< Colossiens 4 >
1 Maîtres, rendez le droit et l'équité à vos serviteurs, sachant que vous avez aussi un Seigneur dans les Cieux.
Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Persévérez dans la prière, veillant dans cet exercice avec des actions de grâces:
Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3 Priez aussi tous ensemble pour nous, afin que Dieu nous ouvre la porte de la parole, pour annoncer le mystère de Christ, pour lequel aussi je suis prisonnier.
Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4 Afin que je le manifeste selon qu'il faut que j'en parle.
Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5 Conduisez-vous sagement envers ceux de dehors, rachetant le temps.
Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6 Que votre parole soit toujours assaisonnée de sel avec grâce, afin que vous sachiez comment vous avez à répondre à chacun.
Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7 Tychique, notre frère bien-aimé, et fidèle Ministre, et compagnon de service en [notre]Seigneur, vous fera savoir tout mon état.
Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8 Je l'ai envoyé vers vous expressément, afin qu'il connaisse quel est votre état, et qu'il console vos cœurs;
Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9 Avec Onésime notre fidèle et bien-aimé frère, qui est des vôtres, ils vous avertiront de toutes les affaires de deçà.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10 Aristarque, qui est prisonnier avec moi, vous salue aussi, et Marc qui est le cousin de Barnabas, touchant lequel vous avez reçu un ordre: s'il vient à vous, recevez-le,
Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11 Et Jésus, appelé Juste, qui sont de la Circoncision; ceux-ci qui sont mes compagnons d'œuvre au Royaume de Dieu, sont [aussi] les seuls qui m'ont été en consolation.
Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12 Epaphras, qui est des vôtres, Serviteur de Christ, vous salue, combattant toujours pour vous par ses prières, afin que vous demeuriez parfaits et accomplis en toute la volonté de Dieu.
Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13 Car je lui rends témoignage qu'il a un grand zèle pour vous, et pour ceux de Laodicée, et pour ceux d'Hiérapolis.
Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14 Luc, le médecin bien-aimé, vous salue; et Démas aussi.
Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15 Saluez les frères qui sont à Laodicée, et Nymphas, avec l'Eglise qui est en sa maison.
Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16 Et quand cette Lettre aura été lue entre vous, faites qu'elle soit aussi lue dans l'Eglise des Laodiciens; et vous aussi lisez celle qui [est venue] de Laodicée.
Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17 Et dites à Archippe: prends garde à l'administration que tu as reçue en [notre] Seigneur, afin que tu l'accomplisses.
Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18 La salutation est de la propre main de moi Paul. Souvenez-vous de mes liens. Que la grâce soit avec vous! Amen!
Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.