< Josué 8 >
1 Puis l'Eternel dit à Josué: Ne crains point, et ne t'effraye de rien. Prends avec toi tout le peuple propre à la guerre, et te lève, monte contre Haï; regarde, j'ai livré entre tes mains le Roi de Haï, et son peuple, et sa ville, et son pays.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Usiogope; usivunjike moyo. Chukua pamoja nawe watu wa vita. Pandeni kwenda Ai. Tazama nimemtia mkononi mwako mfalme wa Ai, watu wake, mji wake na nchi yake.
2 Et tu feras à Haï, et à son Roi, comme tu as fait à Jérico, et à son Roi: seulement vous en pillerez pour vous le butin, et les bêtes. Mets des gens en embuscade derrière la ville.
Mtafanya hivyo pia huko Ai na mfalme wake kama mlivyofanya kwa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mtachukua nyara na mifugo kwa ajili yenu. Pangeni mashambulizi ya uviziaji nyuma ya mji.”
3 Josué donc se leva avec tout le peuple propre à la guerre, pour monter contre Haï, et Josué choisit trente mille hommes forts et vaillants, et les envoya de nuit.
Basi Yoshua aliinuka na akawachukua kwenda Ai watu wote wa vita. Kisha Yoshua akachagua watu elfu thelathini - wenye nguvu na ujasiri - na aliwatuma waende wakati wa usiku.
4 Et il leur commanda, disant: Voyez, vous qui serez en embuscade derrière la ville, ne vous éloignez pas beaucoup de la ville, mais tenez-vous prêts.
Aliwaamuru, “Tazama, mtalala katika hali ya mashambulizi ya uviziaji dhidi ya mji, kwa nyuma yake. Usiende mbali sana na mji, lakini ninyi nyote muwe tayari.
5 Et moi, et tout le peuple qui est avec moi, nous nous approcherons de la ville, et quand ils sortiront à notre rencontre, comme [ils ont fait] la première fois, nous nous enfuirons de devant eux.
Mimi pamoja na watu wote walio pamoja nami tutaukaribia mji. Na wakati watakapokuja kutushambulia sisi, tutawakimbia kama tulivyofanya hapo mwanzo.
6 Ainsi ils sortiront après nous, jusqu'à ce que nous les ayons attirés hors de la ville; car ils diront: Ils fuient devant nous comme la première fois; parce que nous fuirons devant eux.
Watatoka nje watukimbize mpaka hapo tutakapokuwa tumewavuta mbali sana na mji, watasema, “Wanatukimbia kama walivyofanya mara ya mwisho.' Hivyo tutawakimbia na kwenda mbali.
7 Mais vous vous lèverez de l'embuscade, et vous vous saisirez de la ville; car l'Eternel votre Dieu la livrera entre vos mains.
Kisha mtapanda kutoka sehemu mliyojificha, na mtauteka mji. Yahweh Mungu wenu atawapa mkononi mwenu.
8 Et quand vous l'aurez prise, vous y mettrez le feu; vous ferez selon la parole de l'Eternel. Regardez, je vous l'ai commandé.
Tazama nimewaamuru, mtakapouteka mji, mtauchoma moto. Mtayafanya haya wakati mtakapotii agizo lililotolewa katika neno la Yahweh.”
9 Josué donc les envoya, et ils allèrent se mettre en embuscade, et se tinrent entre Béthel et Haï, à l'Occident de Haï; mais Josué demeura cette nuit-là avec le peuple.
Yoshua akawatuma, na wakaenda sehemu ya uviziajia, na wakajificha kati ya Betheli na Ai sehemu ya magharibi ya Ai. Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku ule.
10 Puis Josué se leva de bon matin, et dénombra le peuple; et il monta lui et les anciens d'Israël, devant le peuple vers Haï.
Yoshua aliamka asubuhi na mapema na akawaandaa tayari wanajeshi wake, Yoshua na wazee wa Israeli walishambuliwa watu wa Ai.
11 Et tout le peuple propre à la guerre, qui [était] avec lui, monta, et s'approcha, et ils vinrent vis-à-vis de la ville, et se campèrent du côté du Septentrion de Haï; et la vallée était entre lui et Haï.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda na kuukaribia mji. Walisogea karibu na mji na wakapiga kambi sehemu ya kasikazini mwa Ai. Kulikuwa na bonde kati yao na Ai.
12 Il prit aussi environ cinq mille hommes, lesquels il mit en embuscade entre Béthel et Haï, à l'Occident de Haï.
Alichukua watu wapatao elfu tano hivi na akawaweka katika hali ya kuvizia katika upande wa magharibi mwa mji kati ya Betheli na Ai.
13 Et le peuple mit tout le camp qui était du côté du Septentrion contre la ville, et l'embuscade, à l'Occident de la ville; et cette nuit-là Josué s'avança dans la vallée.
Waliwapanga wanajeshi wote, jeshi kuu katika upande wa kasikazini mwa mji, na walinzi wa nyuma upande wa magharibi mwa mji. Yoshua alilala bondeni usiku ule.
