< Ézéchiel 27 >

1 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Toi donc, fils d'homme, prononce à haute voix une complainte sur Tyr;
“Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
3 Et dis à Tyr: Toi qui demeures aux avenues de la mer, qui fais métier de revendre aux peuples en plusieurs Iles; ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: Tyr, tu as dit: je suis parfaite en beauté.
na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
4 Tes confins [sont] au cœur de la mer, ceux qui t'ont bâtie t'ont rendue parfaite en beauté.
Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
5 Ils t'ont bâti tous les côtés [des navires] de sapins de Senir; ils ont pris les cèdres du Liban pour te faire des mâts.
Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
6 Ils ont fait tes rames de chênes de Basan, et la troupe des Assyriens a fait tes bancs d'ivoire, apporté des Iles de Kittim.
Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
7 Le fin lin d'Egypte, travaillé en broderie, a été ce que tu étendais pour te servir de voiles; ce dont tu te couvrais était la pourpre et l'écarlate des Iles d'Elisa.
Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
8 Les habitants de Sidon et d'Arvad ont été tes matelots; ô Tyr! tes sages [qui] étaient au dedans de toi ont été tes pilotes.
Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
9 Les anciens de Guébal, et ses [hommes] experts ont été parmi toi, réparant tes brèches; tous les navires de la mer, et leurs mariniers, ont été au dedans de toi, pour trafiquer avec toi de ton trafic.
Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
10 Ceux de Perse, et de Lud, et de Put ont été au dedans de toi pour être tes gens de guerre; ils ont pendu chez toi le bouclier et le casque; ils t'ont rendue magnifique.
Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
11 Les enfants d'Arvad avec tes troupes ont été sur tes murailles tout à l'entour, et ceux de Gammad ont été dans tes tours; ils ont pendu leurs boucliers sur tes murailles à l'entour, ils ont achevé de te rendre parfaite en beauté.
Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
12 Ceux de Tarsis ont trafiqué avec toi de toutes sortes de richesses, faisant valoir tes foires en argent, en fer, en étain et en plomb.
Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
13 Javan, Tubal, et Mésec ont été tes facteurs, faisant valoir ton commerce en hommes, et en vaisseaux d'airain.
Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
14 Ceux de la maison de Thogarma ont fait valoir tes foires en chevaux, et en cavaliers, et en mulets.
Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
15 Les enfants de Dédan ont été tes facteurs; tu avais en ta main le commerce de plusieurs Iles; et on t'a rendu en échange des dents d'ivoire, et de l'ébène.
Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
16 La Syrie a trafiqué avec toi; en quantité d'ouvrages faits pour toi; on a fait valoir tes foires en escarboucles, en écarlate, en broderie, en fin lin, en corail, et en agate.
Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
17 Juda et le pays d'Israël ont été tes facteurs, faisant valoir ton commerce en blé de Minnith et de Pannag, en miel, en huile, et en baume.
Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
18 Damas a trafiqué avec toi en quantité d'ouvrages faits pour toi en toute sorte de richesses, en vin de Helbon, et en laine blanche.
Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
19 Et Dan, et Javan et Mosel, ont fait valoir tes foires en fer luisant; la casse et le roseau [aromatique] ont été dans ton commerce.
Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
20 Ceux de Dédan ont été tes facteurs en draps précieux pour les chariots.
Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
21 Les Arabes, et tous les principaux de Kédar, ont été des marchands [que tu avais] en ta main, trafiquant avec toi en agneaux, en moutons, et en boucs.
Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 Les marchands de Séba et de Rahma ont été tes facteurs, faisant valoir tes foires en toutes sortes de drogues les plus exquises, et en toute sorte de pierres précieuses, et en or.
Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
23 Haran, et Canne, et Héden, ont fait trafic de ce qui venait de Séba; et l'Assyrie a appris ton trafic.
Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
24 Ceux-ci ont été tes facteurs en toutes sortes de choses, en draps de pourpre et de broderie, et en des caisses pour des vêtements précieux, en cordons entortillés; même les coffres de cèdre ont été dans ton trafic.
Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
25 Les navires de Tarsis t'ont célébrée dans leurs chansons à cause de ton commerce, et tu as été remplie et rendue fort glorieuse, [bâtie] au cœur de la mer.
Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
26 Tes matelots t'ont amenée en de grosses eaux, le vent d'Orient t'a brisée au cœur de la mer.
Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
27 Tes richesses, et tes foires, ton commerce, tes mariniers, et tes pilotes, ceux qui réparaient tes brèches, et ceux qui avaient le soin de ton commerce, tous tes gens de guerre qui étaient au dedans de toi, et toute ta multitude qui est au milieu de toi, tomberont dans le cœur de la mer au jour de ta ruine.
Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
28 Les faubourgs trembleront au bruit du cri de tes pilotes.
Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
29 Et tous ceux qui manient la rame descendront de leurs navires, les mariniers, [et] tous les pilotes de la mer; ils se tiendront sur la terre;
Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
30 Et feront ouïr sur toi leur voix, et crieront amèrement; ils jetteront de la poudre sur leurs têtes, [et] se vautreront dans la cendre;
Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
31 Ils arracheront leurs cheveux, et rendront leur tête chauve à cause de toi, ils se ceindront de sacs, et te pleureront avec amertume d'esprit, en menant deuil amèrement.
Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
32 Et ils prononceront à haute voix sur toi une complainte dans leur lamentation, et feront leur complainte sur toi, [en disant]: qui [fut jamais] telle que Tyr, telle que celle qui a été détruite au cœur de la mer?
Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
33 Tu as rassasié plusieurs peuples par la traite des marchandises qu'on apportait de tes foires au delà des mers; et tu as enrichi les Rois de la terre par la grandeur de tes richesses et de ton commerce.
Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
34 [Mais] quand tu as été brisée par la mer au fond des eaux, ton commerce et toute ta multitude sont tombés avec toi.
Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
35 Tous les habitants des Iles ont été désolés à cause de toi; et leurs Rois ont été horriblement épouvantés, et leur visage en a pâli.
Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
36 Les marchands d'entre les peuples t'ont insulté, tu es cause qu'on est tout étonné de ce que tu ne seras plus à jamais.
Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”

< Ézéchiel 27 >