< Job 21 >
1 Mais Job répondit, et dit:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Ecoutez attentivement mon discours, et cela me tiendra lieu de consolations de votre part.
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
3 Supportez-moi, et je parlerai, et après que j'aurai parlé, moquez-vous.
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
4 Pour moi, mon discours s'adresse-t-il à un homme? si cela était, comment mon esprit ne défaudrait-il pas?
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
5 Regardez-moi, et soyez étonnés, et mettez la main sur la bouche.
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
6 Quand je pense à [mon état], j'en suis tout étonné, et un tremblement saisit ma chair.
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
7 Pourquoi les méchants vivent-ils, [et] vieillissent, et même pourquoi sont-ils les plus puissants?
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
8 Leur race se maintient en leur présence avec eux, et leurs rejetons s'élèvent devant leurs yeux.
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
9 Leurs maisons jouissent de la paix loin de la frayeur; la verge de Dieu n'est point sur eux.
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 Leur vache conçoit, et n'y manque point; leur jeune vache se décharge de son veau, et n'avorte point.
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
11 Ils font sortir devant eux leurs petits, comme un troupeau de brebis, et leurs enfants sautent.
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
12 Ils sautent au son du tambour et du violon, et se réjouissent au son des orgues.
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
13 Ils passent leurs jours dans les plaisirs, et en un moment ils descendent au sépulcre. (Sheol )
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
14 Cependant ils ont dit au [Dieu] Fort: Retire-toi de nous; car nous ne nous soucions point de la science de tes voies.
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
15 Qui est le Tout-puissant que nous le servions? et quel bien nous reviendra-t-il de l'avoir invoqué?
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
16 Voilà, leur bien n'est pas en leur puissance. Que le conseil des méchants soit loin de moi!
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
17 Aussi combien de fois arrive-t-il que la lampe des méchants est éteinte, et que l'orage vient sur eux! [Dieu] leur distribuera leurs portions en sa colère.
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
18 Ils seront comme la paille exposée au vent, et comme la balle qui est enlevée par le tourbillon.
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
19 Dieu réservera aux enfants du méchant la punition de ses violences, il la leur rendra, et il le saura.
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
20 Ses yeux verront sa ruine, et il boira [le calice de] la colère du Tout-puissant.
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
21 Et quel plaisir aura-t-il en sa maison, laquelle il laisse après soi, puisque le nombre de ses mois aura été retranché?
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
22 Enseignerait-on la science au [Dieu] Fort, à lui qui juge ceux qui sont élevés?
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
23 L'un meurt dans toute sa vigueur, tranquille et en repos;
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
24 Ses vaisseaux sont remplis de lait, et ses os sont abreuvés de moëlle.
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
25 Et l'autre meurt dans l'amertume de son âme, et n'ayant jamais fait bonne chère.
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
26 Et néanmoins ils sont couchés également dans la poudre, et les vers les couvrent.
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
27 Voilà, je connais vos pensées, et les jugements que vous formez contre moi.
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
28 Car vous dites: Où est la maison de cet homme si puissant, et où est la tente dans laquelle les méchants demeuraient?
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
29 Ne vous êtes-vous jamais informés des voyageurs, et n'avez-vous pas appris par les rapports qu'ils vous ont faits,
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
30 Que le méchant est réservé pour le jour de la ruine, pour le jour que les fureurs sont envoyées?
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
31 [Mais] qui le reprendra en face de sa conduite? et qui lui rendra le mal qu'il a fait?
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
32 Il sera néanmoins porté au sépulcre, et il demeurera dans le tombeau.
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
33 Les mottes des vallées lui sont agréables; et tout le monde s'en va à la file après lui, et des gens sans nombre marchent au-devant de lui.
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
34 Comment donc me donnez-vous des consolations vaines, puisqu'il y a toujours de la prévarication dans vos réponses?
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”