< Jérémie 33 >

1 Et la parole de l'Eternel fut [adressée] une seconde fois à Jérémie, quand il était encore enfermé dans la cour de la prison, en disant:
Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
2 Ainsi a dit l'Eternel qui s'en va faire ceci, l'Eternel qui s'en va le former pour l'établir, le Nom duquel est l'Eternel.
“Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
3 Crie vers moi, je te répondrai, et je te déclarerai des choses grandes et cachées, lesquelles tu ne sais point.
‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
4 Car ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël, touchant les maisons de cette ville-ci, et les maisons des Rois de Juda; elles s'en vont être démolies par le moyen des terrasses, et par l'épée.
Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
5 Ils sont venus à combattre contre les Caldéens, mais ç'a été pour remplir leurs maisons des corps morts des hommes que j'ai fait frapper en ma colère et en ma fureur, et parce que j'ai caché ma face de cette ville à cause de toute leur malice.
katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
6 Voici, je m'en vais lui donner la santé et la guérison, je les guérirai, et je leur ferai voir abondance de paix et de vérité.
“‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
7 Et je ferai retourner les captifs de Juda, et les captifs d'Israël, et je les rétablirai comme auparavant.
Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
8 Et je les purifierai de toute leur iniquité, par laquelle ils ont péché contre moi; et je pardonnerai toutes leurs iniquités par lesquelles ils ont péché contre moi, et par lesquelles ils ont péché grièvement contre moi.
Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
9 Et [cette ville] me sera un sujet de réjouissance, de louange et de gloire, chez toutes les nations de la terre qui entendront parler de tout le bien que je vais leur faire, et elles seront effrayées et épouvantées à cause de tout le bien, et de toute la prospérité que je vais lui donner.
Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
10 Ainsi a dit l'Eternel: dans ce lieu-ci duquel vous dites: il est désert, n'y ayant ni homme ni bête, dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem, qui sont désolées, n'y ayant ni homme, ni habitant, ni aucune bête, on y entendra encore,
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
11 La voix de joie, et la voix d'allégresse, la voix de l'époux, et la voix de l'épouse, [et] la voix de ceux qui disent: célébrez l'Eternel des armées; car l'Eternel est bon, parce que sa miséricorde demeure à toujours, lorsqu'ils apportent des oblations d'action de grâces à la maison de l'Eternel; car je ferai retourner les captifs de ce pays, [et je les mettrai] au même état qu'auparavant, a dit l'Eternel.
sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
12 Ainsi a dit l'Eternel des armées: en ce lieu désert, où il n'y a ni homme ni bête, et dans toutes ses villes, il y aura encore des cabanes de bergers qui y feront reposer leurs troupeaux;
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
13 Dans les villes des montagnes, et dans les villes de la plaine, dans les villes du Midi, dans le pays de Benjamin, dans les environs de Jérusalem, et dans les villes de Juda; et les troupeaux passeront encore sous les mains de celui qui les compte, a dit l'Eternel.
Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
14 Voici, les jours viennent, dit l'Eternel, que je mettrai en effet la bonne parole que j'ai prononcée touchant la maison d'Israël, et la maison de Juda.
“‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
15 En ces jours-là, et en ce temps-là je ferai germer à David le Germe de justice, qui exercera le jugement et la justice en la terre.
“‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
16 En ces jours-là Juda sera délivré, et Jérusalem habitera en assurance, et c'est ici le nom dont elle sera appelée: l'Eternel notre justice.
Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
17 Car ainsi a dit l'Eternel, il ne manquera jamais à David d'homme assis sur le trône de la maison d'Israël;
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
18 Et d'entre les Sacrificateurs Lévites, il ne manquera jamais d'y avoir devant moi d'homme offrant des holocaustes, faisant les parfums de gâteau, et faisant des sacrifices tous les jours.
wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
19 Davantage la parole de l'Eternel fut [adressée] à Jérémie, en disant:
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
20 Ainsi a dit l'Eternel: Si vous pouvez abolir mon alliance touchant le jour, et mon alliance touchant la nuit, tellement que le jour et la nuit ne soient plus en leur temps;
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
21 Aussi mon alliance avec David mon serviteur sera abolie; tellement qu'il n'ait plus de fils régnant sur son trône; et avec les Lévites Sacrificateurs, faisant mon service.
basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
22 Car [comme] on ne peut compter l'armée des cieux, ni mesurer le sable de la mer, ainsi je multiplierai la postérité de David mon serviteur, et les Lévites qui font mon service.
Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
23 La parole de l'Eternel fut encore [adressée] à Jérémie, en disant:
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
24 N'as-tu pas vu ce que ce peuple a prononcé, disant: l'Eternel a rejeté les deux familles qu'il avait élues; car [par là] ils méprisent mon peuple; tellement qu'à leur compte il ne sera plus une nation?
“Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
25 Ainsi a dit l'Eternel: si [je n'ai point établi] mon alliance touchant le jour et la nuit, et si je n'ai point établi les ordonnances des cieux et de la terre;
Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
26 Aussi rejetterai-je la postérité de Jacob, et celle de David mon serviteur, pour ne prendre plus de sa postérité des gens qui dominent sur la postérité d'Abraham, d'Isaac, et de Jacob; car je ferai retourner leurs captifs, et j'aurai compassion d'eux.
basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”

< Jérémie 33 >