< Jérémie 13 >

1 Ainsi m'a dit l'Eternel: Va, et achète-toi une ceinture de lin, et mets-la sur tes reins, et ne la mets point dans l'eau.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
2 J'achetai donc une ceinture selon la parole de l'Eternel, et la mis sur mes reins.
Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
3 Et la parole de l'Eternel me fut [adressée] pour la seconde fois, en disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
4 Prends la ceinture que tu as achetée, et qui est sur tes reins, et te lève, et t'en va vers l'Euphrate, et la cache là dans le trou d'un rocher.
“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
5 Je m'en allai donc, et la cachai dans l'Euphrate, comme l'Eternel m'avait commandé.
Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
6 Et il arriva que plusieurs jours après l'Eternel me dit: lève-toi, et t'en va vers l'Euphrate, et reprends de là la ceinture que je t'avais commandé d'y cacher.
Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
7 Et je m'en allai vers l'Euphrate, je creusai; et je repris la ceinture du lieu où je l'avais cachée, et voici, la ceinture était pourrie, et n'était plus bonne à rien.
Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
8 Alors la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia:
9 Ainsi a dit l'Eternel: je ferai ainsi pourrir l'orgueil de Juda, et le grand orgueil de Jérusalem.
“Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 [L'orgueil] de ce peuple très méchant, qui refusent d'écouter mes paroles, et qui marchent selon la dureté de leur cœur, et vont après d'autres dieux pour les servir, et pour se prosterner devant eux, tellement qu'il sera comme cette ceinture, qui n'est bonne à aucune chose.
Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
11 Car comme une ceinture est jointe sur les reins d'un homme, je m'étais attaché toute la maison d'Israël, et toute la maison de Juda, dit l'Eternel, afin qu'ils fussent mon peuple, ma renommée, ma louange, et ma gloire; mais ils n'ont point écouté.
Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
12 Tu leur diras donc cette parole-ci: ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël: tout vaisseau sera rempli de vin; et ils te diront: ne savons-nous pas bien que tout vaisseau sera rempli de vin?
“Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
13 Mais tu leur diras: ainsi a dit l'Eternel: voici, je m'en vais remplir d'ivresse tous les habitants de ce pays, et les Rois qui sont assis sur le trône de David pour l'amour de lui, et les Sacrificateurs, et les Prophètes, et tous les habitants de Jérusalem.
Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
14 Et je les briserai l'un contre l'autre, les pères et les enfants ensemble, dit l'Eternel, je n'en aurai point de compassion, je ne les épargnerai point, et je n'en aurai point de pitié pour ne les détruire point.
Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
15 Ecoutez et prêtez l'oreille, ne vous élevez point, car l'Eternel a parlé.
Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
16 Donnez gloire à l'Eternel votre Dieu, avant qu'il fasse venir les ténèbres, et avant que vos pieds bronchent sur les montagnes dans lesquelles on ne voit pas clair; vous attendrez la lumière, et il la changera en une ombre de mort, et la réduira en obscurité.
Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
17 Que si vous n'écoutez ceci, mon âme pleurera en secret à cause de [votre] orgueil, et mon œil versera des larmes en abondance, même il se fondra en larmes, parce que le troupeau de l'Eternel aura été emmené prisonnier.
Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
18 Dis au Roi et à la Régente: humiliez-vous, et vous asseyez [sur la cendre], car votre couronne magnifique tombera de dessus vos têtes.
Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
19 Les villes du Midi sont fermées, et il n'y a personne qui les ouvre; tout Juda est transporté en captivité, il est universellement transporté.
Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
20 Levez vos yeux, et voyez ceux qui viennent de l'Aquilon. Où est le parc qui t'a été donné, et ton magnifique troupeau?
Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
21 Que diras-tu quand il te punira? car tu les as enseignés contre toi, pour être supérieurs sur ta tête; les douleurs ne te saisiront-elles point, comme elles saisissent la femme qui enfante?
Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
22 Que si tu dis en ton cœur: pourquoi me sont arrivées ces choses? C'est pour la grandeur de ton iniquité que tes habits ont été retroussés, [et] que tes talons ont été serrés de près.
Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
23 Le More changerait-il sa peau, et le léopard ses taches? pourriez-vous aussi faire quelque bien, vous qui n'êtes appris qu'à mal faire?
Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
24 C'est pourquoi je les disperserai comme du chaume, qui est emporté ça et là par le vent du désert.
“Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
25 C'est ici ton lot, et la portion que je t'ai mesurée dit l'Eternel; parce que tu m'as oublié, et que tu as mis ta confiance au mensonge,
Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 A cause de cela j'ai retroussé tes habits sur ton visage, et ton ignominie paraîtra.
Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
27 Tes adultères, et tes hennissements, l'énormité de ta prostitution est sur les collines, par les champs, j'ai vu tes abominations; malheur à toi, Jérusalem, ne seras-tu point nettoyée? jusques à quand cela durera-t-il?
uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”

< Jérémie 13 >