< Joël 3 >

1 Car voici, en ces jours-là et en ce temps-là auquel je ferai retourner ceux qui auront été emmenés captifs de Juda et de Jérusalem,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 J'assemblerai toutes les nations, et les ferai descendre en la vallée de Josaphat, et là j'entrerai en jugement avec eux, à cause de mon peuple, et de mon héritage d'Israël, lequel ils ont dispersé parmi les nations, et parce qu'ils ont partagé entre eux mon pays;
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 Et qu'ils ont jeté le sort sur mon peuple; et qu'ils ont donné un enfant pour une prostituée, et ont vendu la jeune fille pour du vin, qu'ils ont bu.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 Et qu'ai-je aussi affaire de vous, Tyr et Sidon, et de vous, toutes les limites de la Palestine, me rendrez-vous ma récompense, ou me voulez-vous irriter? Je vous rendrai promptement et sans délai votre récompense sur votre tête.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 Car vous avez pris mon argent et mon or, et avez emporté dans vos temples mes choses les plus précieuses, et les meilleures.
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 Et vous avez vendu les enfants de Juda, et les enfants de Jérusalem aux enfants des Grecs, afin de les éloigner de leur contrée.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Voici, je les ferai lever du lieu auquel [ils ont été transportés après que] vous les avez vendus; et je ferai retourner votre récompense sur votre tête.
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 Je vendrai donc vos fils et vos filles entre les mains des enfants de Juda, et ils les vendront à ceux de Séba, [qui les transporteront] vers une nation éloignée; car l'Eternel a parlé.
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Publiez ceci parmi les nations: Préparez la guerre; réveillez les hommes forts, que tous les gens de guerre s'approchent, et qu'ils montent.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Forgez des épées de vos hoyaux, et des javelines de vos serpes; et que le faible dise: Je suis fort.
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Amassez-vous, et venez, toutes nations d'alentour, et soyez assemblées; l'Eternel abattra là tes hommes forts.
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 Que les nations se réveillent, et qu'elles montent à la vallée de Josaphat; car je serai assis là pour juger toutes les nations d'alentour.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Mettez la faucille, car la moisson est mûre; venez, et descendez, car le pressoir est plein: les cuves regorgent, car leur malice est grande.
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Peuples, peuples, à la vallée de décision; car la journée de l'Eternel est proche dans la vallée de décision.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 Le soleil et la lune ont été obscurcis, et les étoiles ont retiré leur lueur.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 Et l'Eternel rugira de Sion, et fera ouïr sa voix de Jérusalem, et les Cieux et la terre seront ébranlés, et l'Eternel [sera] un asile à son peuple, et la force des enfants d'Israël.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 Et vous saurez que je suis l'Eternel votre Dieu, qui habite en Sion, la montagne de ma sainteté; et Jérusalem ne sera que sainteté, et les étrangers n'y passeront plus.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 Et il arrivera en ce jour-là que les montagnes distilleront le moût, et que les coteaux se fondront en lait, les eaux courront dans tous les ruisseaux de Juda, et il sortira une fontaine de la maison de l'Eternel, et elle arrosera la vallée de Sittim.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 L'Egypte sera en désolation, et l'Idumée en désert de désolation, à cause de la violence faite aux enfants de Juda, desquels ils ont répandu le sang innocent dans leur pays.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 Mais la Judée sera habitée éternellement, et Jérusalem d'âge en âge.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 Et je nettoierai leur sang que je n'avais point nettoyé; car l'Eternel habite en Sion.
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joël 3 >