< Isaïe 16 >

1 Envoyez l'agneau au Dominateur de la terre, envoyez-le du rocher du désert, à la montagne de la fille de Sion.
Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
2 Car il arrivera que les filles de Moab seront au passage d'Arnon, comme un oiseau volant çà et là, [comme] une nichée chassée de son nid.
Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
3 Mets en avant le conseil, fais l'ordonnance, sers d'ombre comme une nuit au milieu du midi; cache ceux qui ont été chassés, et ne décèle point ceux qui sont errants.
“Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
4 Que ceux de mon peuple qui ont été chassés séjournent chez toi, ô Moab! sois leur une retraite contre celui qui fait le dégât; car celui qui usait d'extorsion a cessé, le dégât a pris fin, ceux qui foulaient sont consumés de dessus la terre.
Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
5 Et le trône sera établi par la gratuité; et sur ce trône sera assis en vérité, dans le tabernacle de David, un qui jugera, qui recherchera le droit, et qui se hâtera de faire justice.
Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
6 Nous avons entendu l'orgueil de Moab le très-orgueilleux, sa fierté, et son orgueil, et son arrogance; ceux sur qui il s'appuie ne sont rien de ferme.
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
7 C'est pourquoi Moab hurlera sur Moab, chacun hurlera; vous grommellerez pour les fondements de Kir-Haréseth; il n'y aura que des gens blessés à mort.
Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
8 Car les guérets de Hesbon, et le vignoble de Sibma, languissent; les Seigneurs des nations ont foulé ses meilleurs plants, [qui] atteignaient jusques à Jahzer, ils couraient çà et là par le désert, et ses provins s'étendaient et passaient au delà de la mer.
Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
9 C'est pourquoi je pleurerai du pleur de Jahzer, le vignoble de Sibma; je t'arroserai de mes larmes, ô Hesbon et Elhalé! car l'ennemi avec des cris s'est jeté sur tes fruits d'Eté, et sur ta moisson.
Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
10 Et la joie et la gaieté s'est retirée du champ fertile; on ne se réjouira plus, et on ne s'égayera plus dans les vignes, celui qui foulait le vin ne le foulera plus dans les cuves, j'ai fait cesser la chanson de la vendange.
Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
11 C'est pourquoi mes entrailles mèneront du bruit comme une harpe sur Moab, et mon ventre sur Kir-Hérès.
Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
12 Et il arrivera qu'on verra que Moab se lassera [pour aller] au haut lieu, et qu'il entrera en son saint lieu pour prier; mais il ne pourra rien obtenir.
Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
13 C'est là la parole que l'Eternel a prononcée depuis longtemps sur Moab.
Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
14 Et maintenant l'Eternel a parlé, en disant; dans trois ans, tels que sont les ans d'un mercenaire, la gloire de Moab sera avilie, avec toute cette grande multitude; et le résidu sera petit, ce sera peu de chose, ce ne sera rien de considérable.
Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”

< Isaïe 16 >