< Deutéronome 19 >
1 Quand l'Eternel ton Dieu aura exterminé les nations desquelles l'Eternel ton Dieu te donne le pays, et que tu posséderas leur pays, et demeureras dans leurs villes, et dans leurs maisons;
Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao,
2 Alors tu sépareras trois villes au milieu du pays que l'Eternel ton Dieu te donne pour le posséder.
ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki.
3 Tu dresseras le chemin, et tu diviseras en trois parties les contrées de ton pays, que l'Eternel ton Dieu te donnera en héritage; et ce sera afin que tout meurtrier s'y enfuie.
Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.
4 Or voici comment on procédera envers le meurtrier qui se sera retiré là, afin qu'il vive. Celui qui aura frappé son prochain par mégarde, et sans l'avoir haï auparavant;
Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo.
5 Comme si quelqu'un étant allé avec son prochain dans une forêt pour couper du bois, et avançant sa main avec la cognée pour couper du bois, il arrive que le fer échappe hors du manche, et rencontre tellement son prochain, qu'il en meure; il s'enfuira dans une de ces villes-là, afin qu'il vive.
Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.
6 De peur que celui qui a le droit de venger le sang ne poursuive le meurtrier, pendant que son cœur est échauffé, et qu'il ne l'atteigne, si le chemin est trop long, et ne le frappe à mort, quoiqu'il ne fût pas digne de mort, parce qu'il ne haïssait pas son prochain auparavant.
Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia.
7 C'est pourquoi je te commande, en disant: Sépare-toi trois villes.
Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.
8 Que si l'Eternel ton Dieu étend tes limites, comme il l'a juré à tes pères, et qu'il te donne tout le pays qu'il a promis de donner à tes pères.
Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi,
9 Pourvu que tu prennes garde à faire tous ces commandements que je te prescris aujourd'hui, afin que tu aimes l'Eternel ton Dieu, et que tu marches toujours dans ses voies; alors tu t'ajouteras encore trois villes, outre ces trois-là;
kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi.
10 Afin que le sang de celui qui est innocent ne soit pas répandu au milieu de ton pays, que l'Eternel ton Dieu te donne [en] héritage, et que tu ne sois pas coupable de meurtre.
Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.
11 Mais quand un homme qui haïra son prochain, lui aura dressé des embûches, et se sera élevé contre lui, et l'aura frappé à mort, et qu'il s'en sera fui dans l'une de ces villes.
Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii,
12 Alors les Anciens de sa ville enverront et le tireront de là, et le livreront entre les mains de celui qui a le droit de venger le sang, afin qu'il meure.
wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua.
13 Ton œil ne l'épargnera point; mais tu vengeras en Israël le sang de l'innocent; et tu prospéreras.
Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.
14 Tu ne transporteras point les bornes de ton prochain que les prédécesseurs auront plantées dans l'héritage que tu posséderas, au pays que l'Eternel ton Dieu te donne pour le posséder.
Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.
15 Un témoin seul ne sera point valable contre un homme, en quelque crime et péché que ce soit, en quelque péché qu'on ait commis; mais sur la parole de deux ou de trois témoins la chose sera valable.
Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
16 Quand un faux témoin s'élèvera contre quelqu'un, pour déposer contre lui le crime de révolte;
Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu,
17 Alors ces deux hommes-là qui auront contestation entr'eux, comparaîtront devant l'Eternel, en la présence des Sacrificateurs et des Juges qui seront en ce temps-là;
watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo.
18 Et les Juges s'informeront exactement; et s'il se trouve que ce témoin soit un faux témoin, qui ait déposé faussement contre son frère;
Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake,
19 Tu lui feras comme il avait dessein de faire à son frère; et ainsi tu ôteras le méchant du milieu de toi.
basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.
20 Et les autres qui entendront cela craindront, et à l'avenir ils ne feront plus de méchante action comme celle-là, au milieu de toi.
Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu.
21 Ton œil ne l'épargnera point; mais il y aura vie pour vie, œil pour œil, dent pour dent, main pour main, pied pour pied.
Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.