< Ézéchiel 12 >
1 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d'homme: tu demeures au milieu d'une maison rebelle, [au milieu de gens] qui ont des yeux pour voir, et ne voient point; et qui ont des oreilles pour ouïr, et n'entendent point; parce qu'ils [sont] une maison rebelle.
“Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
3 Toi donc, fils d'homme, fais-toi l'équipage d'un homme qui déloge, et déloge de jour, eux le voyant; déloge, dis-je, de ton lieu pour aller en un autre, eux le voyant; peut-être qu'ils y prendront garde; quoiqu'ils soient une maison rebelle.
“Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
4 Tu mettras donc dehors pendant le jour ton équipage, tel qu'est l'équipage d'un homme qui déloge, eux le voyant; et sur le soir tu sortiras, eux le voyant, comme quand on sort pour déloger.
Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
5 Perce-toi la paroi, eux le voyant, et tire par-là dehors [ton équipage].
Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
6 Tu [le] porteras sur l'épaule, eux le voyant, et tu [le] tireras dehors sur la brune; tu couvriras aussi ton visage, afin que tu ne voies point la terre; car je t'ai mis pour être un signe à la maison d'Israël.
Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
7 Je fis donc comme il m'avait été commandé: je portai dehors durant le jour mon équipage tel qu'est l'équipage d'un homme qui déloge, et sur le soir je me perçai la paroi avec la main, je le tirai dehors sur la brune, [et] le portai sur l'épaule, eux le voyant.
Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
8 Et au matin la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
9 Fils d'homme, la maison d'Israël, maison rebelle, ne t'a-t-elle pas dit: qu'est-ce que tu fais?
“Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
10 Dis-leur: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: Cet ordre dont je suis chargé s'adresse au Prince qui est dans Jérusalem, et à toute la maison d'Israël qui est parmi eux.
“Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
11 Dis: Je vous suis pour un signe; comme j'ai fait, ainsi il leur sera fait; ils délogeront pour s'en aller en captivité.
Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
12 Et le Prince qui est parmi eux, portera sur la brune [son équipage] sur l'épaule, et sortira; on lui percera la paroi pour le tirer par-là dehors; il couvrira son visage, afin qu'il ne voie point de ses yeux la terre.
“Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
13 J'étendrai mon rets sur lui, et il sera pris dans mes filets; et je le ferai entrer dans Babylone au pays des Caldéens, mais il ne la verra point, et il y mourra.
Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
14 Et je disperserai à tout vent tout ce qui est autour de lui, son secours, et toutes ses troupes; et je tirerai l'épée après eux.
Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
15 Et ils sauront que je suis l'Eternel, quand je les aurai répandus parmi les nations, et que je les aurai dispersés par les pays.
“Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
16 Et je laisserai de reste d'entre eux quelque peu de gens, [préservés] de l'épée, de la famine, et de la mortalité, afin qu'ils racontent toutes leurs abominations, parmi les nations vers lesquelles ils seront parvenus; et ils sauront que je suis l'Eternel.
Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
17 Puis la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
18 Fils d'homme, mange ton pain dans l'agitation, et bois ton eau en tremblant et avec inquiétude.
“Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
19 Puis tu diras au peuple du pays: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel touchant les habitants de Jérusalem, à la terre d'Israël: ils mangeront leur pain avec chagrin, et ils boiront leur eau avec frayeur, parce que son pays sera désolé, étant privé de son abondance, à cause de la violence de tous ceux qui y habitent.
Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
20 Et les villes peuplées seront désertes, et le pays ne sera que désolation; et vous saurez que je suis l'Eternel.
Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
21 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
22 Fils d'homme, quel est ce proverbe dont vous usez touchant la terre d'Israël, en disant: les jours seront prolongés, et toute vision périra?
“Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
23 C'est pourquoi dis-leur: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel, je ferai cesser ce proverbe, et on ne s'en servira plus pour proverbe en Israël; et dis-leur: les jours, et la parole de toute vision sont proches.
Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
24 Car il n'y aura plus désormais aucune vision de vanité, ni aucune divination de flatteur, au milieu de la maison d'Israël.
Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
25 Car moi l'Eternel, je parlerai, et la parole que j'aurai prononcée sera mise en exécution, elle ne sera plus différée; mais, ô maison rebelle! je prononcerai en vos jours la parole, et je l'exécuterai, dit le Seigneur l'Eternel.
Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
26 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
27 Fils d'homme, voici, ceux de la maison d'Israël disent: la vision que celui-ci voit n'arrivera pas de longtemps, et il prophétise pour des temps qui sont encore éloignés.
“Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
28 C'est pourquoi dis-leur: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: aucune de mes paroles ne sera plus différée, mais la parole que j'aurai prononcée sera exécutée [incessamment], dit le Seigneur l'Eternel.
“Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”