14 Or il arriva qu'aussitôt que le Roi de Haï l'eut vu, les hommes de la ville se hâtèrent, et se levèrent de bon matin, et au temps marqué le Roi et tout son peuple sortirent à la campagne contre Israël pour le combattre. Or il ne savait pas qu'il y eût des gens en embuscade contre lui derrière la ville.
Na ilikuwa alipoona hilo mfalme wa Ai, yeye pamoja na jeshi lake, waliamka asubuhi na mapema na walitoka kwa haraka kwenda kuwashambulia Israeli katika eneo linalokabili bonde la Mto Yordani. Hakujua kuwa kulikuwa na shambulizi la kuvizia lilikuwa linasubiria kushambulia kutokea kwa nyuma ya mji.
15 Alors Josué et tout Israël [feignant d'être] battus à leur rencontre s'enfuirent par le chemin du désert.
Yoshua na Waisraeli wote walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu, na wakakimbia kuelekea nyikani.
16 C'est pourquoi tout le peuple qui était dans la ville, fut assemblé à grand cri pour les poursuivre; et ils poursuivirent Josué; et ils furent [ainsi] attirés hors de la ville;
Watu wote waliokuwa kwenye mji waliitwa kwa pamoja waende mbele yao, na walienda mbele ya Yoshua na kwa jinsi hiyo walivutwa mbali na mji.
17 De sorte qu'il ne resta pas un seul homme dans Haï ni dans Béthel qui ne sortît après Israël; ils laissèrent la ville ouverte, et ils poursuivirent Israël.
Hapakuwa na mtu mme aliyesalia Ai na Betheli ambaye alikuwa hajaenda nje kuwafuatilia waisraeli. Na walipokuwa wanawafuatilia Waisraeli, Wakatoka na waliuacha mji wazi.
18 Alors l'Eternel dit à Josué: Etends l'étendard qui est en ta main, vers Haï; car je la livrerai entre tes mains, et Josué étendit vers la ville l'étendard qui était en sa main.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Nyosha mkuki huo ulio mkononi mwako kuelekea Ai, kwa kuwa nitaitia Ai mikononi mwako.” Yoshua akaunyosha mkuki uliokuwa mkononi mwake kuuelekea mji.
19 Et ceux qui étaient en embuscade se levèrent incontinent du lieu où ils étaient; ils commencèrent à courir aussitôt que [Josué] eut étendu sa main; ils vinrent dans la ville, la prirent, et ils se hâtèrent de mettre le feu dans la ville.
Wanajeshi waliojificha katika hali ya kuvizia walitoka upesi katika eneo lao mara tu alipounyosha mkono wake. Walikimbia mbio na kuuingia mji na kuuteka. Na kwa haraka wakauchoma moto mji.
20 Et les gens de Haï se tournant derrière eux, regardèrent; et voici, la fumée de la ville montait jusqu'au ciel: et il n'y eut en eux aucune force pour fuir: et le peuple qui fuyait vers le désert, se tourna contre ceux qui le poursuivaient.
Watu wa Ai waligeuka na kuangalia nyuma. Waliona moshi kutoka katika mji ukipanda kwenda angani, na hawakuweza kutoroka kwa njia hii au ile. Kwa kuwa wanajeshi wa Israelei waliokuwa wamekimbia katika nyika, sasa walirudi kuwakabili wale waliokuwa wanawafuatilia.
21 Et Josué et tout Israël voyant que ceux qui étaient en embuscade avaient pris la ville, et que la fumée de la ville montait, se retournèrent, et frappèrent les gens de Haï.
Na wakati Yoshua na Israeli wote walipoona kuwa wale watu wa kuvizia wameuteka mji kwa ule moshi uliokuwa ukipanda, waligeuka nyuma na kuwaua watu wa Ai.
22 Les autres aussi sortirent de la ville contr'eux; ainsi ils furent [enveloppés] par les Israélites, les uns deçà, et les autres delà; et ils furent tellement battus qu'on n'en laissa aucun qui demeurât en vie, ou qui échappât.
Na wanajeshi wengine wa Israeli, wale waliokuwa wameingia ndani ya mji, walitoka nje ili kuwashambulia. Hivyo, watu wa Ai walikamatwa katikati ya majeshi ya Israeli, baadhi katika upande huu na wengine katika upande ule.
23 Ils prirent aussi vif le Roi de Haï, et le présentèrent à Josué.
Lakini walimhifadhi mfalme wa Ai, ambaye walimteka akiwa hai, na kisha wakamleta kwa Yoshua.
24 Et quand les Israélites eurent achevé de tuer tous les habitants de Haï sur les champs, au désert où ils les avaient poursuivis, et que tous furent tombés sous le tranchant de l'épée, jusqu'à être entièrement défaits, tous les Israélites se tournèrent vers Haï, et la frappèrent au tranchant de l'épée.
