Jérusalem jusqu'à ce jour.
Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
22 Ceux aussi de la maison de Joseph montèrent contre Bethel, et l'Eternel fut avec eux.
Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
23 Et ceux de la maison de Joseph firent reconnaître Bethel, dont le nom était auparavant, Luz.
Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
24 Et les espions virent un homme qui sortait de la ville, auquel ils dirent: Nous te prions de nous montrer un endroit par où l'on puisse entrer dans la ville, et nous te ferons grâce.
wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
25 Il leur montra donc un endroit par où l'on pouvait entrer dans la ville, et ils la firent passer au tranchant de l'épée; mais ils laissèrent aller cet homme-là, et toute sa famille.
Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
26 Puis cet homme s'en étant allé au pays des Héthiens, y bâtit une ville, et l'appela Luz, qui est son nom jusqu'à ce jour.
Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
27 Manassé aussi ne déposséda point [les habitants] de Beth-séan, ni des villes de son ressort, ni [les habitants] de Tahanac, ni des villes de son ressort; ni les habitants de Dor, ni des villes de son ressort; ni les habitants de Jibléham, ni des villes de son ressort, ni les habitants de Meguiddo, ni des villes de son ressort; et les Cananéens osèrent encore habiter en ce pays-là.
Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
28 Il est vrai qu'il arriva que quand Israël fut devenu plus fort, il rendît les Cananéens tributaires; mais il ne les déposséda pas entièrement.
Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
29 Ephraïm aussi ne déposséda point les Cananéens qui habitaient à Guézer; mais les Cananéens habitèrent avec lui à Guézer.
Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
30 Zabulon ne déposséda point les habitants de Kitron, ni les habitants de Nahalol; mais les Cananéens habitèrent avec lui, et lui furent tributaires.
Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
31 Aser ne déposséda point les habitants de Hacco, ni les habitants de Sidon, ni d'Ahlab, ni d'Aczib, ni d'Helba, ni d'Aphik, ni de Rehob.
Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
32 Mais ceux d'Aser habitèrent parmi les Cananéens habitants du pays; car ils ne les dépossédèrent point.
na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
33 Nephthali ne déposséda point les habitants de Beth-sémes, ni les habitants de Beth-hanath, mais il habita parmi les Cananéens habitants du pays; et les habitants de Beth-sémes, et de Beth-hanath lui furent tributaires.
Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
34 Et les Amorrhéens tinrent les enfants de Dan fort resserrés dans la montagne, et ils ne souffraient point qu'ils descendissent dans la vallée.
Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
35 Et ces Amorrhéens-là osèrent encore habiter à Har-Hérés, à Ajalon, et à Sahalbim; mais la main de la maison de Joseph étant devenue plus forte, ils furent rendus tributaires.
Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
36 Or la contrée des Amorrhéens [était] depuis la montée de Hakrabbim, depuis la roche, et au-dessus.
Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.