< Job 29 >

1 Et Job continuant, reprit son discours sentencieux, et dit:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Oh! qui me ferait être comme j'étais autrefois, comme j'étais en ces jours où Dieu me gardait.
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Quand il faisait luire sa lampe sur ma tête, et quand je marchais parmi les ténèbres, [éclairé] par sa lumière.
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Comme j'étais aux jours de mon automne, lorsque le secret de Dieu était dans ma tente.
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Quand le Tout-puissant était encore avec moi, et mes gens autour de moi.
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Quand je lavais mes pas dans le beurre, et que des ruisseaux d'huile découlaient pour moi du rocher.
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Quand je sortais vers la porte passant par la ville, et que je me faisais préparer un siège dans la place,
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Les jeunes gens me voyant se cachaient, les vieillards se levaient, et se tenaient debout.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Les principaux s'abstenaient de parler, et mettaient la main sur leur bouche.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 Les Conducteurs retenaient leur voix, et leur langue était attachée à leur palais.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 L'oreille qui m'entendait, disait que j'étais bienheureux, et l'œil qui me voyait, déposait en ma faveur.
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Car je délivrais l'affligé qui criait, et l'orphelin qui n'avait personne pour le secourir.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 La bénédiction de celui qui s'en allait périr, venait sur moi, et je faisais que le cœur de la veuve chantait de joie.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 J'étais revêtu de la justice, elle me servait de vêtement, et mon équité m'était comme un manteau, et [comme] une tiare.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Je servais d'œil à l'aveugle, et de pieds au boiteux.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 J'étais le père des pauvres, et je m'informais diligemment de la cause qui ne m'était point connue.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Je cassais les grosses dents de l'injuste, et je lui arrachais la proie d'entre ses dents.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 C'est pourquoi je disais: Je mourrai dans mon lit, et je multiplierai mes jours comme les grains de sable.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Ma racine était ouverte aux eaux, et la rosée demeurait toute la nuit sur mes branches.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Ma gloire se renouvelait en moi, et mon arc était renforcé en ma main.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 On m'écoutait, et on attendait [que j'eusse parlé]; et lorsque j'avais dit mon avis, on se tenait dans le silence.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Ils ne répliquaient rien après ce que je disais, et ma parole se répandait sur eux [comme une rosée].
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Ils m'attendaient comme on attend la pluie; ils ouvraient leur bouche, comme après la pluie de la dernière saison.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Riais-je avec eux? ils ne le croyaient point; et ils ne faisaient point disparaître la sérénité de mon visage.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Voulais-je aller avec eux? j'étais assis au haut bout, j'étais entr'eux comme un Roi dans son armée, et comme un homme qui console les affligés.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Job 29 >