< Ézéchiel 20 >
1 Or il arriva la septième année, au dixième jour du cinquième mois, que quelques-uns des Anciens d'Israël vinrent pour consulter l'Eternel, et s'assirent devant moi.
Ikawa ikaja katika mwaka wa saba, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wa Israeli wakaja kumuuliza Yahwe na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
3 Fils d'homme, parle aux Anciens d'Israël, et leur dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: est-ce pour me consulter que vous venez? Je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, si vous me consultez.
“mwanadamu, tangaza kwa wazee wa Israeli na uwaambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Mmekuja kuniuliza swali? Kama niishivyo, sitaulizwa swali na ninyi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
4 Ne les jugeras-tu pas, ne les jugeras-tu pas, fils d'homme? donne-leur à connaître les abominations de leurs pères.
Je! Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu? Wajulishe kuhusu machukizo ya baba zao.
5 Et leur dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: le jour que j'élus Israël, et que je levai ma main à la postérité de la maison de Jacob, et que je me donnai à connaître à eux au pays d'Egypte, et que je leur levai ma main, en disant: Je suis l'Eternel votre Dieu.
Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyoichagua Israeli na kuinua mkono wangu kuapa kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo, na kufanya kujulikana mimi mwenyewe kwao katika nchi ya Misri, wakati nilipoinua mkono wangu kuapa kiapo kwao. Nalisema, “Mimi ni Yahwe Mungu wenu”-
6 En ce jour-là même je leur levai ma main, que je les tirerais hors du pays d'Egypte, pour les amener au pays que j'avais découvert pour eux, pays découlant de lait et de miel, et qui est la noblesse de tous les pays.
siku hiyo niliinua mkono wangu kuapa kiapo kwa ajili yao kwamba nitawatoa kutoka nchi ya Misri kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimeichagua kwa umakini kwa ajili yao. Ilikuwa ikitiririka maziwa na asali; ilikuwa nzuri sana utukufu miongoni mwa nchi mbali mbali.
7 Alors je leur dis: que chacun de vous rejette de devant ses yeux les abominations, et ne vous souillez point par les idoles d'Egypte; je suis l'Eternel votre Dieu.
Nikawaambia, “Kila mtu atupilie mabli mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake na sanamu za Misri. Msijitie unajisi; mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
8 Mais ils se rebellèrent contre moi, et ils n'agréèrent point de m'écouter; pas un d'eux ne rejeta de devant ses yeux les abominations, ni ne quitta les idoles d'Egypte; et je dis que je répandrais ma fureur sur eux, [et] que je consommerais ma colère sur eux au pays d'Egypte.
Lakini wameasi juu yangu hawakuwa tayari kunisikiliza. Kila mtu hakutupilia mbali mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake wala kwa ajili ya sanamu za Misri, hivyo nikaona nimwage ghadhabu yangu juu yao kukamilisha hasira yangu miongoni mwao katikati ya nchi ya Misri.
9 Mais ce que je les ai tirés hors du pays d'Egypte, je l'ai fait pour l'amour de mon Nom, afin qu'il ne fût point profané en la présence des nations parmi lesquelles ils étaient, et en la présence desquelles je m'étais donné à connaître à eux.
Nilifanya kwa ajili ya jina langu ili lisinajisiwe katika macho ya mataifa ambao walikaa pamoja nao. Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao, katika macho yao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.
10 Je les tirai donc hors du pays d'Egypte, et les amenai au désert.
Basi nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta kwenye jangwa.
11 Et je leur donnai mes statuts, et leur fis connaître mes ordonnances, lesquelles si l'homme accomplit, il vivra par elles.
Kisha nikawapa amri zangu na kufanya maagizo yangu kujulikana kwao, kwa kila mwanadamu atakayezishika ataishi.
12 Je leur donnai aussi mes Sabbats, pour être un signe entre moi et eux, afin qu'ils connussent que je suis l'Eternel qui les sanctifie.
Pia nikawapatia Sabato zangu kama ishara kati yangu na wao, ili wajue kwamba mimi ni Yahwe niwafanyao wawe watakatifu.
13 Mais ceux de la maison d'Israël se rebellèrent contre moi au désert, ils ne marchèrent point dans mes statuts, mais ils rejetèrent mes ordonnances; lesquelles si l'homme accomplit il vivra par elles; et ils profanèrent extrêmement mes Sabbats; c'est pourquoi je dis que je répandrais sur eux ma fureur au désert pour les consumer.
