< Isaïe 2 >

1 La parole qu'Esaïe fils d'Amots a vue touchant Juda et Jérusalem.
Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
2 Or il arrivera aux derniers jours que la montagne de la maison de l'Eternel sera affermie au sommet des montagnes, et qu'elle sera élevée par-dessus les coteaux, et toutes les nations y aborderont.
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
3 Et plusieurs peuples iront, et diront; venez, et montons à la montagne de l'Eternel, à la maison du Dieu de Jacob; et il nous instruira de ses voies, et nous marcherons dans ses sentiers; car la Loi sortira de Sion, et la parole de l'Eternel sortira de Jérusalem.
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
4 Il exercera le jugement parmi les nations, et il reprendra plusieurs peuples; ils forgeront de leurs épées des hoyaux, et de leurs hallebardes des serpes; une nation ne lèvera plus l'épée contre l'autre, et ils ne s'adonneront plus à la guerre.
Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
5 Venez, ô Maison de Jacob! et marchons dans la lumière de l'Eternel.
Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
6 Certes tu as rejeté ton peuple, la maison de Jacob, parce qu'ils se sont remplis d'Orient, et de pronostiqueurs, comme les Philistins; et qu'ils se sont plu aux enfants des étrangers.
Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
7 Son pays a été rempli d'argent et d'or, et il n'y a point eu de fin à ses trésors; son pays a été rempli de chevaux, et il n'[y a] point [eu] de fin à ses chariots.
Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
8 Son pays a été rempli d'idoles; ils se sont prosternés devant l'ouvrage de leurs mains, devant ce que leurs doigts ont fait.
Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
9 Et ceux du commun se sont inclinés, et les personnes de qualité se sont baissées; ne leur pardonne donc point.
Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
10 Entre dans la roche, et te cache dans la poudre, à cause de la frayeur de l'Eternel, et à cause de la gloire de sa majesté.
Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
11 Les yeux hautains des hommes seront abaissés, et les hommes qui s'élèvent seront humiliés, et l'Eternel sera seul haut élevé en ce jour-là.
Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
12 Car il y a un jour [assigné] par l'Eternel des armées contre tout orgueilleux et hautain, et contre tout homme qui s'élève, et il sera abaissé;
Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
13 Et contre tous les cèdres du Liban hauts et élevés, et contre tous les chênes de Basan;
kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
14 Et contre toutes les hautes montagnes, et contre tous les coteaux élevés;
kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
15 Et contre toute haute tour, et contre toute muraille forte;
kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
16 Et contre tous les navires de Tarsis, et contre toutes les peintures de plaisance.
kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
17 Et l'élévation des hommes sera humiliée, et les hommes qui s'élèvent seront abaissés; et l'Eternel sera seul haut élevé en ce jour-là.
Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
18 Et quant aux idoles, elles tomberont toutes.
nazo sanamu zitatoweka kabisa.
19 Et [les hommes] entreront aux cavernes des rochers, et aux trous de la terre, à cause de la frayeur de l'Eternel, et à cause de sa gloire magnifique, lorsqu'il se lèvera pour châtier la terre.
Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
20 En ce jour-là l'homme jettera aux taupes et aux chauves-souris les idoles de son argent, et les idoles de son or, qu'on lui aura faites pour se prosterner [devant elles].
Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
21 Et ils entreront dans les fentes des rochers, et dans les quartiers des rochers à cause de la frayeur de l'Eternel, et à cause de sa gloire magnifique, quand il se lèvera pour punir la terre.
Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
22 Retirez-vous de l'homme duquel le souffle est dans ses narines; car quel cas mérite-t-il qu'on en fasse?
Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?

< Isaïe 2 >