< Deutéronome 29 >
1 Ce sont ici les paroles de l'alliance que l'Eternel commanda à Moïse de traiter avec les enfants d'Israël, au pays de Moab, outre l'alliance qu'il avait traitée avec eux en Horeb.
Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
2 Moïse donc appela tout Israël, et leur dit: Vous avez vu tout ce que l'Eternel a fait en votre présence dans le pays d'Egypte, à Pharaon et à tous ses serviteurs, et à tout son pays.
Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
3 Les grandes épreuves que tes yeux ont vues, ces signes, et ces grands miracles.
mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
4 Mais l'Eternel ne vous a point donné un cœur pour entendre, ni des yeux pour voir, ni des oreilles pour entendre, jusqu'à aujourd'hui.
Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
5 Et je vous ai conduits durant quarante ans par le désert, sans que vos vêtements se soient envieillis sur vous, et sans que ton soulier ait été envieilli sur ton pied.
Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
6 Vous n'avez point mangé de pain, ni bu de vin, ni de cervoise, afin que vous connaissiez que je suis l'Eternel votre Dieu.
Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
7 Et vous êtes parvenus en ce lieu-ci, et Sihon, Roi de Hesbon, et Hog, Roi de Basan, sont sortis au devant de nous pour nous combattre, et nous les avons battus.
Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
8 Et avons pris leur pays, et l'avons donné en héritage aux Rubénites, aux Gadites, et à la demi Tribu de Manassé.
Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
9 Vous garderez donc les paroles de cette alliance, et vous les ferez, afin que vous prospériez dans tout ce que vous ferez.
Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
10 Vous comparaissez tous aujourd'hui devant l'Eternel votre Dieu, les chefs de vos Tribus, vos Anciens, vos Officiers, et tout homme d'Israël;
Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
11 Vos petits enfants, vos femmes, et ton étranger qui est au milieu de ton camp, depuis ton coupeur de bois jusqu'à ton puiseur d'eau;
watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
12 Afin que tu entres dans l'alliance de l'Eternel ton Dieu, laquelle il traite aujourd'hui avec toi, et dans l'exécration du serment qu'il te fait faire;
Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
13 Afin qu'il t'établisse aujourd'hui pour [être] son peuple, et qu'il te soit Dieu, ainsi qu'il t'a dit, et ainsi qu'il a juré à tes pères, Abraham, Isaac, et Jacob.
ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
14 Et ce n'est pas seulement avec vous que je traite cette alliance, et cette exécration du serment que vous faites;
Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
15 Mais c'est tant avec celui qui est ici avec nous aujourd'hui devant l'Eternel notre Dieu, qu'avec celui qui n'est point ici avec nous aujourd'hui.
pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
16 Car vous savez comment nous avons demeuré au pays d'Egypte, et comment nous avons passé chez les nations, parmi lesquelles vous avez passé.
Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
17 Et vous avez vu leurs abominations, et leurs dieux de fiente, [les dieux] de bois et de pierre, d'argent et d'or qui sont parmi eux.
Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
18 [Prenez garde] qu'il n'y ait parmi vous ni homme, ni femme, ni famille, ni Tribu qui détourne aujourd'hui son cœur de l'Eternel notre Dieu, pour aller servir les dieux de ces nations, [et] qu'il n'y ait parmi vous quelque racine qui produise du fiel et de l'absinthe.
Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
19 Et qu'il n'arrive que quelqu'un entendant les paroles de cette exécration du serment que vous faites, ne se bénisse en son cœur, en disant: J'aurai la paix, quoique je vive selon que je l'ai arrêté en mon cœur; afin d'ajouter l'ivrognerie à l'altération.
Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
20 L'Eternel refusera de lui pardonner; la colère de l'Eternel et sa jalousie s'enflammeront alors contre cet homme-là, et toute l'exécration du serment que vous faites, laquelle est écrite dans ce livre, demeurera sur lui, et l'Eternel effacera le nom de cet homme de dessous les cieux.
Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
21 Et l'Eternel le séparera de toutes les Tribus d'Israël pour son malheur, selon toutes les exécrations du serment de l'alliance qui est écrite dans ce livre de la Loi.
Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
22 Et la génération à venir, vos enfants qui viendront après vous, et le forain qui viendra d'un pays éloigné, diront lorsqu'ils verront les plaies de ce pays, et ses maladies, dont l'Eternel l'affligera;
Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
23 Et que toute la terre de ce pays-là ne sera que soufre, que sel, et qu'embrasement, qu'elle ne sera point semée, et qu'elle ne fera rien germer, et que nulle herbe n'en sortira, ainsi qu'en la subversion de Sodome, et de Gomorrhe, et d'Adma, et de Tséboïm, lesquelles l'Eternel détruisit en sa colère et en sa fureur;
na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
24 Même toutes les nations diront: Pourquoi l'Eternel a-t-il fait ainsi à ce pays? Quelle est l'ardeur de cette grande colère?
watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
25 Et on répondra: C'est à cause qu'ils ont abandonné l'alliance de l'Eternel le Dieu de leurs pères, laquelle il avait traitée avec eux quand il les fit sortir du pays d'Egypte.
Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
26 Car ils s'en sont allés, et ont servi d'autres dieux, et se sont prosternés devant eux, devant ces dieux qu'ils n'avaient point connus, et aucun desquels ne leur avait rien donné.
na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
27 A cause de cela la colère de l'Eternel s'est embrasée contre ce pays, pour faire venir sur lui toutes les malédictions écrites dans ce livre.
Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
28 Et l'Eternel les a arrachés de leur terre en sa colère, et en sa fureur, et en sa grande indignation, et les a chassés en un autre pays, comme [il paraît] aujourd'hui.
Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
29 Les choses cachées sont pour l'Eternel notre Dieu; mais les choses révélées sont pour nous et pour nos enfants à jamais, afin que nous fassions toutes les paroles de cette Loi.
Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.