< Ézéchiel 26 >

1 Et il arriva en l'onzième année, le premier jour du mois, que la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d'homme, parce que Tyr a dit touchant Jérusalem: ha! ha! celle qui était la porte des peuples a été rompue, elle s'est réfugiée chez moi, je serai remplie [parce] qu'elle a été rendue déserte.
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 A cause de cela ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici, j'en veux à toi, Tyr, et je ferai monter contre toi plusieurs nations, comme la mer fait monter ses flots.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Et elles détruiront les murailles de Tyr, et démoliront ses tours; je raclerai sa poudre, et la rendrai semblable à une pierre sèche.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Elle servira à étendre les filets au milieu de la mer; car j'ai parlé, dit le Seigneur l'Eternel, et elle sera en pillage aux nations.
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 Et les villes de son ressort, qui sont à la campagne, seront mises au fil de l'épée, et elles sauront que je suis l'Eternel.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 Car ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici je m'en vais faire venir de l'Aquilon contre Tyr, Nébucadnetsar, Roi de Babylone, le Roi des Rois, avec des chevaux, et des chariots, et des gens de cheval, et un grand peuple assemblé de toutes parts.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Il mettra au fil de l'épée les villes de ton ressort qui sont à la campagne, il fera des forts contre toi, il dressera des terrasses contre toi, et il lèvera les boucliers contre toi.
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 Et il posera ses machines de guerre contre tes murailles, et démolira tes tours avec ses marteaux.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 La poussière de ses chevaux te couvrira à cause de leur multitude; tes murailles trembleront du bruit des gens de cheval, des charrettes, et des chariots, quand il entrera par tes portes, comme on entre dans une ville à laquelle on a fait brèche.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 Il foulera toutes tes rues avec la corne des pieds de ses chevaux; il tuera ton peuple avec l'épée, et les trophées de ta force tomberont par terre.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Puis ils butineront tes biens, et pilleront ta marchandise; ils ruineront tes murailles, et démoliront tes maisons de plaisance; et ils mettront tes pierres et ton bois et ta poussière au milieu des eaux.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Et je ferai cesser le bruit de tes chansons, et le son de tes harpes ne sera plus ouï.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Je te rendrai semblable à une pierre sèche; elle sera un lieu pour étendre les filets, et elle ne sera plus rebâtie, parce que moi l'Eternel j'ai parlé, dit le Seigneur l'Eternel.
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel à Tyr: les Iles ne trembleront-elles pas du bruit de ta ruine, quand ceux qui seront blessés à mort gémiront, quand le carnage se fera au milieu de toi?
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Tous les Princes de la mer descendront de leurs sièges, et ôteront leurs manteaux, et dépouilleront leurs vêtements de broderie, et se vêtiront de frayeur; ils s'assiéront sur la terre, et ils seront effrayés de moment en moment, et seront désolés à cause de toi.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Et ils prononceront à haute voix une complainte sur toi, et te diront: comment as-tu péri, toi qui étais fréquentée par ceux qui vont sur la mer, ville renommée, qui étais forte en la mer, toi et tes habitants, qui se sont fait redouter à tous ceux qui habitent en elle?
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Maintenant les Iles seront effrayées au jour de ta ruine, et les Iles qui [sont] en la mer seront étonnées à cause de ta fuite.
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 Car ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: quand je t'aurai rendue une ville désolée, comme sont les villes qui ne sont point habitées, quand j'aurai fait tomber sur toi l'abîme, et que les grosses eaux t'auront couverte;
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 Alors je te ferai descendre avec ceux qui descendent en la fosse, vers le peuple d'autrefois, et je te placerai aux lieux les plus bas de la terre, aux endroits désolés depuis longtemps, avec ceux qui descendent en la fosse, afin que tu ne sois plus habitée; mais je remettrai la noblesse parmi la terre des vivants.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Je ferai qu'on sera tout étonné à cause de toi, de ce que tu n'es plus; et quand on te cherchera, on ne te trouvera plus à jamais, dit le Seigneur l'Eternel.
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 26 >