Lakini nyumba ya Israeli imeasi dhidi yangu jangwani. Hawakuenenda katika amri zangu; badala yake, wameyakataa maagizo yangu, ambayo mwanadamu ataishi kama akiyatii. Wamezinajisi Sabato zangu sana, basi nikasema nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani ili kuwamalliza.
14 Et je l'ai fait pour l'amour de mon Nom, afin qu'il ne fût point profané devant les nations, en la présence desquelles je les avais tirés [d'Egypte].
Lakini nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao kutoka Misri.
15 Et même je leur levai ma main au désert que je ne les amènerais point au pays que je [leur] avais donné, pays découlant de lait et de miel, [et] qui est la noblesse de tous les pays.
Basi mimi mwenyewe pia nimeinua mkono wangu kuapa kiapo kwao jangwani sitawarudisha kwenye nchi ile niliyokuwa naenda kuwapatia, nchi inayotiririkayo maziwa na asali, ambayo ilikuwa nzuri sana ambayo ni nzuri kati ya nchi zote.
16 Parce qu'ils avaient rejeté mes ordonnances, qu'ils n'avaient point marché dans mes statuts, et qu'ils avaient profané mes Sabbats; car leur cœur marchait après leurs idoles.
Nimeapa hivi kwa sababu walikataa maagizo yangu na kutotembea katika amri zangu, na wazikufuru Sabato zangu.
17 Toutefois mon œil les épargna pour ne les détruire point, et je ne les consumai point entièrement au désert.
Lakini jicho langu likawahurumia kutokana na uharibifu na sikuwaangamiza jangwani.
18 Mais je dis à leurs enfants au désert: ne marchez point dans les statuts de vos pères, et ne gardez point leurs ordonnances, et ne vous souillez point par leurs idoles.
Nikawaambia watoto wao jangwani, “Msitembee kutokana na amri za wazazi wenu; msiweke maagizo yao au kujinajisi wenyewe kwa sanamu.
19 Je suis l'Eternel votre Dieu; marchez dans mes statuts, et gardez mes ordonnances, et les faites.
Mimi ni Yahwe Mungu wenu, tembeeni katika amri zangu; tunzeni maagizo yangu na kuyatii.
20 Sanctifiez mes Sabbats, et ils seront un signe entre moi et vous, afin que vous connaissiez que je suis l'Eternel votre Dieu.
Zitunzeni Sabato zangu takatifu ili kwamba zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, hivyo basi mtajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
21 Mais les enfants se rebellèrent aussi contre moi, et ils ne marchèrent point dans mes statuts, et ne gardèrent point mes ordonnances pour les faire; lesquelles si l'homme accomplit, il vivra par elles; et ils profanèrent mes Sabbats; c'est pourquoi je dis que je répandrais ma fureur sur eux, [et] que je consommerais ma colère sur eux au désert.
Lakini watoto wao waliniasi. Hawakutembea kwenye sheria zangu au kushika maagizo yangu, ambazo mwanadamu ataishi kama akizitii. Wamezinajisi Sabato zangu, hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu dhidi yao katika jangwa.
22 Toutefois je retirai ma main, et je le fis pour l'amour de mon Nom, afin qu'il ne fût point profané devant les nations, en la présence desquelles je les avais tirés [d'Egypte].
Lakini niliurudisha mkono wangu na kutenda kwa ajili ya jina langu, hivyo lisitiwe unajisi katika macho ya mataifa ambao mbele ya macho yao niliwatoa Waisraeli.
23 Et néanmoins je leur levai ma main au désert, que je les répandrais parmi les nations, et que je les disperserais dans les pays.
Mimi mwenyewe pia nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali.
24 Parce qu'ils n'avaient point accompli mes ordonnances, et qu'ils avaient rejeté mes statuts, et profané mes Sabbats, et que leurs yeux étaient attachés aux idoles de leurs pères,
Nimeamua kufanya hivi kwa kuwa hawakuzitii amri zangu, na tangu walipo zikataa sheria zangu na kuzinajisi Sabato zangu. Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao.
25 A cause de cela je leur ai donné des statuts [qui n'étaient] pas bons, et des ordonnances par lesquelles ils ne vivraient point.
Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo.
26 Et je les ai souillés en leurs dons, en ce qu'ils ont fait passer [par le feu] tous les premiers-nés, afin que je les misse en désolation, [et] afin que l'on connût que je suis l'Eternel.
