< Josué 7 >

1 Mais les enfants d'Israël se rendirent coupables au sujet de l'interdit: car Hacan fils de Carmi, fils de Zabdi, fils de Zara, de la Tribu de Juda, prit de l'interdit, et la colère de l'Eternel s'enflamma contre les enfants d'Israël.
Lakini Waisraeli hawakuwa waaminifu kuhusu vile vitu vilivyowekwa wakfu; Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, alivichukua baadhi ya hivyo vitu. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli.
2 Car Josué envoya de Jérico des hommes vers Haï, qui [était] près de Bethaven du côté de l'Orient de Béthel, et leur parla, en disant: Montez, et reconnaissez le pays. Ces hommes donc montèrent et reconnurent Haï.
Basi Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko waende Ai, karibu na Beth-Aveni mashariki ya Betheli, akawaambia, “Pandeni mkaipeleleze nchi.” Basi wale watu wakapanda wakaipeleleza Ai.
3 Et étant retournés vers Josué, ils lui dirent: Que tout le peuple n'y monte point [mais qu']environ deux mille ou trois mille hommes y montent, et ils battront Haï. Ne fatigue point tout le peuple [en l'envoyant] là; car ils sont peu de gens.
Waliporudi kwa Yoshua, wakasema, “Si lazima watu wote waende kupigana na Ai. Watume watu elfu mbili au tatu wakauteke huo mji. Usiwachoshe watu wote, kwa sababu huko kuna watu wachache tu.”
4 Ainsi environ trois mille hommes du peuple y montèrent, mais ils s'enfuirent de devant ceux de Haï.
Basi wakapanda kama watu elfu tatu tu, lakini wakashambuliwa na watu wa Ai,
5 Et ceux de Haï en tuèrent environ trente-six hommes; car ils les poursuivirent depuis le devant de la porte jusqu'à Sébarim, et les battirent en une descente; et le cœur du peuple se fondit, et devint comme de l'eau.
ambao waliwaua watu kama thelathini na sita miongoni mwao. Wakawafukuza Waisraeli kutoka lango la mji hadi Shebarimu, nao wakawauwa huko kwenye materemko. Kutokana na hili mioyo ya watu ikayeyuka ikawa kama maji.
6 Alors Josué déchira ses vêtements, et se jeta, le visage contre terre, devant l'Arche de l'Eternel, jusqu'au soir, lui et les Anciens d'Israël, et ils jetèrent de la poudre sur leur tête.
Ndipo Yoshua akayararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana, na akabakia hapo mpaka jioni. Wazee wa Israeli nao wakafanya vivyo hivyo wakatia mavumbi vichwani mwao.
7 Et Josué dit: Hélas! Seigneur Eternel, pourquoi as-tu fait [si magnifiquement] passer le Jourdain à ce peuple, pour nous livrer entre les mains de l'Amorrhéen, [et] nous faire périr? Ô que n'avons-nous eu dans l'esprit [de demeurer], et que ne sommes-nous demeurés au delà du Jourdain!
Yoshua akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, kwa nini umewavusha watu hawa ngʼambo ya Yordani ili kututia mikononi mwa Waamori watuangamize? Laiti tungeliridhika kukaa ngʼambo ile nyingine ya Yordani!
8 Hélas! Seigneur, que dirai-je, puisque Israël a tourné le dos devant ses ennemis?
Ee Bwana, niseme nini sasa, ikiwa sasa Israeli ameshafukuzwa na adui zake?
9 Les Cananéens et tous les habitants du pays l'entendront, et nous envelopperont, et ils retrancheront notre nom de dessus la terre; et que feras-tu à ton grand Nom?
Wakanaani na watu wengine wa nchi watasikia habari hii, nao watatuzunguka na kutufutilia jina letu duniani. Utafanya nini basi kwa ajili ya jina lako mwenyewe lililo kuu?”
10 Alors l'Eternel dit à Josué: Lève-toi; pourquoi te jettes-tu ainsi le visage [contre terre]?
Bwana akamwambia Yoshua, “Simama! Unafanya nini hapo chini kifudifudi?
11 Israël a péché; ils ont transgressé mon alliance que je leur avais commandée, même ils ont pris de l'interdit; même ils [en] ont dérobé; même ils ont menti, et même ils l'ont mis dans leurs hardes.
Israeli ametenda dhambi. Wamekiuka agano langu nililowaamuru kulishika. Wamechukua baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu, wameiba, wamesema uongo, wameviweka pamoja na mali zao.
12 C'est pourquoi les enfants d'Israël ne pourront subsister devant leurs ennemis; ils tourneront le dos devant leurs ennemis; car ils sont devenus un interdit. Je ne serai plus avec vous si vous n'exterminez d'entre vous l'interdit.
Ndiyo sababu Waisraeli hawawezi kusimama dhidi ya adui zao. Wanawapa visogo na kukimbia kwa kuwa wanastahili maangamizi. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka mwangamize kila kitu miongoni mwenu kilichotengwa kwa maangamizi.
13 Lève-toi; sanctifie le peuple, et dis: Sanctifiez-vous pour demain; car ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël; il y a de l'interdit parmi toi, ô Israël! tu ne pourras subsister devant tes ennemis jusqu'à ce que vous ayez ôté l'interdit d'entre vous.
“Nenda, ukawatakase watu. Waambie, ‘Jitakaseni mjiandae kwa kesho; kwa sababu hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Kitu kilichowekwa wakfu kipo katikati yenu, ee Israeli. Hamwezi kusimama dhidi ya adui zenu mpaka mtakapokiondoa.
