< Osée 10 >
1 Israël est une vigne déserte, elle ne fait de fruit que pour elle-même, il a multiplié des autels selon la multiplication de son fruit, selon la bonté de leur pays, ils ont embelli leurs statues.
Israeli ni mzabibu mzuri ambao huzaa matunda yake. kwa kadiri matunda yake yanavyoongezeka vivyo hivyo anajenga madhabahu nyingi. Kwa kuwa nchi yake ilizalishwa zaidi, aliboresha nguzo zake.
2 Il a divisé leur cœur, ils vont être traités en coupables, il abattra leurs autels, il détruira leurs statues.
Moyo wao ni udanganyifu; sasa wanapaswa kubeba hatia yao. Bwana ataharibu madhabahu zao; ataharibu nguzo zao.
3 Car bientôt ils diront: Nous n'avons point de Roi, parce que nous n'avons point craint l'Eternel; et que nous ferait un Roi?
Kwa maana watasema, “Hatuna mfalme, kwa maana hatukumcha Bwana. Na mfalme-angeweza kutufanyia nini?”
4 Ils ont prononcé des paroles, jurant faussement quand ils ont traité alliance; c'est pourquoi le jugement germera sur les sillons des champs, comme le fiel.
Wanasema maneno tupu na kufanya maagano kwa kuapa uongo. Kwa hivyo haki inakuja kama magugu yenye sumu katika mito ya shamba.
5 Les habitants de Samarie seront épouvantés à cause des jeunes vaches de Beth-aven: car le peuple mènera deuil sur son idole; et les prêtres de ses idoles, qui s'en étaient réjouis, [mèneront deuil] à cause que sa gloire est transportée loin d'elle.
Wakazi wa Samaria wataogopa kwa sababu ya ndama za Beth Aveni. Watu wake waliomboleza juu yao, kama walivyofanya wale makuhani wa sanamu ambao walikuwa wamefurahi juu yao na utukufu wao, lakini hawako tena.
6 Même elle sera transportée en Assyrie, pour en faire présent au Roi Jareb; Ephraïm recevra de la honte, et Israël sera honteux de son conseil.
Wao watachukuliwa kwenda Ashuru kama sadaka kwa mfalme mkuu. Efraimu atakuwa na aibu, na Israeli atakuwa na aibu kwa sanamu yake.
7 Le Roi de Samarie sera retranché, comme l'écume qui est au-dessus de l'eau.
Mfalme wa Samaria ataangamizwa, kama chipu cha kuni juu ya uso wa maji.
8 Et les hauts lieux d'Aven, qui sont le péché d'Israël, seront détruits; l'épine et le chardon croîtront sur les autels; et on dira aux montagnes, Couvrez-nous; et aux coteaux: Tombez sur nous.
Sehemu za juu za uovu zitaharibiwa. Hii ndiyo dhambi ya Israeli! Miti na vichaka vitakua juu ya madhabahu zao. Watu wataiambia milima, “Tufunike sisi!” na kwa vilima, “Tuangukieni!”
9 Israël, tu as péché dès les jours de Guibha; ils s'y sont arrêtés; la bataille qui était contre les pervers, ne les empoigna point à Guibha.
Ee Israeli, umetenda dhambi tangu siku za Gibea; huko umebaki. Je, vita vitawapata wana wa uovu huko Gibea?
10 Je les châtierai selon ma volonté, et les peuples seront assemblés contre eux, parce qu'ils se sont attachés aux deux objets de leurs amours.
Nitakapotaka, nitawaadhibu. Mataifa wataungana pamoja nao na kuwaweka katika vifungo kwa uovu wao mara mbili.
11 Ephraïm est comme une jeune vache bien dressée, qui aime à fouler [le blé], mais j'ai méprisé la beauté de son cou. Je ferai qu'Ephraïm tirera [la charrue], Juda labourera, Jacob rompra ses mottes.
Efraimu ni ndama mwenye mafunzo ambayo anapenda kupura nafaka, hivyo nitaweka jozi juu ya shingo yake nzuri. Efraimu nitauweka jozi; Yuda ataimea; Yakobo atauvuta pigo kwa nafsi yake.
12 Semez-vous à la justice, et vous moissonnerez selon la gratuité; rompez les mottes de terre; car il est temps de rechercher l'Eternel, jusqu'à ce qu'il vienne, et fasse pleuvoir sur vous la justice.
Jifanyieni haki, vuneni matunda ya uaminifu wa agano. Chimbueni ardhi yenu isiyopandwa, kwa maana ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuinua haki juu yenu.
13 Vous avez labouré la méchanceté, et vous avez moissonné la perversité; vous avez mangé le fruit du mensonge, parce que tu as eu confiance en tes voies, à cause de la multitude de tes hommes forts.
Mmelima uovu; mmevuna udhalimu. Mmekula matunda ya udanganyifu kwa sababu uliamini katika mipango yako na katika askari wako wengi.
14 C'est pourquoi un tumulte s'élèvera parmi ton peuple, et on saccagera toutes tes forteresses, comme Salman saccagea Beth-Abel au jour de la bataille, [où] la mère fut écrasée sur les enfants.
Kwa hiyo mlipuko wa vita utafufuka kati ya watu wako, na miji yako yote yenye ngome itaharibiwa. Itakuwa kama Shalmani aliharibu Beth Arbeli siku ya vita, wakati mama alivunjika vipande vipande na watoto wake.
15 Béthel vous fera de même, à cause de la malice de votre méchanceté; le Roi d'Israël sera entièrement exterminé au point du jour.
Kwa hiyo itakuwa kwako, Betheli, kwa sababu ya uovu wako mkubwa. Wakati wa mchana mfalme wa Israeli atakatwa kabisa.