< Juges 8 >
1 Alors les hommes d'Ephraïm lui dirent: Que veut dire ce que tu nous as fait, de ne nous avoir pas appelés quand tu es allé à la guerre contre Madian; et ils s'emportèrent fortement contre lui.
Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
2 Et il leur répondit: Qu'ai-je fait maintenant au prix de ce que vous avez fait? Les grappillages d'Ephraïm ne sont-ils pas meilleurs que la vendange d'Abihézer?
Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
3 Dieu a livré entra vos mains les chefs de Madian, Horeb et Zééb; or qu'ai-je pu faire au prix de ce que vous avez fait? et leur esprit fut apaisé envers lui quand il leur eut ainsi parlé.
Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
4 Or Gédeon étant arrivé au Jourdain le passa, lui et les trois cents hommes qui étaient avec lui, lesquels tout las qu'ils étaient, poursuivaient [l'ennemi].
Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
5 C'est pourquoi il dit aux gens de Succoth: Donnez, je vous prie, au peuple qui me suit, quelques pains car ils sont las; et ainsi je poursuivrai Zébah et Tsalmunah, Rois de Madian.
Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
6 Mais les principaux de Succoth répondirent: La paume de Zébah et celle de Tsalmunah sont-elles maintenant en ta main, que nous donnions du pain à ton armée?
Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
7 Et Gédeon dit: Quand donc l'Eternel aura livré Zébah et Tsalmunah en ma main, je froisserai alors votre chair avec des épines du désert, et avec des chardons.
Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
8 Puis de là il monta à Pénuël, et il tint les mêmes discours à ceux de Pénuël. Et les gens de Pénuël lui répondirent comme les gens de Succoth avaient répondu.
Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
9 Il parla donc aussi aux hommes de Pénuël, en disant: Quand je retournerai en paix, je démolirai cette tour.
Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
10 Or Zébah et Tsalmunah étaient à Karkor, et leurs armées avec eux, environ quinze mille hommes, qui étaient tous ceux qui étaient restés de toute l'armée des Orientaux; car il en était tombé morts six vingt mille hommes tirant l'épée.
Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
11 Et Gédeon monta par le chemin de ceux qui habitent dans les tentes, du côté oriental de Nobah et de Jogbeha, et défit l'armée, qui se croyait assurée.
Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
12 Et comme Zébah et Tsalmunah s'enfuyaient, il les poursuivit, et prit les deux Rois de Madian, Zébah et Tsalmunah, et mit en déroute toute l'armée.
Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
13 Puis Gédeon fils de Joas retourna de la bataille de la montée de Hèrés.
Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
14 Et prenant un garçon de Succoth, il l'interrogea; [et] ce garçon lui donna par écrit les principaux de Succoth, et ses Anciens, [au nombre] de soixante dix-sept hommes.
Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
15 Et il s'en vint aux gens de Succoth, et leur dit: Voici Zébah et Tsalmunah, au sujet desquels vous m'avez insulté, en disant: La paume de Zébah et celle de Tsalmunah sont-elles maintenant en ta main, que nous donnions du pain à tes gens fatigués?
Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
16 Il prit donc les Anciens de la ville, et des épines du désert, et des chardons, et il en froissa les hommes de Succoth.
Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
17 Or il avait démoli la tour de Pénuël, et mis à mort les gens de la ville.
Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
18 Puis il dit à Zébah et à Tsalmunah: Comment [étaient faits] ces hommes que vous avez tués sur le Tabor? Ils répondirent: Ils étaient entièrement comme toi; chacun d'eux avait l'air d'un fils de Roi.
Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
19 Et il leur dit: C'étaient mes frères, enfants de ma mère; l'Eternel est vivant, si vous leur eussiez sauvé la vie, je ne vous tuerais pas.
Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
20 Puis il dit à Jéther son premier-né: Lève-toi, tue-les; mais le jeune garçon ne tira point son épée, car il avait peur, parce qu'il était encore jeune garçon.
Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
21 Et Zébah et Tsalmunah dirent: Lève-toi toi-même, et te jette sur nous; car tel qu'est l'homme, telle est sa force. Et Gédeon se leva, et tua Zébah et Tsalmunah, et prit les colliers qui étaient aux cous de leurs chameaux.
Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
22 Et ceux d'Israël dirent tous d'un accord à Gédeon: Domine sur nous, tant toi que ton fils, et le fils de ton fils; car tu nous as délivrés de la main de Madian.
Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
23 Et Gédeon leur répondit: Je ne dominerai point sur vous, ni mon fils ne dominera point sur vous; l'Eternel dominera sur vous.
Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
24 Mais Gédeon leur dit: Je vous ferai une prière, qui est que vous me donniez chacun de vous les bagues qu'il a eues du butin; car les ennemis avaient des bagues d'or, parce qu'ils étaient Ismaélites.
Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
25 Et ils répondirent: Nous les donnerons très-volontiers; et étendant un manteau ils y jetèrent chacun les bagues qu'ils avaient eues du butin.
Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
26 Et le poids des bagues d'or qu'il avait demandées, fut de mille sept cents [sicles] d'or, sans les colliers, les bœttes de senteur, et les vêtements d'écarlate qui étaient sur les Rois de Madian, et sans les chaînes qui étaient aux cous de leurs chameaux.
Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
27 Puis Gédeon en fit un Ephod; et le mit en sa ville, qui était Hophra; et tout Israël paillarda après lui en ce lieu-là; ce qui tourna en piège à Gédeon, et à sa maison.
Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
28 Ainsi Madian fut humilié devant les enfants d'Israël, et n'éleva plus sa tête; et le pays fut en repos quarante ans aux jours de Gédeon.
Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
29 Jérubbahal donc fils de Joas s'en vint [en sa ville], et se tint en sa maison.
Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
30 Or Gédeon eut soixante et dix fils, sortis de sa hanche, parce qu'il eut plusieurs femmes.
Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
31 Et sa concubine, qui était à Sichem, lui enfanta aussi un fils, et il le nomma Abimélec.
Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
32 Puis Gédeon, fils de Joas, mourut en bonne vieillesse, et fut enseveli au sépulcre de Joas son père à Hophra des Abihézérites.
Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
33 Et il arriva après que Gédeon fut mort, que les enfants d'Israël se détournèrent, et paillardèrent après les Bahalins, et s'établirent Bahal-bérith pour Dieu.
Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
34 Ainsi les enfants d'Israël ne se souvinrent point de l'Eternel leur Dieu, qui les avait délivrés de la main de tous leurs ennemis qui les environnaient.
Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
35 Et ils n'usèrent d'aucune gratuité envers la maison de Jérubbahal Gédeon, selon tout le bien qu'il avait fait à Israël.
Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.