Nikawafanya unajisi kwa zawadi zao wakati walipofanya dhabihu za kila limbuko la tumbo la uzazi na kutupa kwenye moto. Nalifanya hivi ili kuwaogofya hivyo wangeweza kujua kwamba mimi ni Yahwe!'
27 C'est pourquoi, toi fils d'homme, parle à la maison d'Israël, et leur dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: vos pères m'ont encore outragé, en ce qu'ils ont commis un tel crime contre moi;
Kwa hiyo, mwanadamu, waambie nyumba ya Israeli na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika hili pia baba zenu walinikufuru wakati walipokuwa sio waaminifu kwangu.
28 C'est que les ayant introduits au pays, touchant lequel j'avais levé ma main pour le leur donner, ils ont regardé toute haute colline, et tout arbre branchu, et ils y ont fait leurs sacrifices, ils y ont posé leur oblation pour m'irriter, ils y ont mis leurs parfums, et ils y ont répandu leurs aspersions.
Wakati nilipowaleta kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimewaapia kuwapatia, na kisha popote walipoona jiwe lolote refu na mti wenye majani, walitoa sadaka zao, walinikasirisha kwa sadaka zao, na huko pia walichoma ubani wao wa kunukia na kumwaga sadaka zao za kinywaji.
29 Et je leur ai dit: que veulent dire ces hauts lieux auxquels vous allez? et toutefois leur nom a été appelé hauts lieux jusqu'à ce jour.
Kisha nikawaambia, “Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko?” Hivyo jina lake linaitwa Bana hata leo.'
30 C'est pourquoi dis à la maison d'Israël: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: ne vous souillez-vous pas dans le train de vos pères, et ne vous prostituez-vous point à leurs idoles abominables?
Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Kwa nini unajinajisi mwenyewe kwa njia za baba zako? Kwahiyo kwa nini unatenda kama makahaba, kutafuta kwa ajili ya mambo ya machukizo?
31 Et en offrant vos dons, quand vous faites passer vos enfants par le feu; vous vous souillez par toutes vos idoles jusqu'à ce jour. Est-ce ainsi que vous me consultez, ô maison d'Israël? Je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, que vous ne me consultez point.
Kwa kuwa wakati mtoapo zawadi zenu na kuwaweka watoto wenu kwenye moto, siku hii mnajitia unajisi pamoja na sanamu zenu zote. Kwa hiyo kwa nini niwaache mniulize mimi, nyumba ya Israeli? Kama niishivyo-Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Sitawaacha mniulize swali.
32 Et ce que vous pensez n'arrivera nullement, en ce que vous dites: nous serons comme les nations, et comme les familles des pays, en servant le bois et la pierre.
Mawazo yanayoumbika kwenye moyo wako hayatatokea kamwe. Mmesema, “Ngoja tuwe kama mataifa mengine, kama koo za nchi nyingine waabuduo mti na jiwe.”
33 Je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, si je ne règne sur vous avec une main forte, et un bras étendu, et avec effusion de colère.
Kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Nitatawala hakika juu yenu kwa mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa, na ghadhabu itakayomwagwa juu yenu.
34 Et si je ne vous tire d'entre les peuples, et ne vous rassemble hors des pays dans lesquels vous aurez été dispersés avec une main forte, et un bras étendu et avec effusion de colère.
Nitawatoa kutoka kwa watu wengine na kuwakusanya kutoka kwenye nchi mlizotawanyika ndani mwao. Nitafanya hivi kwa mkono hodari na kwa ghadhabu iliyomwagika.
35 Et si je ne vous fais venir au désert des peuples, et si je ne conteste là contre vous, face à face.
Kisha nitawaleta kwenye jangwa la watu, na huko nitawahukumu uso kwa uso.
36 Comme j'ai contesté contre vos pères au désert du pays d'Egypte, ainsi contesterai-je contre vous, dit le Seigneur l'Eternel.
Kama nilivyo wahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, hivyo pia nitawahukumu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
37 Et je vous ferai passer sous la verge, et vous ramènerai au lieu de l'alliance.
Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, na nitawafanya kutii maagizo yangu ya agano.
38 Et je mettrai à part d'entre vous les rebelles, et ceux qui se révoltent contre moi; [et] je les ferai sortir du pays auquel ils séjournent, mais ils n'entreront point en la terre d'Israël; et vous saurez que je suis l'Eternel.
