< Isaïe 15 >

1 La charge de Moab; parce que Har de Moab a été ravagée de nuit, il a été défait; parce que Kir de Moab a été saccagée de nuit, il a été défait.
Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
2 Il est monté à Bajith, et à Dibon, dans les hauts lieux, pour pleurer; Moab hurlera sur Nébo, et sur Médeba, toutes ses têtes seront chauves, et toute barbe sera rasée.
Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
3 On sera ceint de sacs dans ses rues, chacun hurlera fondant en larmes sur ses toits, et dans ses places.
Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
4 Hesbon et Elhalé se sont écriées, leur voix a été ouïe jusqu'à Jahats; c'est pourquoi ceux de Moab qui seront équipés [pour aller à la guerre], jetteront des cris lamentables, son âme se tourmentera au dedans de lui.
Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
5 Mon cœur crie à cause de Moab; ses fugitifs s'en sont fuis jusqu'à Tsohar, [comme] une génisse de trois ans; car on montera par la montée de Luhith avec des pleurs, et on fera retentir le cri de la plaie au chemin de Horonajim.
Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
6 Même les eaux de Nimrim ne seront que désolations, même le foin est déjà séché, l'herbe a été consumée, et il n'y a point de verdure.
Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
7 Il aura acquis des richesses en abondance, afin que ce qu'ils auront réservé soit porté dans la vallée des Arabes.
Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
8 Car le cri a environné la contrée de Moab; son hurlement [ira] jusqu'à Eglajim, et son hurlement jusqu'à Béer-Elim.
Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
9 Même les eaux de Dimon ont été remplies de sang; car j'ajouterai un surcroît sur Dimon, [savoir] le lion à ceux qui seront réchappés de Moab, et au résidu du pays.
Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

< Isaïe 15 >