< Jérémie 14 >
1 La parole de l'Eternel, qui fut [adressée] à Jérémie, sur ce que [les pluies avaient été] retenues.
Neno la Bwana lilimjia Yeremia kuhusu ukame,
2 La Judée a mené deuil, et ses portes sont en un pitoyable état. Ils sont tous en deuil [gisant] par terre, et le cri de Jérusalem est monté [au ciel].
“Wayahudi waomboleze; basi milango yake ianguke. Wao wanaomboleza kwa ajili ya ardhi; Kilio chao kwa Yerusalemu kimepaa juu.
3 Et les personnes distinguées ont envoyé à l'eau les moindres d'entre eux; ils sont venus aux lieux creux, ils n'y ont point trouvé d'eau, et ils s'en sont retournés leurs vaisseaux vides; ils ont été rendus honteux et confus, et ils ont couvert leur tête.
Wenye nguvu huwatuma watumishi wao kwa ajili ya maji. Wanapoingia kwenye visima, hawawezi kupata maji. Wote wanarudi hawajafanikiwa; Wao hufunika vichwa vyao na aibu.
4 Parce que la terre s'est crevassée à cause qu'il n'y a point eu de pluie au pays; les laboureurs ont été rendus honteux, [et] ils ont couvert leur tête.
Kwa sababu hii ardhi imepasuka, kwa maana hakuna mvua katika nchi. Wakulima huwa na aibu na kufunika vichwa vyao.
5 Même la biche a fait son faon au champ et l'a abandonné, parce qu'il n'y a point d'herbe.
Kwa maana hata kunguru huwaacha wanawe katika mashamba, kwa maana hakuna nyasi.
6 Et les ânes sauvages se sont tenus sur les lieux élevés, ils ont attiré l'air comme des dragons; leurs yeux sont consumés, parce qu'il n'y a point d'herbe.
Punda mwitu husimama kwenye mabonde yaliyo wazi na hupiga upepo kama mbweha. Macho yao yanashindwa kufanya kazi, kwa maana hakuna mimea.
7 Eternel, si nos iniquités rendent témoignage contre nous, agis à cause de ton Nom, car nos rébellions sont multipliées; c'est contre toi que nous avons péché.
Hata ingawa maovu yetu yanatushuhudia, Bwana, tenda kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu matendo yetu yasiyo na imani yamezidi; tumekutenda dhambi.
8 Toi qui es l'attente d'Israël, [et] son libérateur au temps de la détresse, pourquoi serais-tu en la terre comme un étranger, et comme un voyageur qui se détourne pour passer la nuit?
Matumaini ya Israeli, yule anayemwokoa wakati wa dhiki, kwa nini utakuwa kama mgeni katika nchi, kama mtu akaaye nchi ya kigeni ambaye hujinyoosha na kutumia hutumia usiku mmoja tu?
9 Pourquoi serais-tu comme un homme étonné, et comme un homme fort qui ne peut délivrer? Or tu es au milieu de nous, ô Eternel! et ton Nom est réclamé sur nous; ne nous abandonne point.
Kwa nini utakuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, kama shujaa ambaye hawezi kuokoa mtu yeyote? Kwa maana wewe u katikati yetu, Bwana! Jina lako limetangazwa juu yetu. Usiondoke
10 L'Eternel a dit ainsi à ce peuple, parce qu'ils ont aimé à aller ainsi çà et là, et qu'ils n'ont point retenu leurs pieds, l'Eternel n'a point pris plaisir en eux, il se souviendra maintenant de leurs iniquités, et il punira leurs péchés.
Bwana awaambia hivi watu hawa “Kwa kuwa wanapenda kutanga tanga, hawakuzuia miguu yao kufanya hivyo.” Bwana hafurahi nao. Sasa anawakumbusha uovu wao na ameadhibu dhambi zao.
11 Puis l'Eternel me dit: ne fais point de requête en faveur de ce peuple.
Bwana akaniambia, Usiombe kwa ajili ya watu hawa.
12 Quand ils jeûneront, je n'exaucerai point leur cri, et quand ils offriront des holocaustes et des oblations, je n'y prendrai point de plaisir; mais je les consumerai par l'épée, et par la famine, et par la mortalité.
Maana ikiwa wanafunga, sitasikiliza kulia kwao; na wanapotoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga, sitawafurahia. Kwa maana nitawaangamiza kwa upanga, njaa, na tauni.
13 Et je dis: ah! ah! Seigneur Eternel! voici, les Prophètes leur disent: vous ne verrez point l'épée, et vous n'aurez point de famine, mais je vous donnerai une paix assurée en ce lieu-ci.