14 Vous vous approcherez donc le matin selon vos Tribus; et la Tribu que l'Eternel aura saisie s'approchera selon les familles; et la famille que l'Eternel aura saisie s'approchera selon les maisons; et la maison que l'Eternel aura saisie, s'approchera selon les têtes.
“‘Asubuhi, mjihudhurishe kabila kwa kabila. Itakuwa kabila lile atakalolitwaa Bwana litakuja mbele ukoo kwa ukoo, ukoo ule atakaoutwaa Bwana utakuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ile atakayoitwaa Bwana itakuja mbele mtu kwa mtu.
15 Alors celui qui aura été saisi en l'interdit, sera brûlé au feu, lui et tout ce qui [est] à lui; à cause qu'il a transgressé l'alliance de l'Eternel, et qu'il a commis une infamie en Israël.
Yule atakayekutwa na vitu vilivyowekwa wakfu, atateketezwa kwa moto, pamoja na vitu vyote alivyo navyo. Kwa kuwa amelivunja agano la Bwana na kufanya kitu cha aibu katika Israeli!’”
16 Josué donc se leva de bon matin, et fit approcher Israël selon ses Tribus; et la Tribu de Juda fut saisie.
Kesho yake asubuhi na mapema Yoshua akawaamuru Israeli kuja mbele kabila kwa kabila; na Yuda akatwaliwa.
17 Puis il fit approcher les familles de Juda, et il saisit la famille de ceux qui étaient descendus de Zara. Puis il fit approcher par têtes la famille de ceux qui étaient descendus de Zara, et Zabdi fut saisi.
Koo za Yuda zikaja mbele, naye akawatwaa Wazera. Akaamuru ukoo wa Wazera kuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ya Zabdi ikatwaliwa.
18 Et quand il eut fait approcher sa maison par têtes, Hacan fils de Carmi, fils de Zabdi, fils de Zara, de la Tribu de Juda, fut saisi.
Yoshua akaamuru watu wa jamaa ya Zabdi kuja mbele mtu kwa mtu, naye Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akatwaliwa.
19 Alors Josué dit à Hacan: Mon fils, donne, je te prie, gloire à l'Eternel le Dieu d'Israël, et fais-lui confession; et déclare-moi, je te prie, ce que tu as fait; ne me le cache point.
Ndipo Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, mtukuze Bwana, Mungu wa Israeli, nawe ukiri kwake. Niambie ni nini ulichotenda; usinifiche.”
20 Et Hacan répondit à Josué, et dit: J'ai péché, il est vrai, contre l'Eternel le Dieu d'Israël, et j'ai fait telle et telle chose.
Akani akamjibu Yoshua, “Ni kweli! Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana, Mungu wa Israeli. Hili ndilo nililofanya:
21 J'ai vu parmi le butin un beau manteau de Sinhar, deux cents sicles d'argent, et un lingot d'or du poids de cinquante sicles; je les ai convoités, [je les ai] pris; et voilà ces choses [sont] cachées en terre au milieu de ma tente, et l'argent est sous le manteau.
Nilipoona katika nyara joho zuri la kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kabari ya dhahabu ya uzito wa shekeli hamsini, nikavitamani na nikavichukua. Tazama, vimefichwa ardhini ndani ya hema langu, pamoja na hiyo fedha chini yake.”
22 Alors Josué envoya des messagers qui coururent à cette tente; et voici le manteau était caché dans la tente d'Hacan, et l'argent sous le manteau.
Kwa hiyo Yoshua akatuma wajumbe, nao wakapiga mbio mpaka hemani, tazama, vile vitu vilikuwa vimefichwa hemani mwake, pamoja na ile fedha chini yake.
23 Ils les prirent donc du milieu de la tente, et les apportèrent à Josué, et à tous les enfants d'Israël, et ils les déployèrent devant l'Eternel.
Wakavichukua vile vitu toka mle hemani, wakamletea Yoshua pamoja na Waisraeli wote, na wakavitandaza mbele za Bwana.
24 Alors Josué et tout Israël avec lui, prenant Hacan fils de Zara, et l'argent, et le manteau, et le lingot d'or, et ses fils, et ses filles, et ses bœufs, et ses ânes, et ses brebis, et sa tente, et tout ce qui [était] à lui, les firent venir en la vallée de Hacor.
Basi Yoshua, pamoja na Israeli yote, wakamchukua Akani mwana wa Zera, pamoja na ile fedha, lile joho, ile kabari ya dhahabu, wanawe na binti zake, ngʼombe, punda na kondoo wake, hema yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta katika Bonde la Akori.
25 Et Josué dit: Pourquoi nous as-tu troublés? l'Eternel te troublera aujourd'hui. Et tous les Israélites l'assommèrent de pierres, et les brûlèrent au feu, après les avoir assommés de pierres.
Yoshua akasema, “Kwa nini umeleta taabu hii juu yetu? Bwana ataleta taabu juu yako leo hii.” Ndipo Israeli yote ikampiga Akani kwa mawe, na baada ya kuwapiga jamaa yake yote kwa mawe, wakawateketeza kwa moto.
26 Et ils dressèrent sur lui un grand monceau de pierres, [qui dure] jusqu'à ce jour. Et l'Eternel apaisa l'ardeur de sa colère; c'est pourquoi ce lieu-là a été appelé jusqu'à aujourd'hui, la vallée de Hacor.
Wakakusanya lundo la mawe juu ya Akani, ambalo lipo mpaka leo. Naye Bwana akageuka kutoka hasira yake kali. Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Bonde la Akori tangu siku hiyo.

< Josué 7 >