< Isaïe 25 >

1 Eternel, tu [es] mon Dieu, je t'exalterai, je célébrerai ton nom, car tu as fait des choses merveilleuses; les conseils pris dès longtemps [se sont trouvés être] la fermeté même.
Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
2 Car tu as fait de la ville un monceau de pierres, et de la forte cité une ruine; le palais des étrangers qui était dans la ville, ne sera jamais rebâti.
Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
3 Et à cause de cela le peuple fort te glorifiera, la ville des nations redoutables te révérera.
Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
4 Parce que tu as été la force du chétif, la force du misérable en sa détresse, le refuge contre le débordement, l'ombrage contre le hâle; car le souffle des terribles est comme un débordement [qui abattrait] une muraille.
Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
5 Tu rabaisseras la tempête éclatante des étrangers, comme le hâle [est rabaissé] dans un pays sec, le hâle, [dis-je, ] par l'ombre d'une nuée; le branchage des terribles sera abattu.
na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
6 Et l'Eternel des armées fera à tous les peuples en cette montagne un banquet de choses grasses, un banquet de vins étant sur leur mère, [un banquet, dis-je, ] de choses grasses et mœlleuses, et de vins étant sur leur mère, bien purifiés.
Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
7 Et il enlèvera en cette montagne l'enveloppe redoublée qu'on voit sur tous les peuples, et la couverture qui est étendue sur toutes les nations.
Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
8 Il détruira la mort par sa victoire; et le Seigneur l'Eternel essuiera les larmes de dessus tout visage, et il ôtera l'opprobre de son peuple de dessus toute la terre; car l'Eternel a parlé.
yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
9 Et l'on dira en ce jour-là; voici, c'est ici notre Dieu; nous l'avons attendu, aussi nous sauvera-t-il; c'est ici l'Eternel; nous l'avons attendu; nous nous égayerons, et nous réjouirons de son salut.
Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
10 Car la main de l'Eternel reposera sur cette montagne; mais Moab sera foulé sous lui, comme on foule la paille pour en faire du fumier.
Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
11 Et il étendra ses mains au travers de lui, comme celui qui nage les étend pour nager, et il rabaissera sa fierté, se faisant ouverture avec ses mains.
Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
12 Et il abaissera la forteresse des plus hautes retraites de tes murailles, il les renversera, il les jettera à terre, et les réduira en poussière.
Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

< Isaïe 25 >