< Éphésiens 5 >

1 Soyez donc les imitateurs de Dieu, comme [ses] chers enfants;
Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
2 Et marchez dans la charité, ainsi que Christ aussi nous a aimés, et s'est donné lui-même pour nous en oblation et sacrifice à Dieu, en odeur de bonne senteur.
mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
3 Que ni la fornication, ni aucune souillure, ni l'avarice, ne soient pas même nommées parmi vous, ainsi qu’il est convenable à des Saints;
Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
4 Ni aucune chose déshonnête, ni parole folle, ni plaisanterie; car ce sont là des choses qui ne sont pas bienséantes; mais plutôt des actions de grâces.
Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
5 Car vous savez ceci, que nul fornicateur, ni impur, ni avare, qui est un idolâtre, n'a point d'héritage dans le Royaume de Christ, et de Dieu.
Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
6 Que personne ne vous séduise par de vains discours, car à cause de ces choses la colère de Dieu vient sur les rebelles.
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
7 Ne soyez donc point leurs associés.
Kwa hiyo, msishirikiane nao.
8 Car vous étiez autrefois ténèbres, mais maintenant vous êtes lumière au Seigneur; conduisez-vous [donc] comme des enfants de lumière.
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
9 Car le fruit de l'Esprit consiste en toute débonnaireté, justice et vérité.
(kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
10 Eprouvant ce qui est agréable au Seigneur.
nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
11 Et ne communiquez point aux œuvres infructueuses des ténèbres, mais au contraire reprenez-les.
Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
12 Car il est même déshonnête de dire les choses qu'ils font en secret.
Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
13 Mais toutes choses étant mises en évidence par la lumière, sont rendues manifestes; car la lumière est celle qui manifeste tout.
Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
14 C'est pourquoi il [est] dit: Réveille-toi, toi qui dors, et te relève d'entre les morts, et Christ t'éclairera.
kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
15 Prenez donc garde comment vous vous conduirez soigneusement, non point comme étant dépourvus de sagesse, mais comme étant sages:
Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
16 Rachetant le temps: car les jours sont mauvais.
mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
17 C'est pourquoi ne soyez point sans prudence, mais comprenez bien quelle est la volonté du Seigneur.
Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
18 Et ne vous enivrez point du vin auquel il y a de la dissolution; mais soyez remplis de l'Esprit.
Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
19 Vous entretenant par des Psaumes, des cantiques et des chansons spirituelles; chantant et psalmodiant de votre cœur au Seigneur.
Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
20 Rendant toujours grâces pour toutes choses au Nom de notre Seigneur Jésus-Christ [à notre] Dieu, et Père.
siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21 Vous soumettant les uns aux autres, en la crainte de Dieu.
Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
22 Femmes soyez soumises à vos maris, comme au Seigneur.
Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
23 Car le mari est le chef de la femme, comme Christ est le chef de l'Eglise, et il est aussi le Sauveur de [son] Corps.
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
24 Comme donc l'Eglise est soumise à Christ, que les femmes le soient de même à leurs maris, en toutes choses.
Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
25 [Et] vous maris, aimez vos femmes, comme Christ a aimé l'Eglise, et s'est donné lui-même pour elle.
Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
26 Afin qu'il la sanctifiât, après l’avoir nettoyée dans le baptême d'eau et par sa parole:
kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
27 Afin qu'il se la rendît une Eglise glorieuse, n'ayant ni tache, ni ride, ni autre chose semblable, mais afin qu'elle fût sainte et irrépréhensible.
apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
28 Les maris donc doivent aimer leurs femmes comme leurs propres corps; celui qui aime sa femme s'aime soi-même.
Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
29 Car personne n'a jamais eu en haine sa propre chair, mais il la nourrit et l'entretient, comme le Seigneur entretient l'Eglise.
Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
30 Car nous sommes membres de son corps, étant de sa chair, et de ses os.
Sisi tu viungo vya mwili wake.
31 C'est pourquoi l'homme laissera son père et sa mère, et il s'unira à sa femme, et les deux seront une même chair.
“Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
32 Ce mystère est grand, or je parle de Christ et de l'Eglise.
Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
33 Que chacun de vous aime donc sa femme comme soi-même; et que la femme révère son mari.
Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.

< Éphésiens 5 >