Ndipo nikasema, “Ee Bwana, Bwana! Angalia! mabii wanawaambia watu, 'Huwezi kuona upanga; hakutakuwa na njaa kwako, kwa kuwa nitakupa usalama wa kweli mahali hapa.'”
14 Et l'Eternel me dit: ce n'est que mensonge ce que ces prophètes prophétisent en mon Nom; je ne les ai point envoyés, je ne leur ai point donné de charge, et je ne leur ai point parlé; ils vous prophétisent des visions de mensonge, des divinations de néant, et des tromperies de leur cœur.
Bwana akaniambia, 'manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwafukuza, wala sikuwapa amri au kusema nao. Lakini maono ya udanganyifu na ya maana, uchawi wa udanganyifu unaotokana na akili zao ndicho wanachowahubiria.”
15 C'est pourquoi, ainsi a dit l'Eternel touchant les prophètes qui prophétisent en mon Nom, et que je n'ai point envoyés, et qui disent: l'épée ni la famine ne sera point en ce pays; ces prophètes-là seront consumés par l'épée et par la famine.
Kwa hiyo Bwana asema hivi, “Kwa habari ya manabii wakihubiri kwa jina langu, ambao mimi siwakutuma; wale wanaosema kuwa hakutakuwa na upanga wala njaa katika nchi hii mabii hawa wataangamia kwa upanga na njaa.
16 Et le peuple auquel ils ont prophétisé sera jeté par les rues de Jérusalem à cause de la famine et de l'épée; et il n'y aura personne qui les ensevelisse, tant eux que leurs femmes, leurs fils et leurs filles, et je répandrai sur eux leur méchanceté.
Na watu waliopewa utabiri watafukuzwa nje ya barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga; kwa kuwa hakuna mtu wa kuwazikas-wao, na wake zao, na wana wao, wala binti zao; kwa maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.
17 Tu leur diras donc cette parole-ci: que mes yeux se fondent en larmes nuit et jour, et qu'ils ne cessent point; car la vierge, fille de mon peuple, a été fort maltraitée, la plaie [en] est fort douloureuse.
Sema neno hili kwao 'Acha macho yangu yatokwe machozi, usiku na mchana. wala yasikome, kwa kuwa kutakuwa na kuanguka kwa bikira, binti ya watu wangu - jeraha kubwa lisilotibika.
18 Si je sors aux champs, voici les gens morts par l'épée; et si j'entre en la ville, voici les langueurs de la faim; même le Prophète et le Sacrificateur ont couru par le pays, et ils ne savent où ils en sont.
Ikiwa nitatoka kwenye shamba basi angalia! kuna wale waliouawa kwa upanga. Na kama nitakuja mjini, basi, tazama! kuna wale walio na ugonjwa wa njaa. Hata nabii na kuhani wote wanatembea juu ya nchi bila maarifa.'”
19 Aurais-tu entièrement rejeté Juda? et ton âme aurait-elle Sion en dédain? Pourquoi nous as-tu frappés tellement qu'il n'y a point de guérison? on attend la paix, et il n'y a rien de bon; et le temps de la guérison, et voici le trouble.
Je! Umemkataa kabisa Yuda? Je, unaichukia Sayuni? Kwa nini umetupiga wakati hakuna uponyaji kwetu? Tulitumaini amani, lakini hapakuwa na kitu kizuri-na kwa wakati wa uponyaji, lakini tazama, kuna hofu tu.
20 Eternel, nous reconnaissons notre méchanceté, [et] l'iniquité de nos pères; car nous avons péché contre toi.
Tunakubali, Bwana, makosa yetu, uovu wa babu zetu, kwa kuwa tumekukosea.
21 Ne nous rejette point à cause de ton Nom, et n'expose point à opprobre le trône de ta gloire; souviens-toi de ton alliance avec nous, [et] ne la romps point.
Usitukatae! Kwa ajili ya jina lako, usikifedheheshe kiti chako cha enzi cha utukufu. Kumbuka na usivunje agano lako na sisi.
22 Parmi les vanités des nations y en a-t-il qui fassent pleuvoir, et les cieux donnent-ils la menue pluie? N'est-ce pas toi qui le fais, ô Eternel notre Dieu? C'est pourquoi nous nous attendrons à toi; car c'est toi qui as fait toutes ces choses.
Je, kuna miongoni mwa sanamu za mataifa yeyote zinazoweza kuifanya mbingu kutoa mvua? Je, si wewe, Bwana Mungu wetu, ambaye hufanya jambo hili? Tunatumaini kwako, kwa kuwa umefanya mambo haya yote.