Ilikuwa baada ya Israeli walipokuwa wamemaliza kuuwaua wenyeji wote wa Ai katika uwanda kariibu na nyika mahali walipowafuata, na baada ya wao wote, hata yule wa mwisho, walipokuwa wamekwisha kulala kwa ncha ya upanga, Waisraeli wote walirudi Ai. Waliuteka mji kwa ncha ya upanga.
25 Et tous ceux qui tombèrent ce jour-là, tant des hommes que des femmes, furent [au nombre de] douze mille, tous gens de Haï.
Wale wote walikufa siku hiyo walikuwa watu elfu kumi na mbili elfu, wanaume na wanawake, wote ni watu wa Ai.
26 Et Josué ne retira point sa main, laquelle il avait élevée en haut avec l'étendard, qu'on n'eut entièrement défait à la façon de l'interdit, tous les habitants de Haï.
Yoshua hakuukunja mkono wake ambao alikuwa ameunyosha huku akishikilia mkuki wake, mpaka pale alipowateketeza kabisa watu wote wa Ai.
27 Seulement les Israélites pillèrent pour eux les bêtes et le butin de cette ville-là, suivant ce que l'Eternel avait commandé à Josué.
Waisraeli walichukua tu wanyama na nyara kutoka katika mji kwa ajili yao wenyewe, kama Yahweh alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 Josué donc brûla Haï, et la mit en un monceau perpétuel [de ruines], et en un désert, jusqu'à aujourd'hui.
Yoshua aliichoma Ai na kuigeuza kuwa kichuguu cha mapango. Ni mahali palipoachwa ukiwa hata leo.
29 Puis il fit pendre le Roi de Haï à une potence, jusqu'au temps du soir: et comme le soleil se couchait, Josué fit commandement, qu'on descendît de la potence son corps mort, lequel on jeta à l'entrée de la porte de la ville, et on dressa sur lui un grand amas de pierres, [qui y est demeuré] jusqu'à aujourd'hui.
Alimtundika mfalme wa Ai juu ya mti mpaka jioni. Na jua lilipokuwa linaenda kuzama, Yoshua aliwaagiza na wakautoa mwili wa mfalme wakaushusha chini ya mti na kuutupa mbele ya malango ya mji. Huko wakaweka kichuguu kikubwa cha mawe juu yake. Kichuguu hicho kimebaki huko hata leo.
30 Alors Josué bâtit un autel à l'Eternel, le Dieu d'Israël, sur la montagne de Hébal;
Kisha Yoshua akajenga madhabahu kwa Yahweh, Mungu wa Israeli katika Mlima wa Ebali,
31 Comme Moïse serviteur de l'Eternel l'avait commandé aux enfants d'Israël, ainsi qu'il est écrit au Livre de la Loi de Moïse. Il fit cet autel de pierres entières sur lesquelles personne n'avait levé le fer; et ils offrirent dessus des holocaustes à l'Eternel, et sacrifièrent des sacrifices de prospérités.
kama vile Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza watu wa Israeli, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa: “Madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna mtu yeyote aliyetumia zana ya chuma.” Na allimtolea Yahweh sadaka ya kuteketezwa juu yake na wakatoa sadaka ya amani.
32 Il écrivit aussi là sur des pierres un double de la Loi de Moïse, laquelle [Moïse] avait mise par écrit devant les enfants d'Israël.
Na huko aliandika juu ya mawe nakala ya sheria za Musa mbele ya watu wa Israeli.
33 Et tout Israël, et ses anciens, et ses Officiers, et ses juges étaient au deçà et au delà de l'Arche, vis-à-vis des Sacrificateurs qui sont de la race de Lévi, portant l'Arche de l'alliance de l'Eternel, tant les étrangers que les Hébreux naturels; une moitié étant contre la montagne de Guérizim, et l'autre moitié contre la montagne de Hébal, comme Moïse serviteur de l'Eternel l'avait commandé, pour bénir le peuple d'Israël la première fois.
Waisraeli wote, wazee wao, maafisa, na waamuzi wao walisimama katika sehemu mbili za sanduku mbele ya makuhani na Walawi ambao hulibeba sanduku la Agano la Yahweh - wageni pamoja na wazalia, nusu yao walisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu walisimama mbele ya Mlima Ebali. Waliwabariki watu wa Israeli kama Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza hapo mwanzo.
34 Et après cela il lut tout haut toutes les paroles de la Loi, tant les bénédictions que les malédictions, selon tout ce qui est écrit au Livre de la Loi.
Baada ya hayo, Yoshua alisoma maneno yote ya sheria, baraka na laana, kama zilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.
35 Il n'y eut rien de tout ce que Moïse avait commandé, que Josué ne lût tout haut devant toute l'assemblée d'Israël, des femmes, et des petits enfants, et des étrangers conversant parmi eux.
Halikusalia hata neno moja katika yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua ambalo halikusomwa mbele ya kusanyiko la Waisraeli lilojumuisha wanawake, watoto wadogo na wageni walioishi miongoni mwao.