Nitawasafisha kutoka miongoni mwenu maasi na wale ambao walionichukiza. Nitawatoa kutoka nchi ambayo wanayoishi kama wageni, lakini hawataingia kwenye nchi ya Israeli. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
39 Vous donc, ô maison d'Israël! ainsi a dit le Seigneur l'Eternel, allez, servez chacun vos idoles, même puisque vous ne me voulez pas écouter; aussi ne profanerez-vous plus le Nom de ma sainteté par vos dons, et par vos idoles.
Basi kwenu, nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Kila mmoja wenu ataenda kwa sanamu zake mwenyewe. Muwaabudu kama mtakataa kunisikiliza, lakini hamtalikufuru tena jina langu takatifu kwa zawadi zenu na sanamu zenu.
40 Mais ce sera en ma sainte montagne, en la haute montagne d'Israël, dit le Seigneur l'Eternel, que toute la maison d'Israël me servira, dans toute cette terre; je prendrai là plaisir en eux, et là je demanderai vos offrandes élevées, et les prémices de vos dons, avec toutes vos choses sanctifiées.
Kwa kuwa juu ya mlima wangu mtakatifu, juu ya kilele cha mlima wa Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-wote wa nyumba ya Israeli mtaniabudu huko katika nchi. Nitabarikiwa kwa kutaka sadaka zenu huko, na pia malimbuko yenu ya shukrani pamoja na vitu vyenu vyote vitakatifu.
41 Je prendrai plaisir en vous par vos agréables odeurs, quand je vous aurai retirés d'entre les peuples, et que je vous aurai rassemblés des pays dans lesquels vous aurez été dispersés; et je serai sanctifié en vous, les nations le voyant.
Nitawapokea kama harufu nzuri ya ubani wakati nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika. Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone.
42 Et vous saurez que je suis l'Eternel, quand je vous aurai fait revenir en la terre d'Israël, qui est le pays touchant lequel j'ai levé ma main pour le donner à vos pères.
Kisha, wakati nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, kwenye nchi ambayo niliuinulia mkono wangu kuapa kuwapatia baba zenu, mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
43 Et là vous vous souviendrez de vos voies, et de toutes vos actions, par lesquelles vous vous êtes souillés; et vous vous déplairez en vous-mêmes de tous vos maux que vous aurez faits.
Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya huko, na matendo yenu yote machafu mliyoyafanya wenyewe, na mtajichukia wenyewe katika macho yenu kwa matendo yenu yote maovu mliyoyafanya.
44 Et vous saurez que je suis l'Eternel, par tout ce que j'aurai fait envers vous, à cause de mon Nom, et non pas selon vos méchantes voies, et vos actions corrompues, ô maison d'Israël! dit le Seigneur l'Eternel.
Hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe nifanyapo haya kwenu kwa ajili ya jina langu, sio kwa njia zenu mbaya au matendo yenu mabovu, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
45 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
46 Fils d'homme, tourne ta face vers le chemin de Théman, et fais découler [ta parole] vers le Midi, et prophétise contre la forêt du champ du Midi.
“Mwanadamu, weka uso wako kuelekea nchi za kusini, na kuongea juu ya kusini; tabiri juu ya msitu wa Negebu.
47 Et dis à la forêt du Midi: écoute la parole de l'Eternel. Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici, je m'en vais allumer au dedans de toi un feu qui consumera tout bois vert et tout bois sec au dedans de toi; la flamme de l'embrasement ne s'éteindra point, et tout le dessus en sera brûlé, depuis le Midi jusqu'au Septentrion.
Uuambie msitu wa Negebu, 'Hivi ndivyo Yahwe asemavyo-Bwana Yahwe asema hivi: Tazama, nitaweka moto ndani yako. Utakula kila mti mbichi na kila mti mkavu ndani yako. Miali ya moto haitazimika; na kila uso utokao kusini hata kaskazini utateketezwa kwa moto.
48 Et toute chair verra que moi l'Eternel j'y ai allumé le feu; [et] il ne s'éteindra point.
Kisha watu wote wenye mwili watajua yakwamba mimi ni Yahwe nimeuwasha moto, na hautazimika.”'
49 Et je dis: ha! ha! Seigneur Eternel, ils disent de moi: n'est-il pas vrai que celui-ci ne fait que mettre en avant des similitudes?
Kisha nimesema, Ee! Bwana Yahwe, Wananisema mimi, 'Je! yeye sio mwenye kusema mafumbo?”'