< Jérémie 48 >

1 Quant à Moab; ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: malheur à Nébo, car elle a été saccagée! Kiriathajim a été rendue honteuse, et a été prise; la haute retraite a été rendue honteuse et effrayée.
Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
2 Moab ne se glorifiera plus de Hesbon; car on a machiné du mal contre elle, [en disant]: venez, et exterminons-la, [et] qu'elle ne soit plus nation; toi aussi Madmen tu seras détruite, et l'épée te poursuivra.
Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Il y a un bruit de crierie de devers Horonajim, pillage et une grande défaite.
Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
4 Moab est brisé, on a fait ouïr le cri de ses petits enfants.
Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
5 Pleurs sur pleurs monteront par la montée de Luhith, car on entendra dans la descente de Horonajim ceux qui crieront à cause des plaies que les ennemis leur auront faites.
Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
6 Fuyez, [dira-t-on], sauvez vos vies; et vous serez comme de la bruyère dans un désert.
Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
7 Car parce que tu as eu confiance en tes ouvrages, et en tes trésors, tu seras prise, et Kémos sortira pour être transporté avec ses Sacrificateurs, et ses principaux.
Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
8 Et celui qui fait le dégât entrera dans toutes les villes, et pas une ville n'échappera; la vallée périra, et le plat pays sera détruit, suivant ce que l'Eternel a dit;
Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
9 Donnez des ailes à Moab; car certainement il s'envolera, et ses villes seront réduites en désolation, sans qu'il y ait personne qui [y] habite.
Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
10 Maudit soit celui qui fera l'œuvre de l'Eternel frauduleusement, et maudit soit celui qui gardera son épée de répandre le sang!
“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 Moab a été à son aise depuis sa jeunesse; il a reposé sur sa lie; il n'a point été vidé de vaisseau en vaisseau, et n'a point été transporté, c'est pourquoi sa saveur lui est toujours demeurée, et son odeur ne s'est point changée;
“Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
12 Mais voici, les jours viennent, dit l'Eternel, que je lui enverrai des gens qui l'enlèveront, qui videront ses vaisseaux, et qui mettront ses outres en pièces.
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
13 Et Moab sera honteux à cause de Kémos, comme la maison d'Israël est devenue honteuse à cause de Béthel, qui était sa confiance.
Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
14 Comment dites-vous: nous sommes forts et vaillants dans le combat?
“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
15 Moab va être saccagé, et chacune de ses villes s'en va en fumée, et l'élite de ses jeunes gens va descendre pour être égorgée, dit le Roi dont le Nom est l'Eternel des armées.
Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
16 La calamité de Moab est proche, et sa ruine s'avance à grands pas.
“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
17 Vous tous qui êtes autour de lui, soyez-en émus à compassion, et [vous] tous qui connaissez son nom, dites: comment a été rompue cette forte verge, et ce sceptre d'honneur?
Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
18 Toi qui te tiens chez la fille de Dibon, descends de ta gloire, et t'assieds dans un lieu de sécheresse; car celui qui a saccagé Moab est monté contre toi, [et] a détruit tes forteresses.
“Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
19 Habitante d'Haroher, tiens-toi sur le chemin, et contemple; interroge celui qui s'enfuit, et celle qui est échappée, [et] dis: qu'est-il arrivé?
Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
20 Moab est rendu honteux; car il a été mis en pièces; hurlez et criez, rapportez dans Arnon que Moab a été saccagé;
Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 Et que le jugement est venu sur le plat pays, sur Holon, et sur Jathsa, et sur Mephahat,
Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
22 Et sur Dibon, et sur Nebo, et sur Bethdiblathajim,
katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 Et sur Kiriathajim, et sur Beth-gamul, et sur Beth-méhon,
katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 Et sur Kérijoth, et sur Botsra, et sur toutes les villes du pays de Moab éloignées et proches.
katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 La force de Moab a été rompue, et son bras a été cassé, dit l'Eternel.
Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
26 Enivrez-le, car il s'est élevé contre l'Eternel. Moab se vautrera dans le vin qu'il aura rendu et il deviendra aussi un sujet de moquerie.
“Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
27 Car, [ô Moab!] Israël ne t'a-t-il pas été en dérision, [comme] un homme qui aurait été surpris entre les larrons? chaque fois que tu as parlé de lui, tu en as tressailli de joie.
Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
28 Habitants de Moab quittez les villes, et demeurez dans les rochers, et soyez comme le pigeon qui fait son nid aux côtés de l'entrée des cavernes.
Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
29 Nous avons appris l'orgueil de Moab le très-superbe, son arrogance et son orgueil, et sa fierté, et son cœur altier.
“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
30 J'ai connu sa fureur, dit l'Eternel; mais il n'en sera pas ainsi; [j'ai connu] ceux sur lesquels il s'appuie; ils n'ont rien fait de droit.
Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
31 Je hurlerai donc à cause de Moab, même je crierai à cause de Moab tout entier; on gémira sur ceux de Kir-hérès.
Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
32 Ô vignoble de Sibmah je pleurerai sur toi du pleur de Jahzer; tes provins ont passé au delà de la mer, ils ont atteint jusqu’à la mer de Jahzer; celui qui fait le dégât s'est jeté sur tes fruits d'Eté, et sur ta vendange.
Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
33 L'allégresse aussi, et la gaieté s'est retirée loin du champ fertile, et du pays de Moab, et j'ai fait cesser le vin des cuves; on n'y foulera plus en chantant, et la chanson de la vendange n'[y] sera plus chantée.
Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
34 A cause du cri de Hesbon qui est parvenu jusqu’à Elhalé, ils ont jeté leurs cris jusqu’à Jahats; même depuis Tsohar jusqu'à Horonajim, [comme] une génisse de trois ans; car aussi les eaux de Nimrim seront réduites en désolation.
“Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 Et je ferai qu'il n'y aura plus en Moab, dit l'Eternel, aucun qui offre sur les hauts lieux, ni aucun qui fasse des encensements à ses dieux.
Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
36 C'est pourquoi mon cœur mènera un bruit sur Moab comme des flûtes; mon cœur mènera un bruit comme des flûtes sur ceux de Kir-hérès, parce que toute l'abondance de ce qu'il a acquis est périe.
“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
37 Car toute tête sera chauve, et toute barbe sera rasée; et il y aura des incisions sur toutes les mains, et le sac sera sur les reins.
Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
38 Il y aura des lamentations sur tous les toits de Moab, et dans ses places, parce que j'aurai brisé Moab comme un vaisseau auquel on ne prend nul plaisir, dit l'Eternel.
Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
39 Hurlez, [en disant]: comment a-t-il été mis en pièces? Comment Moab a-t-il tourné le dos tout honteux? car Moab sera un objet de moquerie et de frayeur à tous ceux qui sont autour de lui.
“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
40 Car ainsi a dit l'Eternel: voici il volera comme un aigle, et il étendra ses ailes sur Moab.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
41 Kérijoth a été prise, et on s'est saisi des forteresses, et le cœur des hommes forts de Moab sera en ce jour-là comme le cœur d'une femme qui est en travail.
Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
42 Et Moab sera exterminé, tellement qu'il ne sera plus peuple, parce qu'il s'est élevé contre l'Eternel.
Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
43 Habitant de Moab, la frayeur, la fosse, et le filet sont sur toi, dit l'Eternel.
Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
44 Celui qui s'enfuira à cause de la frayeur, tombera dans la fosse; et celui qui remontera de la fosse, sera pris au filet; car je ferai venir sur lui, [c'est-à-savoir] sur Moab, l'année de leur punition, dit l'Eternel.
“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
45 Ils se sont arrêtés en l'ombre de Hesbon, voulant éviter la force; mais le feu est sorti de Hesbon, et la flamme du milieu de Sihon, qui dévorera un canton de Moab, et le sommet de la tête des gens bruyants.
“Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
46 Malheur à toi, Moab! le peuple de Kémos est perdu; car tes fils ont été enlevés pour être emmenés captifs, et tes filles pour être emmenées captives.
Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
47 Toutefois je ramènerai et mettrai en repos les captifs de Moab, aux derniers jours, dit l'Eternel. Jusqu'ici est le jugement de Moab.
“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

< Jérémie 48 >