< Ézéchiel 31 >

1 Il arriva aussi en la onzième année, au premier jour du troisième mois, que la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
2 Fils d'homme, dis à Pharaon Roi d'Egypte, et à la multitude de son peuple: A qui ressembles-tu dans ta grandeur?
“Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake ya wajeuri: “‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
3 Voici, le Roi d'Assyrie a été tel qu'est un cèdre au Liban, ayant de belles branches, et des rameaux qui faisaient une grande ombre, et qui étaient d'une grande hauteur; sa cime a été fort touffue.
Angalia Ashuru, wakati fulani ilikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri ukitia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
4 Les eaux l'ont fait croître, l'abîme l'a fait monter fort haut, ses fleuves ont coulé autour de ses plantes, et il a envoyé les conduits de ses eaux vers tous les arbres des champs.
Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
5 C'est pourquoi sa hauteur s'est élevée par dessus tous les [autres] arbres des champs, ses branches ont été multipliées, et ses rameaux sont devenus longs par les grandes eaux, lorsqu'il poussait ses branches.
Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
6 Tous les oiseaux des cieux ont fait leurs nids dans ses branches, et toutes les bêtes des champs ont fait leurs petits sous ses rameaux, et toutes les grandes nations ont habité sous son ombre.
Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
7 Il était donc devenu beau dans sa grandeur, [et] dans l'étendue de ses branches, parce que sa racine était sur de grandes eaux.
Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake ilikwenda chini mpaka kwenye maji mengi.
8 Les cèdres qui étaient au Jardin de Dieu ne lui ôtaient rien de son lustre; les sapins n'étaient point pareils à ses branches, et les châtaigniers n'égalaient point [l'étendue] de ses rameaux; tous les arbres qui étaient au Jardin de Dieu n'ont point été pareils à lui en sa beauté.
Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
9 Je l'avais fait beau dans la multitude de ses rameaux, tellement que tous les arbres d'Héden, qui étaient au Jardin de Dieu, lui portaient envie.
Niliufanya kuwa mzuri ukiwa na matawi mengi, ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
10 C'est pourquoi le Seigneur l'Eternel dit ainsi: parce que tu t'es élevé en hauteur, [comme celui-là], qui avait sa cime toute touffue, a élevé son cœur dans sa hauteur;
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
11 Et je l'ai livré entre les mains du [plus] fort d'entre les nations, qui l'a traité comme il fallait, [et] je l'ai chassé à cause de sa méchanceté.
niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye aushughulikie sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
12 Et les étrangers les plus terribles d'entre les nations l'ont coupé, et l'ont laissé là, et ses branches sont tombées sur les montagnes, et sur toutes les vallées; et ses rameaux se sont rompus dans tous les cours [des eaux] de la terre, et tous les peuples de la terre se sont retirés de dessous son ombre, et l'ont laissé là.
nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kwenye kivuli chake na kuuacha.
13 Tous les oiseaux des cieux se sont tenus sur ses ruines, et toutes les bêtes des champs se sont retirées vers ses rameaux.
Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
14 C'est pourquoi aucun arbre arrosé d'eaux ne s'élève de sa hauteur, et ne produit de cime touffue, et les plus forts d'entre eux, même de tous ceux qui hument l'eau, ne subsistent point dans leur hauteur; car eux tous sont livrés à la mort dans la terre basse parmi les enfants des hommes, avec ceux qui descendent en la fosse.
Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale waendao shimoni.
15 Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: le jour qu'il descendit au sépulcre, je fis mener deuil [sur lui], je couvris l'abîme devant lui, et j'empêchai ses fleuves de couler, et les grosses eaux furent retenues; je fis que le Liban fut en deuil à cause de lui, et tous les arbres des champs en furent fatigués. (Sheol h7585)
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol h7585)
16 J'ébranlai les nations par le bruit de sa ruine, quand je le fis descendre au sépulcre, avec ceux qui descendent dans la fosse; et tous les arbres d'Héden, l'élite et le meilleur du Liban, tous humant l'eau, furent rendus contents au bas de la terre. (Sheol h7585)
Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol h7585)
17 Eux aussi sont descendus avec lui au sépulcre, vers ceux qui ont été tués par l'épée, et son bras, [c'est-à-dire], ceux qui habitaient sous son ombre parmi les nations, [y sont aussi descendus]. (Sheol h7585)
Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol h7585)
18 A qui donc as-tu ressemblé en gloire et en grandeur entre les arbres d'Héden? et pourtant tu seras jeté bas avec les arbres d'Héden dans les lieux profonds de la terre, tu seras gisant au milieu des incirconcis, avec ceux qui ont été tués par l'épée. C'est ici Pharaon, et toute la multitude de son peuple, dit le Seigneur l'Eternel.
“‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni mpaka kuzimu, utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri, asema Bwana Mwenyezi.’” (questioned)

< Ézéchiel 31 >